1. kuna wengine wanapinga kwa sababu zisizo na mantiki na ambazo Zitto amezionesha kuwa ni dhaifu,
Zitto, amezionyesha kuwa ni dhaifu? Exactly what do you mean mkuu MMJ?
2. lakini kuna wengine tunapinga kwa sababu nzito zaidi
Kama zipi hizo mkuu wangu?
3. lakini tunasimama kuona kuwa Kamati inafanya kazi yake kwa uadilifu, uwazi, na kwa haki.
Tatizo hapa ni kwamba mnaaanza ku-prejudge kamati kabla hata haijaanza kazi, mnaanza ku-question integrity za wanakamati kabla hata kamati haijaanza hivi hakuoni kuwa mnajaribu hata kuiamulia kamati maamuzi yake, na kwamba yasipokuwa mnavyotaka basi mlisema toka mwanzoni? That is shallow kama sio low, au?
4. So it is not just the integrity of the members of the committee that matters but that of the process as well.
Great, sasa nyinyi huu utaalamu wa process of how the kamati should work, mmeutoa wapi for the rocerd mpaka tayari mnaanza ku-question process za kamati hii ambayo hata kazi haijaanza?
5. There are more serious issues involved here kuliko suala la "maslahi ya Taifa tu"... na anayetaka kuamini kuwa "it is about the nation and there no party politics at play.." miye yangu macho.. hili ni goli tena linazidi la Maradona, na kama ni chess.. somebody is about to be "checked"!
Hapa mkuu naona umeandika kitendawili, na kwamba huna imani na yanayoendelea, hebu mkuu kama hujali tutengulie hicho kitendawili maana on this ishu mkuu wangu unaonekana una more to say ila unajaribu kumuheshimu tu Zitto, Mkuu sema tuchambue hapa?
Otherwise muacheni Zitto, akafanye kazi yake ya taifa na sisi tunamhakikishia kuwa tuko nyuma yake, na ninawaomba sana nyie wa the otherside pia muheshimu maamuzi ya Zitto, kama mwananchi pia wa taifa hili, maana na yeye ana uhuru wa kuamua anyoyataka bila ya kuvunja sheria za nchi yetu!
Nilikuwa nikichangia mada nyingine ambayo kada aliipost, ni mada ambayo ina uhusiano moja kwa moja na hii. Hivyo basi, nitaendelea kuzungumzia nilichokuwa nikizungumzia kwenye ile mada nyingine, ila nianze na kuchangia pointi hizo hapo juu baina yako na Mwanakijiji.
Ni kweli kwamba Zitto ana kila haki ya kuheshimiwa maamuzi yake, kumbuka tayari yeye ni muheshimiwa, ila kwenye siasa kuna mijadala. Ni wazi kwamba Mwanakijiji aliposema kuwa kuna hoja ambazo Zitto amezionyesha kuwa ni dhaifu, alikuwa anamaanisha kuwa "Zitto ameweza kuzijibu baadhi ya hoja vyema, hivyo kuzifanya zionekane kuwa ni dhaifu, hivyo kutokuweza kutumika kuwa ni kielelezo cha kupinga yeye kufanya kazi kwenye kamati hiyo. Mojawapo ni ile ya watu kuuliza kwanini yeye? Zitto amejibu kwamba si mara yake ya kwanza kuteuliwa na rais kwenye kamati, na akatolea mfano tume ya kujiunga na jumuiya ya East Africa.
Hivyo ile hoja ya kuuliza kwanini iwe yeye ndiye aliyeteuliwa na rais, na ile hoja kuwa uteuzi wake una mashaka kwa namna moja ama nyingine, hoja hiyo imedhoofu! Ila ngoma haiishii hapo tu! Sasa turudi kwenye kipengele cha pili kinachohusu kupinga kwa sababu nzito zaidi. Licha ya kwamba Mwanakijiji hakuzitaja, lakini ni wazi kwamba zipo! Wadau ni lazima watataka kujua kazi halisi ya kamati hiyo! Kumbuka kuwa Zitto anakwenda huko binafsi lakini bado anawawakilisha wanachama wa CHADEMA na wapenda demokrasia na maendeleo popote pale walipo!"
