Zitto: Najuta kususia bajeti kuu ya serikali!

Zitto: Najuta kususia bajeti kuu ya serikali!

Status
Not open for further replies.

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,829
Kufuatia maamuzi yaliyo tolewa na Mbowe kwa wabunge wote wa CHADEMA kuacha kuhudhuria vikao vya bunge na kuwaamuru wote waende msibani Arusha, ili kujumuika na makamanda wengine kuwazika wahanga waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu, Zitto amefunguka kuhusu kilichopo moyoni mwake kama ifautavyo;

"Kodi ya Tsh. 1000 kwa mwezi kwa kila kadi uliyonayo imeanza rasmi. Bunge la wananchi, wawakilishi wa wananchi, limepitisha kodi hii.

Hailipwi na kampuni ya simu, inalipwa na wewe mwenye simu. Kampuni ya simu ina kusanya kwa niaba ya serikali.

Ingawa sikuwepo wakati kodi hii inapitishwa na bunge, siwezi kukwepa wajibu wa kuaibika kwa kuwa sehemu ya bunge hili.

Ni aibu kwa kuwa pendekezo la kodi hii liliondolewa na waziri wa fedha kwenye hotuba yake ya makadirio ya mapato ya serikali.

Pendekezo lilirudishwa kwa namna gani, kupitia muswaada wa fedha, haieleweki. Ni skandali.

Nasikia vibaya sana kuwa mbunge kwenye bunge lenye maamuzi ya namna hii. Nasikia aibu kwamba hatukupiga kelele za kutosha kuzuia jambo hili."


My take;

Mbowe unapaswa ujifunze UJASIRI na UKOMAVU unapokuwa kwenye siasa. Hisia zako za kudhani wakienda wabunge wote wa CHADEMA ndio itaonyesha kuwa umeguswa na tukio, basi umepotoka.

Maamuzi yako yamepelekea serikali kufanya maamuzi kandamizi kwa wananchi, kwani wote tunajua kuwa Zitto ndiye waziri kivuli wa fedha, na yeye alikuwa na nguvu katika kusimamia uozo huu usifanyike (hata kwa kupiga makelele tu). Lakini kwa maamuzi ya 'kidikteta' ya Mbowe, taifa limeingia kwenye mzigo mzito.

CHADEMA kwenye hili MMELIANGUSHA TAIFA.
 
Hili nalo neno zuri sana, wacha sasa waje wale jamaa.
 
Kufuatia maamuzi yaliyo tolewa na Mbowe kwa wabunge wote wa CHADEMA kuacha kuhudhuria vikao vya bunge na kuwaamuru wote waende msibani Arusha, ili kujumuika na makamanda wengine kuwazika wahanga waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu, Zitto amefunguka kuhusu kulichopo moyoni mwake kama ifautavyo;

"Kodi ya Tsh. 1000 kwa mwezi kwa kila kadi uliyonayo imeanza rasmi. Bunge la wananchi, wawakilishi wa wananchi, limepitisha kodi hii.


Hailipwi na kampuni ya simu, inalipwa na wewe mwenye simu. Kampuni ya sime ina kusanya kwa niaba ya serikali.

Ingawa sikuwepo wakati j]kodi hii inapitishwa na bunge, siwezi kukwepa wajibu wa kuaibika kwa kuwa sehemu ya bunge hili.

Ni aibu kwa kuwa pendekezo la kodi hii liliondolewa na waziri wa fedha kwenye hotuba yake ya makadirio ya mapato ya serikali.


Pendekezo lilirudishwa kwa namna gani, kupitia muswaada wa fedha, haieleweki. Ni skandali.

Nasikia vibaya sana kuwa mbunge kwenye bunge lenye maamuzi ya namna hii. Nasikia aibu kwamba hatukupiga kelele za kutosha kuzuia jambo hili."


My take;

Mbowe unapaswa ujifunze UJASIRI na UKOMAVU unapokuwa kwenye siasa. Hisia zako zimepelekea serikali kufanya maamuzi kandamizi kwa wananchi, kwani wote tunaua kuwa Zitto ndiye waziri kivuli wa fedha, na yeye alikuwa na nguvu katika kulisimamie hili lisifanyike. Lakini kwa maamuzi ya 'kidikteta' ya Mbowe, taifa limeingia kwenye mzigo mzito.

