Zitto Z. Kabwe,tafuta mshauri!

Zitto Z. Kabwe,tafuta mshauri!

Status
Not open for further replies.

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Ukiendelea hivi hautafanikiwa kamwe. Hautafika mbali.Utaishia njiani. Hutapata utakacho. Tafadhali tafuta Mshauri wako mbobezi wa mambo ya kisiasa ili awe anakushauri kabla ya kuamua. Bado hujitoshelezi kisiasa. Kweli kabisa. Labda kiuchumi-kwakuwa nawe ni mchumi.

Katika Mkutano wenu na Waandishi wa Habari juzi,hukupaswa kutaja tuhuma zote zilizojadiliwa ndani ya Kamati Kuu. Kutaja tuhuma zile ni kutoa siri za vikao nje na kujitetea pasipostahili. Sasa ulipojibu pale tuhuma moja baada ya nyingine ulikuwa unamjibu nani? Ili iweje? Kwa ajili ya kumbukumbu gani?

Ndugu Zitto, yawezekana unachokiamini kuwa una uwezo wa kuongoza chochote popote hapa nchini ni kweli. Lakini,imani yako isikuendeshe. Nenda nayo taratibu. Utafika tu! Ukiruhusu machagizo ya vyombo vya habari kukukimbiza mbio kuelekea unapopataka,utajikwaa;utaanguka na kuumia.

Siku ile, ungesema hivi tu: " Nayaheshimu Maamuzi ya chama changu. Nitayamaliza mambo haya kwa mujibu wa Katika na Kanuni za chama changu. Na kwasasa, sina mpango wa kuhama toka CHADEMA.Hatoki mtu hapa." Basi.Ungesubiri maswali na halafu uyajibu. Hapo, ungepata wasaa mzuri wa kuelezea kwa makini na uangalifu mkubwa mambo yako. Watu wangeshangaa.Wangekusifu. Kukosekana kwa Mshauri kumekufanya uongee mengi yenyemshiko haba.

Itoshe kusema kuwa, Zitto Zuberi Kabwe ni mwanasiasa. Bado yuko safarini.Safari ya mafanikio zaidi. Lakini,anapaswa kuwa makini.Aongee kwa kuchagua maneno;kuzingatia hadhira na kuuchuja ujumbe. Achangamane na wenzake chamani. Wawe kitu kimoja. Wasonge mbele. Lakini, Mshauri hakwepeki. Shauriwa kwanza;amua baadaye.

Kila la kheri katika siku zako 14 za utetezi. Yatakwisha tu haya. Wajibu waliokutuhumu. Sisi tunasubiri matokeo tu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Zitto Kabwe Akerwa na Siasa za Majungu CHADEMA