Je, siasa za kamati hiyo zitafifisha sakata la madai ya ufisadi? Je, ni sawa na kukubali kwamba madai yale ya ufisadi hayakuwa ya msingi? CHADEMA wajadili hilo kikaoni kwa maslahi ya chama ili kuepuka "loopholes". Loopholes zinaweza kuunda mazingira yanayohitajika kukuza mgawanyiko! Nadhani mnanielewa hapo. Kusije kukawa na mawasiliano mengine ya tofauti kati ya rais na Zitto ambayo hatuyafahamu! Tunajua uamuzi wa kamati kwa serikali ni wa kujisafisha, kwamba tatizo halikuwa watendaji, bali sheria za kusimamia mikataba. Kwa upande mwingine, Mheshimiwa rais ametumia ile karata amb
ayo athari zake zinaweza kufananishwa na kitendo cha kunawa mikono kwa Pilato. Ila, kama Zitto atashiriki unawaji huo, basi unawaji wake hautakuwa wa maji bali wa damu! Nina maana gani basi ninaposema kunawa kwa damu?
Serikali imekubali kuwa sheria za mikataba ni mbovu, hivyo imenawa mikono, imeanzisha kamati ambayo lengo lake ni kufanya marekebisho ya sheria hizo ili ziwanufaishe wananchi. Hii haina maana kwamba kuna ufisadi wowote uliotokea, kwa sababu kuna ukiri wa "ubovu wa sheria za mikataba". Na kama hiyo kamati si ya kuchunguza utata wa jinsi mikataba ilivyotiwa saini na mazingira yake, basi ni wazi Zitto naye ameshiriki unawaji huo, ila wake ni mbaya zaidi kwa sababu isije ikawa amewageuka wananchi! Na ukiwageuka wananchi, ni sawa na kunawa mikono kwa damu! Kikwete kama Pilato amenawa mikono na kuipeleka kesi hiyo kwa Zitto na wenzake (wanakamati), ambaye kama Kaisari, ndiye atakayetoa maamuzi ya mwisho ambayo ni wazi kwamba mwelekeo wake, hata kama sio kwa makusudi, unalenga kuwasafisha baadhi ya viongozi waliokuwa wakihusishwa na ufisadi! CHADEMA wasije wakajuta kuanzisha lile neno la ufisadi, maana linaanza kuonekana kuwa na sura ya msumeno?! Nyakati zote nilizopata fursa na wasaa wa kuchangia mada hii, nimekuwa nikisisitiza tena na tena kuwa uamuzi wa Zitto utaheshimiwa, isipokuwa kujadiliwa hakuwezi kupingwa katika mfumo huu wa kidemokrasia tulioamua kuufuata, utaratibu ambao matunda yake ya awali ni uwezekano wa kuwa na vyama vya upinzani, utaratibu wa uhuru wa mawazo! Nilishangazwa na maneno ya Zitto pale aliposema kuwa kwanini watu hawakufanya big deal kabla pale alipoteuliwa kwenye tume zilizopita, lakini wana mind yeye kuwa kwenye tume hii?
Hivi, Mheshimiwa Zitto haelewi kwamba kashfa za ufisadi walizokuwa wanazitoa zina uzito wa hali ya juu? Na kama anakubaliana na hilo, je haoni kwamba uteuzi wake ulitokana na hoja walizoibua za "UFISADI"? Akizungumzia ufisadi anataka watu wajadili, lakini anapopewa nafasi ya kuushughulikia, tusijadili? Alipozungumzia ufisadi ni big deal kwa sababu ni suala inayoligusa taifa, mijadala imekuwa ikiendelea, bado tunafuatilia na kuona ni big deal, tangu wakati alipotaka kamati teule ya bunge kuundwa ili kufanya uchunguzi, bado ni big deal, mpaka wakati akiwashutumu kina Karamagi, bado ni big deal... mpaka wanakamati walioteuliwa na rais wanajadiliwa... bado ni big deal... mpaka kamati hiyo itaanza kazi, ufanisi wenu wa kazi... oops, nina hofu bado itakuwa big deal sana! Kwamba madhumuni ya kamati hiyo ni nini hasa, matokeo yake yatakapotoka, utendaji wake, uchangiaji wenu, kupatana kwenu humo kamatini, kukutana kwenu, EVERYTHING ITAKUWA BIG DEAL, Mheshimiwa Zitto! Usisahau hilo! Unafikiri Kikwete sio smart? Msiweje mkamuhadae Mheshimiwa Rais hata siku moja!