CHADEMA kwenye hili MMELIANGUSHA TAIFA.
Kwani wale wote waliokuwa kule bungeni waliridhia hii kodi? Acha uchochezi wa kijinga usiokuwa na chembe cha akili ndani yake.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums
 
A-Z,

..at least wabunge wa Chadema walikuwa na udhuru.

..sasa wabunge wa CCM wana excuse gani ktk kupitisha maamuzi yanayowaumiza wananchi?

..siku zote CCM wanadai CDM hawana jema wanalofanya zaidi ya kuleta vurugu bungeni, sasa ktk maamuzi haya CDM hawakuwepo.

cc: NasDaz, chama, Kubwajinga, Nguruvi3, Mdondoaji
 
Last edited by a moderator:
W -------- kweli, Utailahumu vipi CHADEMA hapo na wakati ni serkali yako sikivu serkal ya tindikali?

Kichwa cha habar hakiendani na content, au unataka tuanze kutukana na matusi ya nguon ndio uelewe kwamba hatupend uboya wako wa kuandika thread za kichochezi?
 
Kwani wale wote waliokuwa kule bungeni waliridhia hii kodi? Acha uchochezi wa kijinga usiokuwa na chembe cha akili ndani yake.


Sent from my BlackBerry 9860 using JamiiForums

Ukitaka kujadiliana na mimi, nenda kwanza kachukue akili zako ndio huje tufanye mjadala. Hivyo ulivyo siwezi kujadili na wewe. CCM na wabunge wake ni wabovu, je CHADEMA na wabunge wake wakoje? kama mbunge wa CHADEMA anajuta kwa maamuzi ya kipuuzi walioyafanya, tuwajadili awa ambao tunawaona wanafaa. CCM si inajulikana kama ni mbovu,sasa kwanini tupoteze muda kuwajadili?
 
sio hilo tu yako mengi hata kuongeza bei ya mafuta na ushuru wa magari vyote ni matatizo , hata kuongeza bei ya bia nayo ni uhuni wanataka watu wakanywe gongo?

ZITTO ANGEKUWEPO AU ASINGEKUWEPO ISINGESAIDIA KITU MAANA MADUDU NI MENGI NA BAJETI INAPITISHWA KWA KURA, WAMBENGE WA SISI NI ZAIDI YA 250. hapo hakuna kitu kaka.SANA TUNGEAMBULIA KWENYE MAGAZETI KUWA HOJA YA ZITTO HAIJAPITA BASI
 
W -------- kweli, Utailahumu vipi CHADEMA hapo na wakati ni serkali yako sikivu serkal ya tindikali?

Kichwa cha habar hakiendani na content, au unataka tuanze kutukana na matusi ya nguon ndio uelewe kwamba hatupend uboya wako wa kuandika thread za kichochezi?

Huu ni mfano mzuri sana wa msukule wa Dr Slaa. Yani haoni chochote kile, haoni uhusika wa CHADEMA, ameshindwa hata kuona kuwa Zitto kajuta kwa kususia kwake bajeti. Jamani hivi CHADEMA ina watu wa aina gani?
 
Ahsante sana mods kwa kunifutia hilo tusi kubwa nililompa huyo boya alieandika thread ya kichochezi, Pia naomba mbadilishe na kichwa cha habar.
 
Huu ni mfano mzuri sana wa msukule wa Dr Slaa. Yani haoni chochote kile, haoni uhusika wa CHADEMA, ameshindwa hata kuona kuwa Zitto kajuta kwa kususia kwake bajeti. Jamani hivi CHADEMA ina watu wa aina gani?

ww ndiyo boya msukule wa Lameck, unaandika utumbo utumbo hapa tena wenye biringanya mbichi then unategemea tukuunge mkono? Kafie mbele, msukule wa lumumba ww.
 
wakati watanzania mnaona hiyo ni ishu uingereza ina mpango wa kuingiza kodi ya KITANDA.
 
Zitto ni kijana mwajibikaji. Amegundua kuwa jambo alilofanya yeye na wabunge wengine wa CHADEMA si sawa, kwani atleast wangekuwepo wangeweza kupigia hilo jambo kelele. Hata kama wasinge badili kitu, hata kulisemea tu wananchi wakajua, ni bora zaidi.