Posted by Jewajua Kweli at 31 October, at 08 : 51 A


NAIBU Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Zitto Kabwe, ameelezea kukerwa na siasa za majungu na vikao vinavyoishia kupigana ndani ya chama chake na badala yake amewataka viongozi wenzake kuelekeza nguvu kwa wanachama, kwani malumbano hayatakijenga chama.
Zitto, ambaye pia ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini, alitoa kauli hiyo jana, baada ya RAI Jumatano kutaka kujua msimamo wake kutokana na kuhusishwa kuwa nyuma ya usaliti anaodaiwa kuufanya Mwenyekiti wa chama hicho Mkoa wa Arusha, Samson Mwigamba.
Katika majibu yake hayo aliyoyatoa kwa njia ya mtandao, Zitto alisema wanaojaribu kumhusisha na suala la Mwigamba ni kawaida yao kupenda kumhusisha na mambo yasiyomhusu.
"Mwigamba ni Mwenyekiti wa chama wa Mkoa mwenye utashi wake wa kisiasa. Ana uwezo wa kusimama mwenyewe. Siyo kila mtu mwenye mawazo yake anatumika. Sasa hao wanaomtuhumu Mwigamba wao wanatumiwa na nani?" alihoji Zitto.
Kuhusu hoja kwamba sakata hilo la Mwigamba chanzo chake ni msuguano wa kuwania nafasi ya uenyekiti kati yake na Mbowe, Zitto alisema uchaguzi ndani ya chama haujatangazwa, kwa hiyo yeyote anayezungumzia kugombea au la anavunja kanuni za uchaguzi.
Katika hilo, Zitto alisema hahitaji mtu wa kumsemea, kwamba akihitaji uenyekiti wa chama atasema yeye mwenyewe.
"Nina sifa zote, siyo tu za kuongoza chama, bali kuongoza nchi. Nina elimu ya kutosha, nina rekodi ya kazi za kibunge kubwa kuliko wabunge takribani wote wa sasa, kwa miswada binafsi, hoja binafsi na hata kuibua masuala nyeti ya nchi.
"Uadilifu wangu hauna shaka, uzalendo wangu kwa nchi yangu ni wa kupigiwa mfano. Zaidi ya yote, najua kero za wananchi na changamoto zao. Sihitaji kusemewa na mtu. Nikitaka uenyekiti nitasimama mwenyewe," alisema Zitto.
Zitto alisema kitendo cha kutaka kumhusisha na masuala yanayoendelea ndani ya Chadema na kuhusu sakata zima la Mwigamba, ni kutaka kuhamisha mjadala na kumtoa kwenye ajenda ya kuwafuatilia watu wanaodaiwa kuficha mamilioni ya fedha nje ya nchi.
"Kwa sasa nina kazi ya kuhakikisha mafisadi na wahuni ‘criminals' walioficha fedha na mali nje ya nchi wanaibuliwa na kurejesha fedha hizo," alisisitiza Zitto.
Kuhusu madai ya kuchunguzwa na chama chake kama na yeye ni mmoja wa wasaliti, Zitto alisema kuwa hizo ni mbinu za kumuondoa kwenye kazi anayofanya ya kupambana na ufisadi.
"Wanajua nikishika jambo siachi mpaka mwisho, hivyo wanajaribu kutengeneza uongo wanaouita uchunguzi. Watanzania wasipumbazwe na vituko vya siasa vinavyoendelea. Tuendelee kudai Katiba Mpya na kupambana na ufisadi. Kwa Wanachadema tuendelee kujenga chama kwenye kanda zetu. Chama kitakachochukua dola ni kile chenye mtandao mpana kwenda vijijini," alisema.
Zitto aliwataka viongozi wenzake na wanachama wa Chadema kupunguza vikao vya majungu vinavyoishia kupigana na badala yake waende kwa wananchi wakafanye kazi, kwamba malumbano hayajengi chama.
Kwa upande mwingine, chama hicho kimeendelea kusisitiza kuwa madai yote yaliyotolewa na Mwigamba dhidi ya chama chao ni ya upotoshaji, uongo na ya kichonganishi.
Kwa mujibu wa tarifa iliyotolewa kwa vyombo vya habari na Ofisa Habari Mwandamizi wa chama hicho, Tumaini Makene, wameshangazwa na hatua ya Mwigamba kuendelea kuvunja katiba ya chama kwa kutunga mambo yasiyokuwepo, badala ya kuwasilisha hoja zake kupitia vikao halali vya chama.
Alisema kwa kuwa Mwigamba amekiri mbele ya waandishi wa habari kuwa amevunja katiba ya chama na kukubali kuwa aliandika kwa kutumia jina bandia waraka na kuuweka kwenye mitandao ya kijamii, ni wazi hana lengo zuri na chama chao, hivyo apuuzwe.
Chanzo – Rai
 
Walimwaga ugali yeye kaamua kumwaga mboga. Ndio siasa za vijana wetu wachanga kisiasa nchi hii. Halafu wasivyopenda kushauriwa hadi wanatia kinyaa kisa wana vi-PhD vyao au viukwasi fulani vyenye walakini wanajiona wao ndio wao. Full kiburi na majigambo yasiyo na maana.
 