Ni kweli anataka hizi sheria zirekebishwe, ila kwenye process zitakwenda na mtu/watu. Binafsi nafikiri Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) na upinzani kwa ujumla wanastahili nafasi zaidi katika uchangiaji huo, zaidi tu ya Zitto na Cheyo, kwa sababu suala ni nyeti. Hawa hao waliofanya mikataba hiyo ndio hao hao wanaotaka kurekebisha sheria zake... kwanini hawakufanya hivyo muda wote huo? Ok, Zitto sasa kawakomalia kichwa, halafu wanamwambia ok, come on in, lets talks, tell us how we can fix it?! Good luck! Nasisitiza Zitto, uamuzi wowote utakaochukua, hakikisha unaweke "imani ya wananchi kwako, kwa chama chako, kwa upinzani, kwa wapenda maendeleo wote." Nasisitiza imani... imani...
The only thing watu wanaweza kudhani ni kuwa umeshaomba msamaha kwa siri hivyo mmeshakubaliana kwamba tatizo lilikuwa sheria na sio kina Karamagi, hilo muweke wazi ili msije mkatulete kizunguzungu! Kwa Mheshimiwa Rais, yeye kwake mambo mdundo tu, kwani huelewi ulitaka kuwatoa nishai mawaziri wake. Kikwete very smart, lakini ni majukumu yenu wote kama viongozi hapa, nikiwaanisha Mheshimiwa Zitto na Mheshimiwa Rais; "better not outsmart your own people." Tuassume kwamba everything that was done ni for the better of our country, so kwa kifupi yaliyopita sindwele tugange yajayo, ila tuwekeane wazi. CHADEMA mjadili hilo, la sivyo wananchi wataona kwamba mmewatumia kama ngazi ya ku-IPRESSURE serikali ili kuweza kuyafikia malengo yenu binafsi. Naamini that's not the case, lakini nasisitiza kuwa maamuzi unayoyachukua kwenye ulingo wa siasa hayana budi kupimwa kwa makini SANA.
That's my personal opinion which, of course, I am entitled to. Sitaki kumhukumu anachokwenda kufanya, rather kujua atakachokwenda kufanya. Sintatumia integrity kama mjaji bali malengo yake na madhumuni yake yakiwekwa wazi, then tutajua namna ya kuipima hiyo integrity yake, na pia kumpima Zitto, kwa sababu ni lazima apimwe hapa kama akichukua uamuzi wa kuingia kamatini. Kelele zote alizopiga kuhusu ufisadi zitafunikwa ama kuwa rewarded na performance yake wakati wa utekelezaji wa hayo majukumu ya hiyo kamati, ambayo hadi sasa sifahamu ni yapi! Akumbuke kuwa kamati imepewa miezi michache tu, na wanakamati wengine wanataka ianze kazi mara moja, kabla hata ya itakachokifanya hakijajulikana ama hata kupewa nafasi ya kujulikana na wananchi, so that ijadiliwe! Is there anything to hide?
Na kwanini rushrush ya kuanza hiyo kazi kabla hata hatujajua hata job description?! Lakini uamuzi wa kikao cha Jumamosi utawasaidia kwa kiasi kikubwa sana. Kwa sababu tulikuwa na imani na Zitto uko bungeni, then ni vyema tukawa na imani naye kamatini, ila ajue wazi kuwa kama ilivyokuwa kule bungeni, ndivyo hivyo inaweza kuwa huko kamatini! Walimdirespect uko bungeni bila kujali kuwa ni wananchi walimpeleka huko, ni matumaini yetu hawatafanya hivyo this time. Je, watamheshimu zaidi kwa sababu sasa ni Rais amempeleka huko kamatini? Najua hoja yake ya kamati teule ilipingwa kwa sababu ingepandisha chati ya CHADEMA na Zitto. Wazo lake likapigwa stop huko bungeni, ambako alipelekwa na wananchi. Lakini linasapotiwa huko kamatini, ambako amepelekwa na Rais.
Je, nani ataibuka shujaa hapo? Ni kanuni Mheshimiwa Rais hakusema kwamba lile wazo la Zitto kule bungeni ni zuri na ameamua kutumia nafasi yake kama Rais kulifanyia kazi? Ok, labda badala ya kusema ndio ameamua kumuita Zitto kuonyesha ishara ya kukubaliana naye?! Zitto amekuwa overwhelmed, bila kujua ni sawa na kukiri kuwa madai yao ya ufisadi yalikuwa nai kuwapotosha wananchi! Mzee Mtei anasema policy ya CHADEMA itakuwa adopted, does he think so? Sijui ni kivipi, ila najua hii ni kamati ya mapendekezo tu! Na tuhope kwamba mapendekezo hayo yatafanyiwa kazi, ila inabidi ni wa warn kwamba mapendekezo hayo yanaweza yasifanyiwe kazi wakati huo, kwani issue haitakuwa hot tena kama ilivyosasa, na pia Rais anaweza akasema anataka pia ayajumuishe mapendekezo ya tume iliyopita. Kwani matokeo ya tume zilizopita hatafahamiki.