Mimi namkubali sana Zitto, haoni vibaya kukubali kosa lake, tofauti na wanaCHADEMA wengine.

Zitto ndiye jembe chadema, kwani ameiva kisiasa.
 
Kufuatia maamuzi yaliyo tolewa na Mbowe kwa wabunge wote wa CHADEMA kuacha kuhudhuria vikao vya bunge na kuwaamuru wote waende msibani Arusha, ili kujumuika na makamanda wengine kuwazika wahanga waliopoteza maisha kwenye mlipuko wa bomu, Zitto amefunguka kuhusu kulichopo moyoni mwake kama ifautavyo;

"Kodi ya Tsh. 1000 kwa mwezi kwa kila kadi uliyonayo imeanza rasmi. Bunge la wananchi, wawakilishi wa wananchi, limepitisha kodi hii.

Hailipwi na kampuni ya simu, inalipwa na wewe mwenye simu. Kampuni ya simu ina kusanya kwa niaba ya serikali.

Ingawa sikuwepo wakati j]kodi hii inapitishwa na bunge, siwezi kukwepa wajibu wa kuaibika kwa kuwa sehemu ya bunge hili.

Ni aibu kwa kuwa pendekezo la kodi hii liliondolewa na waziri wa fedha kwenye hotuba yake ya makadirio ya mapato ya serikali.

Pendekezo lilirudishwa kwa namna gani, kupitia muswaada wa fedha, haieleweki. Ni skandali.

Nasikia vibaya sana kuwa mbunge kwenye bunge lenye maamuzi ya namna hii. Nasikia aibu kwamba hatukupiga kelele za kutosha kuzuia jambo hili."


My take;

Mbowe unapaswa ujifunze UJASIRI na UKOMAVU unapokuwa kwenye siasa. Hisia zako za kudhani wakienda wabunge wote wa CHADEMA ndio itaonyesha kuwa umeguswa na tukio, basi umepotoka.

Maamuzi yako yamepelekea serikali kufanya maamuzi kandamizi kwa wananchi, kwani wote tunajua kuwa Zitto ndiye waziri kivuli wa fedha, na yeye alikuwa na nguvu katika kulisimamia uozo huu usifanyike. Lakini kwa maamuzi ya 'kidikteta' ya Mbowe, taifa limeingia kwenye mzigo mzito.

CHADEMA kwenye hili MMELIANGUSHA TAIFA.

Huu ni ujinga na upotoshaji wa mambo. Kila jambo baya kwa wananchi mnatafuta sababu ya kuihusisha CHADEMA. CCM na wachumi wake FIRST CLASS ndiyo walioandaa bajeti na kushiriki katika kuipitisha bungeni.

Ina maana wabunge wa ccm kazi yao wakiwa bungeni ni kugonga meza na kuangalia nini kinaongelewa na wabunge wa CDM ili waweze kupinga pasipo sababu ya msingi?. Kwa hali hiyo inaonesha wazi kuwa pamoja na wingi wao hakuna wanachofanya zaidi ya kulala na kushabikia mambo ya kijinga yasiyokuwa na faida yoyote kwa wananchi.

Hilo ni lazima liangaliwe kwa undani na wabunge wa CDM waueleze umma wa Watanzania kuwa hilo ni moja kati ya mambo machafu na usaliti wanaofanyiwa na ccm kwa kushirikiana na wabunge wake.
 
Zitto ni kijana mwajibikaji. Amegundua kuwa jambo alilofanya yeye na wabunge wengine wa CHADEMA si sawa, kwani atleast wangekuwepo wangeweza kupigia hilo jambo kelele. Hata kama wasinge badili kitu, hata kulisemea tu wananchi wakajua, ni bora zaidi.

Mimi namkubali sana Zitto, haoni vibaya kukubali kosa lake, tofauti na wanaCHADEMA wengine.

Zitto ndiye jembe chadema, kwani ameiva kisiasa.