Isingekua rahisi kwake kujibu kama wewe unavyoshauri, kwanza definetly alikua na hasira na chama(normal for humans) kwa hiyo in away alitaka akiexpose chama au kionekana kama kina makosa. Pili inawezekana anatafuta sympathy na kujisafisha!
 
Ndio maana wengine tunaamini Zitto ana lake jambo.Hakuna jambo analofanya linaloonesha collective responsibility zaidi ya kujijenga yeye binafsi.Kwa nafasi yake lazima anajua siri na mambo mengi ya chama lakini hizo haziwezi kuwa silaha ya kuogopwa kama mtu unatumwa na dhamira safi.
 
Last edited by a moderator:
Ukishakubali kutumika na mwegulu ujue umepungukiwa akili,kitila nae akafanya kazi ile bila kujua kua bosi wake ni mwegulu
 
PR consultant wake anaitwa Fina Mango
 
Unachekesha sana ! Viongozi walipoitisha vyombo vya habari na kumpaka kwa tuhuma,alafu yeye awe ----- akazungumze chumbani ? Ni sawa akutukanae hadharani halafu wewe ukamtukane chumbani kwa kumrudishia ! Acheni kuwa na akili kwenye vifuniko vya mzee Mtei !
 
Na mimi ngoja niongeze langu. Zitto, usimdharau mtu yeyote. Kila mtu aliyepo humu duniani ana umuhimu wake, ndo maana yupo duniani anyway. Kwa kuangalia tu, kuna baadhi ya watu ndani ya chama chako unawadharau sana. Unawaona hata hawakustahili kuwa wabunge ndani ya chama chako.

Guess what? Hao hao, unaodhani hawakustahili nyuma yao kuna nyomi ya watu wanawaamini. Ukimess na hao, ujue unamess na watu walio nyuma yao. Nilishangaa sana kuona andiko lenu mkirefer mbunge fulani wa chadema kama yule kichaa wa "ars'. Ghosh! Unajua umedharau watu wangapi walio nyuma yake?

Speak small, think louder!
 
Huko ni Kujipima ubavu na Kamati Kuu ya Chama chako iliyokutuhumu!!,
 
Ukiendelea hivi hautafanikiwa kamwe. Hautafika mbali.Utaishia njiani. Hutapata utakacho. Tafadhali tafuta Mshauri wako mbobezi wa mambo ya kisiasa ili awe anakushauri kabla ya kuamua. Bado hujitoshelezi kisiasa. Kweli kabisa. Labda kiuchumi-kwakuwa nawe ni mchumi.

Katika Mkutano wenu na Waandishi wa Habari juzi,hukupaswa kutaja tuhuma zote zilizojadiliwa ndani ya Kamati Kuu. Kutaja tuhuma zile ni kutoa siri za vikao nje na kujitetea pasipostahili. Sasa ulipojibu pale tuhuma moja baada ya nyingine ulikuwa unamjibu nani? Ili iweje? Kwa ajili ya kumbukumbu gani?

Ndugu Zitto, yawezekana unachokiamini kuwa una uwezo wa kuongoza chochote popote hapa nchini ni kweli. Lakini,imani yako isikuendeshe. Nenda nayo taratibu. Utafika tu! Ukiruhusu machagizo ya vyombo vya habari kukukimbiza mbio kuelekea unapopataka,utajikwaa;utaanguka na kuumia.

Siku ile, ungesema hivi tu: " Nayaheshimu Maamuzi ya chama changu. Nitayamaliza mambo haya kwa mujibu wa Katika na Kanuni za chama changu. Na kwasasa, sina mpango wa kuhama toka CHADEMA.Hatoki mtu hapa." Basi.Ungesubiri maswali na halafu uyajibu. Hapo, ungepata wasaa mzuri wa kuelezea kwa makini na uangalifu mkubwa mambo yako. Watu wangeshangaa.Wangekusifu. Kukosekana kwa Mshauri kumekufanya uongee mengi yenyemshiko haba.

