Zitto: Serikali itabidi ikope ili kulipa mishahara

Zitto: Serikali itabidi ikope ili kulipa mishahara

mtu mwenye visasi roho mbaya inda kuandaa mauaji hawezi kupata Baraka za mwneyezi Mugnu atashindwa tu chini ya miezi 24 tangu aapishwe nchi imesambaratika imebaki vipande vipande umoja wa kitaifa kauwa uchumi zero hakunaanaloweza anaona maluweweluwe atubu akiri makosa mbele ya mwenyezi Mugnu aache kuuwa na kutesa watu tofauti na yeye ataona nuru na atakachokufanya chenye nia safi atafanikiwa
 
Mbona ni jambo la kawaida sana bado haijafika 2019.... Alivyo ingia madarakani alivunja na kuiteketeza record ya kukusanya mapato mapato ya kiasi cha Sh 1.5 Trl...

Hiyo 1.5trl ilikuwa anakusanya ni madeni sasa hivi hamna vyanzo vipya ya kukusanya kodi, hakuna wawekezaji wapya wale wazamani na wenyewe wanaondoka..... Mahardware yanafungwa kwa kukosa wateja, ukienda TRA kuna idadi kubwa ya watu wanao peleka barua za kufunga biashara zao hao utaambiwa walikuwa wapiga deal.....

Yaani JK katuingiza chaka.....
 
Bomu la Ajira ni Hydrogen Bomb achilia hili la maslahi yaliyo Dumaa ya watumishi tokea JK aondoke ni [HASHTAG]#Nuclear[/HASHTAG] Bomb na [HASHTAG]#Conventional[/HASHTAG] Bomb ni hili la Bomoa bomoa ....Aya Yote yatalipuka kabla 2020 mark my words
 
Huyu mhe.ndo alitaka kutuaminisha kuwa kutakuwa na upungufu wa mafuta ya ndege pale JNIA!huyu ndo aliyekuwa anahutubia kuwa nchi imekumbwa na njaa!leo hii kaja na la serikali kukopa pesa kwa ajili kulipa mishara ya watumishi wake!!
Come on....give us a break.
 
tusiwe viazi hivi hamkumbuki mh Waziri mkuu alitamka takwimu za mapato ya July na august wakati anafunga buge dogo? Alisema mapato ya Serikali ni 92% kwa mizezi ya lengo ya kukusanya 1.3 tirillion kila mwezi. Data za zito ni unongo sana. Hivi hata kama utakopa pesa ya kulipa mishahara, mbona hayo mashangingi yanatembea na watu wankula night za kufa mtu huku miradi mikubwa ikifanyika?? AACHE uwongo bwana zito

Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi ACT- Wazalendo, Zitto Kabwe amefunguka na kutoa sababu kwanini mapato ya serikali yameshuka na kusema serikali inapaswa kutazama upya utendaji wake vinginevyo itabidi ikope ili kulipa mishahara kwa watumishi.

Mbunge Zitto Kabwe

Zitto Kabwe amesema kuwa kwa miezi ya Julai na Agosti mwaka huu mapato ya serikali yalishuka mpaka shilingi 600 bilioni na kusema ni maporomoko makubwa hivyo madhara yake ni makubwa.

"Ni mporomoko mkubwa Sana na sio jambo la kushangilia hata kidogo. Madhara ya kushuka kwa mapato ni makubwa kwani mishahara ya watumishi wa Umma peke yake ni Shilingi 570 bilioni Kwa mwezi" alisema Zitto Kabwe

Aidha kiongozi huyo ameelezea sababu kubwa iliyopelekea mapato ya nchi kushuka

"Mzee Harry Kitilya alipata kuniambia mwaka 2013 " Mwenyekiti, TRA inatoza kodi kutoka kwenye shughuli za biashara zinazozalisha mapato na sio kutoka kwenye biashara tu ". Kitilya alikuwa na maana kuwa kama hakuna shughuli za biashara ( business transactions), huwezi kutoza kodi. Maelezo haya yanaeleza kwanini mapato ya serikali yameshuka. Shughuli za biashara zimeshuka sana nchini na hivyo kupelekea kuporomoka Kwa mapato" alisema Zitto Kabwe

Zitto Kabwe aliendelea kutoa ufafanuzi juu ya jambo hili la kuporomoka kwa mapato ya serikali

"Kodi inayoingiza mapato mengi Serikalini ni PAYE ( kutoka mishahara ya wafanyakazi). Kitabu cha mapato ya serikali kuu cha mwaka 2016/17 kinaonyesha kuwa wafanyakazi wote wa sekta ya Umma na sekta binafsi walichangia jumla ya shilingi trilioni 3 kwenye mapato yote ya Serikali. Hivi karibuni tumeshuhudia makampuni yakipunguza wafanyakazi na mengine kufungwa. Pia Serikali yenyewe ilipunguza watumishi iliyowaita hewa na wenye vyeti feki. Hivyo eneo kubwa la kodi ya PAYE limeathirika" alisisitiza Zitto Kabwe

Mbali na hilo Zitto Kabwe aliitaka serikali kutazama upya utendaji wake ili kuweka mazingira mazuri ya biashara na uwekezaji nchini na kudai kama serikali haiatafanya hivyo itafika mahali itabidi ikope pesa ili kulipa mishahara ya watumishi mbalimbali.
 
Hakuna kitu kigumu kama kumshauri mtu asie tayari kusikiliza ushauri wako. Muda ni mwalimu Mzuri. Utaongea baada ya Muda c mrefu

Dawa ya mtu asiyekubali kushauriwa ni kuundika ushauri wako uwe kama historia ili siku akiumbuka kila mmoja aone kwamba alishauriwa akakaidi.

Edwin Mtei alishauri mageuzi ya kiuchumi ikiwemo kushusha thamani ya shilingi. Rais Nyerere na serikali yake akamkatalia na Mtei akajiuzulu. Leo hii tumeshusha shilingi yetu kuzidi hata Mtei alivyopendekeza.
 
Hakuna mtu anayefurahia kushuka kwa mapato haya.

Kakini kama mtu hataki kushaurika, na anawaona wapinzani kama maadui....what should we do?
 
kwakweli kwa muda mfupi sana mbona watu wamekatatamaa na serekali...tukirejea post baada ya uchaguzi na post za sasa utagundua poll ya magu inashuka kwa kasi ya 100kl/hr inamzidi hata drop ya trump us....au na tz kuna fake news too
 
Kushuka hadi 600billion ni balaa aisee. Ndiyo maana walisitisha kutangaza. Mwanzoni walikua wanapiga 1.3T sasa hivi hata nusu ya hiyo hawapigi. Makusanyo hayapo tena baada ya makampuni yote kubanwa hadi wakafunga.
 
Huyu jamaa nae Mungu amlinde tu.
 
Mshupaza shingo huvunjika na jambo zuri kuliko yote ni kwamba yeye ndiye kiongozi pekee atakaeibomoa ccm na kuisambaratisha pia kuipoteza na kubaki historia kwamba "alikuwepo mbwa mwitu alieitwa ccm" na haitanyanyuka kamwe
 
Raid atakaevunja rekodi ya kukaa muhula mmoja madarakani na pia ndiye mgombea pekee wa 2020 atakaepopolewa made jukwaan
 
Back
Top Bottom