Kwahiyo hapa unatuthibitishia kwamba wabunge wote wa ccm pamoja na serikali yake ni mamburula wa kutupwa hata kushindwa kuona mzigo mkubwa kama huo kwa wananchi. Pili unatuthibitishia kuwa hata siku moja ccm na serikali yake hawafikirii ama kujali maslahi ya wananchi wengi masikini na ndio maana hawaoni hata chembe ya aibu kuanzisha kodi katika kadi za simu huku wakiacha kukusanya kodi inayostahili kutoka makampuni ya simu pamoja na makampuni ya madini.

Kwa maana hiyo ni kwamba wabunge wa ccm hawana macho wala utashi na maslahi ya wananchi bali wabunge wa Chadema peke yao ndio wana uzalendo kwa nchi yao na wanaojali maslahi ya wananchi masikini wa nchi hii.
 
.. atleast wangekuwepo wangeweza kupigia hilo jambo kelele.

Hivi wabunge wa CCM hawawezi kupigania masuala ambayo yanaonekana kuwakandamiza wapiga kura wao?

Kwa nini watu wasubiri mpaka wabunge wa Chadema ndiyo wawapiganie? Why not wabunge wa CCM? What is their role bungeni?

Hata kama wasinge badili kitu, hata kulisemea tu wananchi wakajua, ni bora zaidi.

Kumbe wabunge wa CCM siyo wasemaji? Kazi yao ni kupitisha hoja tuu bila hata kuzisemea?

Kwa staili hii hata kama serikali ikija na mswada wa kutaka kila nyumba ilipie kodi choo chake wabunge wa CCM wataupitisha na kuwa sheria.
 
Chadema wawepo wasiwepo mambo mengi ndani ya bunge yanapita kishabiki kwa wingi wa wabunge wa CCM kwani wao hawako kusaidia wananchi bali chama chao kionekane tu kinaweza kupitisha chochote cha serekali hata kama ni upuuzi. Tena ndio vizuri wananchi wajue mwaka 2015 ni chama gani wakipe kura kwa ajili ya maslahi ya wananchi. Usitake kumchonganisha Zitto na wanachadema maana hata majina ya walioficha hela Uswisi Zitto amepigania mpaka sasa hayajawekwa hadharani itakuwa kuzui hiyo elfu moja moja kwenye line ya simu. Acha ujinga wako wewe Mwigulu
 
Huu ni mfano mzuri sana wa msukule wa Dr Slaa. Yani haoni chochote kile, haoni uhusika wa CHADEMA, ameshindwa hata kuona kuwa Zitto kajuta kwa kususia kwake bajeti. Jamani hivi CHADEMA ina watu wa aina gani?

jenga hoja matusi ya haribu
 
Hivi wabunge wa CCM hawawezi kupigania masuala ambayo yanaonekana kuwakandamiza wapiga kura wao?

Kwa nini watu wasubiri mpaka wabunge wa Chadema ndiyo wawapiganie? Why not wabunge wa CCM? What is their role bungeni?



Kumbe wabunge wa CCM siyo wasemaji? Kazi yao ni kupitisha hoja tuu bila hata kuzisemea?

Kwa staili hii hata kama serikali ikija na mswada wa kutaka kila nyumba ilipie kodi choo chake wabunge wa CCM wataupitisha na kuwa sheria.

EMT,

Hapa nadhani pro CHADEMA wanataka wakwepe ukweli.

Kila siku imekuwa inasemwa humu, wabunge wa CCM hawafai, sasa iweje leo tuwajadili?

Hapa nadhani tuwajadili wale ambao tunadhani ni bora zaidi kwa watanzania. Kwa hisia za wengi humu nao ni wabunge wa CHADEMA.

Sasa kama wabunge wa CHADEMA ndio bora, sasa iweje Zitto anakiri kufanya blunder ya namna hii? yani hata nafasi yao ya kupiga makele nayo wameikosa?

Sijui kama unanielewa? ni mambo mengi Zitto amekuwa akiyasema bungeni, ila kwake yeye ilikuwa bora taifa lijue kuliko kukaa kimya kwa kuamini kuwa HAWEZI KUBADILI KITU.

Na niseme wazi, bora yake yeye kajuta, kwani wengine ndio hata hawajui impact kwa wananchi kwa kukosekana kwao bungeni.
 
Last edited by a moderator:
Status
Not open for further replies.

Similar Discussions

Back
Top Bottom