Duu!! sasa ukawa wamefanya nini mpaka sasa? au ndio wameungana, sijui unaitafsir vp harakati ya kweli? ni ile inayoonekana kwa vitendo kama PAC ifanyavyo au ya kufikirika!!!Badala ya kushughulikia kupukutisha majani ya mti, tungemwona wa maana kama angeunga na wapiganaji na wanaharakati wa UKAWA kushughulikia kung'oa mizizi ya ufisadi kwa kudai katiba ya wananchi ambayo kama ingepitishwa haya yote yangekuwa yamepatiwa mwarobaini come next year! Lakini sasa anafanya usanii wa kuwasweka ndani vidagaa huku akibeza juhudi za UKAWA. Ni msanii tu kama alivyo propesa jk.
Akili yako nindogo mno!!!
hivi unahisi hao unao ona c wasaliti wana mzidi uwezo wakujenga hoja zitto?
acha ujinga wa kumezeshwa chuki na wajinga ...kaa chini umiza kichwa kutafiti ujuee ukwel..
kipindi kile zitto katangaza kuwania urais kupitia chadema mli mezeshwa sumu eti ana vuruga chama na ni msaliti wapumbavu mka kubali kauli za mazuzu..
hapa juzi Tundu lisu amesema anaweza kugombea uraisi kupitia chadema hakuna mbwa hata mmoja alie sema Lisu ni msaliti..ila ipo sku tuta ujua ukweli.
Zito ni mzuri sana wa kujenga hoja lakini mara nyingi ni mzushi na mwongo. Na mara nyingi hufanya mambo mengi kwaajili ya personal political gains kuliko faida ya umma.
Hata tukilazimisha vipi, ukweli hubakia kuwa Duniani kote mikataba ya kibiashara huru ni siri kati ya wale wahusika wakuu. Tatizo kubwa hapa kwetu siyo usiri wa mikataba bali uadilifu wa wanaosaini mikataba kwa niaba ya Taifa.
Mkuu
Nashukuru kwa maelekezo yako.
Lakini naomba nikuweke sawa, mimi sichangii hapa kishabiki, Lakini natambua kwamba msimamo wangu juu ya Zitto ni Negative, na sidhani kama hilo ni Kosa.
Sasa turudi kwenye hoja yako?
Unamaanisha kwamba Mwanasheria wa Bunge aliwapa akina uzito ushauri kwamba wanaweza wakaruka taratibu za kupeleka mahitaji yao kwa speaker ili ayawasilishe serikalini na hata kuruka ngazi zingine za kiserikali na kwenda moja kwa moja polisi? sababu hicho ndio walichokifanya kina Zitto.
Na Je, lengo lao la kuwaitia jamaa polisi ni nini? Wote tunajua polisi ni njia tu ya kufika mahakamani, sasa PAC walikuwa wamechukua maamuzi ya kuwapeleka jamaa mahakamani?
Ndio maswali yangu hayo, labda ungenijibu na mimi, sababu majibu yako kwa mleta mada nimeyaelewa.
Ama sivyo kama issue imeisha, inabidi tujue lengo lilikuwa ni nini? Sababu kama waliteleza Je, wameanzisha mchakato stahili? Kama hawajaanzisha ni kwa nini? au wameishapewa hiyo mikataba?
Sangarara,
Labda kwa kumaliza hilo nilipenda UFAHAMU SHARIA ZA TANZANIA ZINARUHUSU MTU KAMA ANAONA HAJATENDEWA HAKI BASI ANA HAKI KWENDA MAHAKAMANI KUDAI HAKI YAKE.
Sasa kama viongozi hao wanaona hawakutendewa haki sasa tujiulize kwanini mpaka leo hawajaenda mahakamani.
Tuvute subra tuone kama viongozi hao watakwenda kudai haki yao mahakamani ya kudhalilishwa na bunge.
Mkuu Barubaru
Unanichanganya kidogo.
Kwa nini hautaki kuangalia mstakabali wa chanzo cha tukio husika.
PAC iliwakamatisha polisi wakurugenzi wawili wa TPDC sababu walikuwa wanaleta ubishi na kukataa kukabidhi mikataba 26 kwa PAC.
Kwa nini tusisubiri kuangalia kama kwa maamuzi hayo PAC watapatiwa mikataba badala yake tuangalie kama hao jamaa watakimbilia mahakamani kulalamika kwamba wamedhalilishwa?
au lengo ilikuwa kuwadhalilisha na sio kupatiwa mikataba?