Itoshe kusema kuwa, Zitto Zuberi Kabwe ni mwanasiasa. Bado yuko safarini.Safari ya mafanikio zaidi. Lakini,anapaswa kuwa makini.Aongee kwa kuchagua maneno;kuzingatia hadhira na kuuchuja ujumbe. Achangamane na wenzake chamani. Wawe kitu kimoja. Wasonge mbele. Lakini, Mshauri hakwepeki. Shauriwa kwanza;amua baadaye.

Kila la kheri katika siku zako 14 za utetezi. Yatakwisha tu haya. Wajibu waliokutuhumu. Sisi tunasubiri matokeo tu.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam

Mzee Tupatupa wa Lumumba, nakuheshimu sana kiongozi wa chama chetu. Huu ni ushauri mzuri sana kwa jamaa. Kuretreat ni sehemu ya vita.
 
THIS IS THE BIGGEST OPPORTUNITY FOR CHADEMA

nawashangaa watu wote wanaomsupport zitto. hoja zote zinazojengwa na hao watu ni kwa ku-ignore the fact that mipango yao ya siri ilikua na backup ya CCM. sasa unategemea nini kwa zitto kushika madara ya juu CHADEMA chini ya usaidizi wa CCM. ni mtu mwenye akili fupi tuu ndio hataelewa hili.

1. Idea for suporting zitto was introduced and promoted my CCM. and then zitto knew it and he accepted the deal
2. Strategic plans and set up was done by Kitila Mkumbo and Mwigamba.
3. FINANCIAL BACKUP, INTELLIGENCE SERVICES, AND PLANNED STRATEGIES WERE EXECUTED BY CCM AND SOME OF TISS MEMBERS

hawa wote wanaojitetea... wanajitetea kwa kutokana na hiyo point no 1 and 2. lakini kwa ujanja wao na upotishaji wao wa maukusudi wanafunika hiyo fact no 3

Zitto must be complitely terminated...

ACTION PLAN A = Kumvua madaraka = pre-emptive strike.
1. hao akina zitto na team yake wanachofanya sasa ni kuhakikisha chadema haiwavui uanachama. kuto mvua zito uanachama itakukua ni ushindi kwa zitto.. na ataendelea na mipango yake miovu ya kukiharibu chama....kwa maana atakua ndani ya chama bado...
2. kuto mvua uanachama zitto kutafanya aanze kukusanya wafuasi ndani ya majukwaa ya chadema waziwazi na hatimae kuharibu chama kabisa.
3. akiachwa atajifanya mwaminifu sana na mwenye nia njema... (hii ataifanya pia kwa ajiri ya kudaka wafuasi wake wengi zaidi)

ACTION PLAN B = kumvua uanachama = must be the target action to take
. Lazima mtu huyo asiwe mwanachama wa CHADEMA tena… atahaha kwa muda lakini hatakua na effect.. safi sana CC kwa kumpa 14 days-days ambazo watu wengi tayari tumeshajiridhisha kua huyu jamaa sii mwema kabisa.

FAIDA ZA ACTION B
1. CHADEMA itajidhihirisha kua kweli wako serious na kwa maana hiyo wataingia madarakani kwa kishindo kikuu.. na kwa ouga wa hali ya juu... watu wataacha ufisadi na ujinga wote (irresponsibility) ndani ya serikali.
2. viongozi na wanachama wote wa CDM watakua moyo mmoja with one passion, one vision and one mission kuhakikisha kua chama kinashinda uchaguzi.
mamluki hawatakua na nafasi tena... na kila mamluki ataweza kumulikwa kirahisi sana.
3. hakutakua na lelemama tena.. kila iliye chadema atakua very serious na majukumu ya kichama na kitaifa.
4. CHADEMA wataingia madarakani wakiwa ni wamoja… ready for drastic development of this nation.