Mani ya wananchi inaweza ikawa imepungua kwa wakati huo, hivyo kutosikiliza madai yoyote yale yatakayokuwa yanaelekezwa serikalini, hatuwezi kugurantee kuwa umaarufu wake bado utaendelea kuwepo, kwani hatujui hiyo kamati kama itamtega ama la. Na tunaomba asiye kuja kufikia kwenye hiyo situation ambayo ni lazima achukue uamuzi mmoja wa ama kuwasaliti wananchi ama kuporomoka kisiasa. Ni wazi kwamba nia yako wewe pamoja na Mheshimiwa Rais ni nzuri, na matokeo ya uundaji wa kamati hiyo pamoja na utekelezaji wa mapendekezo hayo ukawa na matokeo mazuri kwa ujumla.
Mapendekezo mtakayoyapeleka mnaaweza kuambiwa "ok, good job, tuashukuru," ila kulishawahi kuwa na mapendekezo kama hayo. Nobody knows cause nobody has seen the reports! Mapendekezo yenu yanaweza yasiwe branded "mapya," kwani yanaweza yakawemo kwenye hizo tume nyingine zilizopita, unless una taarifa zake! Hivyo basi, kisiasa machoni mwa wananchi, baada ya mechi, of course unasoma ubao wa matokeo; Upinzani vs CCM. Siwezi kujaza matokeo hivi sasa, ila nitakumbuka baadaye mkishawakilisha ripoti yenu kwa Mheshimiwa Rais, nitajaza na hopefully matokeo yatakuwa favorably! Ni wazi ushindi utakuwa ni wa taifa, ila klabu zetu mbili za chama tawala na upinzani zina ubao wao! Je, kuna possibility ya suluhu? Suluhu ya bila kufungana ama ya kufungana? Mheshimiwa, wakati mbaya huo... Wakati huo ni mgumu sana, kwani kuwasaliti wananchi ni kutokukeep the same issues you raised bungeni.
Suala la issue nyeti za taifa letu na kuporomoka kisiasa bado lina uhusiano na kuwasaliti wananchi, ingawa tofauti yake ni kwamba imani ya wananchi inapotea lakini maslahi binafsi yanaweza kutimizwa. Kwa hiyo, tunatumai kuwa itafanya kazi kama vile Zitto na Mzee Mtei wanavyofikiria! Hata hivyo, wanapaswa kukumbuka kuwa katika kamati hiyo, ikiwa wanawadharau watu, watu watawajibu kwa kusema, "Tulikwambia!" Swali lingine tunalotaka kujibiwa ni, ikiwa hataafikiana na wenzake katika kamati, bado ana uwezo wa kueleza tofauti zao bila kuvunja taratibu za kamati hiyo?
Wadau wanataka mambo kama hayo yawe wazi! Ni lazima tujue kamati hiyo ina masharti gani, kwa sababu Zitto atasaini, na ikiwa atasaini, ina maana amekubali kufuata taratibu zote zilizowekwa na kamati hiyo! Zitto, kwa niaba ya chama chake na wananchi kwa ujumla, atasaini nyaraka hizo zinazoelezea malengo ya kamati hiyo. Najua kuna wale wanaolalamika kuwa hakuna uwezo wa kuwaapisha kwa sababu haijateuliwa na bunge, hapa sasa kazi kwako kuwaelewesha kuwa kamati hiyo haina haja ya kuapisha mtu yeyote kwa sababu sijui ikiwa ina nia ya kumhoji mtu yeyote. Hii ni kamati ya marekebisho ya sheria za mikataba. Waeleze wananchi kwa uwazi ili wasiendelee kuhoji mambo ya kamati teule ya bunge! Je, anaweza kutuambia taratibu hizo ni zipi na zinampa uhuru kiasi gani? Na ninapozungumzia uhuru, ni uhuru wa kuwaeleza wadau yote yanayojiri ndani ya kamati hiyo bila kikwazo!