Huyo jamaa ana roho wa kiburi, roho wa kujigamba, roho wa misifa, roho wa ubinafsi(u-mimi), roho ya dharua na USALITI

NCHI HII MUNGU HATARUSU KUSHIKWA NA WASHIRIKINA, WANAMITANDAO, WACHEZA RAFU NA WOTE WANAOAMINI KATIKA UCHAWI. WALE WOTE WANAOABUDU SHETANI KWA KUPITIA WAGANGA WA KIENYEJI. NCHI HAITASHIKWA TENA NA WATU WA MAZINGAOMBWE…
 
Unachekesha sana ! Viongozi walipoitisha vyombo vya habari na kumpaka kwa tuhuma,alafu yeye awe ----- akazungumze chumbani ? Ni sawa akutukanae hadharani halafu wewe ukamtukane chumbani kwa kumrudishia ! Acheni kuwa na akili kwenye vifuniko vya mzee Mtei !

Mashidano ya busara hayalinganishwi kwa wingi wa maneno bali umuhimu wa maneno. Kukaa kimya pia ni busara.
 
Isingekua rahisi kwake kujibu kama wewe unavyoshauri, kwanza definetly alikua na hasira na chama(normal for humans) kwa hiyo in away alitaka akiexpose chama au kionekana kama kina makosa. Pili inawezekana anatafuta sympathy na kujisafisha!


Kama ndivyo, ndio maana inasemwa huyo jamaa ama hajakomaa kisiasa au sio mwanasiasa mahiri kama anavyotaka jamii imwelewe. Alikuwa na hasira na chama? Bahati mbaya kwake kakutana na visiki; kwa nini Slaa kamwachia Mnyika amjibu? Hizi siasa zina wenyewe Mkuu. Ukiingia kichwa kichwa au kwa mihemuko au kwa kiburi utajiumiza mbaya.
 
Na mimi ngoja niongeze langu. Zitto, usimdharau mtu yeyote. Kila mtu aliyepo humu duniani ana umuhimu wake, ndo maana yupo duniani anyway. Kwa kuangalia tu, kuna baadhi ya watu ndani ya chama chako unawadharau sana. Unawaona hata hawakustahili kuwa wabunge ndani ya chama chako.

Guess what? Hao hao, unaodhani hawakustahili nyuma yao kuna nyomi ya watu wanawaamini. Ukimess na hao, ujue unamess na watu walio nyuma yao. Nilishangaa sana kuona andiko lenu mkirefer mbunge fulani wa chadema kama yule kichaa wa "ars'. Ghosh! Unajua umedharau watu wangapi walio nyuma yake?

Speak small, think louder!
huyu ndiye rais wa nchi mwenye dharau - angejifunza kwa Kikwete ni lini amewahi kutoa kejeli / dharau kwa mwanachana wake au hata kwa mpinzani yoyote awe mbunge, diwani au hata mwananchi wakawaida!! hili jambo umelisema ni muhimu sana kwa mwanasiasa makini hasa kijana.

Dharau, Majigambo tu kwa sababu mtu ana PHD na Mwingine kaishia darasa la saba la mkoloni kama mimi - mwanasiasa wa namna hii ni kweli hawezi kufika mbali. - DHARAU MBAYA!!
 
Ndio maana wengine tunaamini Zitto ana lake jambo.Hakuna jambo analofanya linaloonesha collective responsibility zaidi ya kujijenga yeye binafsi.Kwa nafasi yake lazima anajua siri na mambo mengi ya chama lakini hizo haziwezi kuwa silaha ya kuogopwa kama mtu unatumwa na dhamira safi.
Nawasifu tu sisiem kwa kufanikiwa kuuonyesha umma wa watanzania kwamba hatujaweza kupata upinzani wenye mwelekeo bado tulionao ni waganga njaa tu wa kawaida. Kama ZZK aliyeaminika na yeye amekuwa mzee wa mishiko nani tena kabakia huko upinzani si kote kumeoza. Sisiem sikupendi lakini bado unayo miaka mingi mbele ya kudunda; njaa haijabana kama watu wanavyotaka tuamini bado kila mtanzania anaambulia kijimkate cha angalauangalau vinginevyo watu wangetoka wenyewe mabarabarani hata kama upunzani ni nyanya kama ulivyo sasa.
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom