Ado Shaibu
Member
- Jul 3, 2010
- 99
- 111
ZITTO NA LISSU WAMERUKA KIUNZI CHA KWANZA
Na Ado Shaibu.
Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo na Tundu Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA wanao wajibu wa kipekee katika kuiondosha CCM madarakani kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Kama nilivyoeleza kwenye makala ya wiki iliyopita, serikali ya awamu ya tano imeshindwa kabisa kusimamia uchumi wa nchi na imekubuhu katika kuvunja haki za binadamu pengine kuliko kipindi kingine chochote katika historia ya Tanzania.
Kila kundi muhimu kwenye jamii (wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, wavuvi, wanafunzi, Asasi za Kiraia, vyama vya siasa, wasanii n.k) kwa namna moja ama nyingine limeonja madhila yanayotokana na utawala wa kimabavu wa awamu ya tano.
Kinachohitajika ni uongozi madhubuti wa kuyaunganisha na kuyaongoza makundi yaliyoguswa na utawala wa awamu ya tano kuikabili na kuidondosha CCM.
Zitto na Lissu wamejijengea heshima na taswira ya kuwa vinara wa kuikabili serikali ya awamu ya tano. Wote wawili wamejenga ushawishi mkubwa kwenye jamii na kwa hakika wanastahili kuwa vinara wa kuyaunganisha makundi niliyoyataja kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Lakini, kabla ya kuutekeleza wajibu huo ambao nitaufafanua vizuri mbeleni, ni muhimu wote wawili wafahamu kuwa kuna vikwazo kadhaa vya kuvishinda. Vipo vikwazo binafsi, vikwazo vya kitaasisi na vikwazo vya dola.
Vikwazo Binafsi na vya Kitaasisi
Zitto na Lissu ni wanasisa wa muda mrefu na wanaofahamiana vyema. Mpango wowote unaowaleta pamoja ni lazima utambue kuwa wanasiasa hawa wamewahi kuhasimiana.
Wakiwa wote CHADEMA, Zitto akiwa Naibu Katibu Mkuu Bara na Lissu akiwa Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, uhasama wao uliwahi kufikia kiwango cha juu. Hili lilionekana dhahiri kipindi cha Zitto Kabwe kuvuliwa uanachama wa CHADEMA. Kipindi hicho kilitawaliwa na matamshi ya kutoaminiana kutoka katika pande zote.
Kwa kuzingatia historia hii, si rahisi kwa mtu kuwaza kwamba Zitto na Lissu wanaweza kupatana na kufanya kazi pamoja kwenye uchaguzi mkuu 2020. Kila wazo hili linaposemwa, baadhi ya watu, ndani ya CCM na kwenye vyama vyao (CHADEMA na ACT Wazalendo) hukumbushia historia hii ya uhasama kuonesha ni mwujiza kwa Zitto na Lissu kupatana na kufanya kazi pamoja.
Kwa maoni yangu, watu wanaodhani kuwa Zitto na Lissu hawawezi kufanya kazi pamoja 2020 kwa kigezo cha historia ya uhasama na kutoaminiana baina yao na baina ya vyama vyao wameshindwa kusoma alama za nyakati. Siasa ni zao la matakwa ya nyakati. Wanamikakati katika medani ya siasa daima huumiza bongo kujiuliza kuhusu matakwa halisi ya wakati husika na kutafuta mbinu zinazoendana nao.
Historia ya dunia na hata ya hapa Tanzania imetufunza mifano chungutele ya namna matakwa ya nyakati yanavyoweza kuzika historia. Iwapo matakwa ya nyakati yanazalisha maslahi mapana, vidonda vya kihistoria huponywa kwa maridhiano na msamaha.
Ni mtu wa ajabu peke yake anayeweza kung'ang'ania kuwa mtumwa wa historia hata kama historia hiyo inamnufaisha adui na kukwaza ukombozi.
Jambo la kufurahisha, viongozi wa CHADEMA na ACT Wazalendo kwa kiasi fulani wameelewa matakwa ya wakati tulio nao. Kuna kila dalili kuwa viongozi wakuu wa vyama hivyo wameelewa kuwa tunaishi katika zama ambazo CCM ikipata upenyo itaumaliza kabisa mfumo wa vyama vingi ambao hivi sasa inaudhoofisha.
Pili, wameelewa kuwa kuikabili CCM ambayo inataka kuvizika vyama makini vya siasa, ni lazima kuzika tofauti za kihistoria na kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano.
Kwa maoni yangu, kati ya mwaka 2017 na mwaka 2019, kazi kubwa imefanywa na viongozi wakuu wa CHADEMA na ACT Wazalendo kupunguza uhasama na tofauti za kihistoria baina ya vyama hivi viwili na viongozi wake.
Hapa nitataja mifano ya matukio makuu matano (5) ambayo kwa kweli ndio yaliyochangia kupunguza msuguano:
Tukio la Kwanza: Zitto "Punda" wa Mbowe?
Mwezi Februari 2017, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul Makonda alimtaja Mwenyekiti wa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe kuwa mmoja wa washukiwa wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya wanaopaswa kuhojiwa.
Zilikuwa tuhuma mbaya sana ambazo bila shaka zililenga kumchafua na kumvunjia heshima Ndugu Mbowe kama ilivyokuwa kwa wengine wengi wakati wa sakata hilo.
Zitto Kabwe alichukua hatua ya kipekee kwa kushiriki mkutano wa waandishi wa habari wa Mbowe na kuongea maneno mazito ya kumkingia kifua.
Kwanza, Zitto alisema yeye anafahamiana vizuri na Mbowe kwa muda mrefu na kama Mbowe angekuwa anauza madawa ya kulevya basi yeye Zitto angekuwa ndiye "punda" wa kumbebea madawa hayo.
Pili, aliweka bayana msimamo wake kuwa shambulio dhidi ya Mbowe na CHADEMA ni shambulio dhidi ya upinzani na yeye hatakubali kuona upinzani ukishambuliwa kisha akae kimya.
Tukio hili, ambalo Zitto liliwahi kumletea rabsha kiasi ndani ya chama kwa maoni kuwa alivuka mstari na kumtetea kupita kiasi Mbowe, lilianza kupanda mbegu ya kufungua ukurasa mpya wa maelewano baina ya marafiki hawa wawili waliopishana zamani (Mbowe na Zitto) na baina ya CHADEMA na ACT Wazalendo kwa upande mwingine.
Tukio la Pili: Lema Ndani ya Mkutano Mkuu wa ACT Wazalendo.
Tarehe 25 Machi 2017, ACT Wazalendo walifanya Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia jijini Arusha. Tofauti na matarajio ya wengi, Mbunge wa Arusha Mjini Ndugu Godbless Lema alihudhuria na kuhutubia mkutano huo.
Kwenye hotuba yake, Lema alisema anamshukuru Rais Magufuli kwa sababu kwa utawala wake wa mabavu anaviunganisha vyama vya kisiasa (ambavyo vilikuwa na uhasama) na makundi mbalimbali ya kijamii pia kama vile viongozi wa dini, wafanyabiashara, Asasi za Kiraia, wakulima n.k
Tukio hili la Lema lina umuhimu wa kipekee kwa sababu, mosi, lilikuwa ndio tukio la kwanza la kiongozi mkubwa wa CHADEMA kuhudhuria na kuhutubia tukio kubwa la ACT Wazalendo.
Pili, mjumbe alioutoa Lema ulikuwa wa kipekee. Ulikuwa ni ujumbe wa kuviamsha vyama vya siasa kwamba vinapaswa kusahau ya nyuma na kuungana ili kumkabili Rais Magufuli na serikali yake ya CCM ambao wanalenga kuviangamiza.
Tukutane wiki ijayo kwa mifano matukio matatu yaliyobaki ambayo kwa hakika yamewafanya Zitto na Lissu kujengewa mazingira ya kushinda kikwazo cha kwanza cha uhasama wao binafsi na taasisi zao.
Na Ado Shaibu.
Zitto Kabwe, Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo na Tundu Lissu, aliyekuwa Mbunge wa Singida Mashariki na Mwanasheria Mkuu wa CHADEMA wanao wajibu wa kipekee katika kuiondosha CCM madarakani kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Kama nilivyoeleza kwenye makala ya wiki iliyopita, serikali ya awamu ya tano imeshindwa kabisa kusimamia uchumi wa nchi na imekubuhu katika kuvunja haki za binadamu pengine kuliko kipindi kingine chochote katika historia ya Tanzania.
Kila kundi muhimu kwenye jamii (wakulima, wafanyakazi, wafanyabiashara, wavuvi, wanafunzi, Asasi za Kiraia, vyama vya siasa, wasanii n.k) kwa namna moja ama nyingine limeonja madhila yanayotokana na utawala wa kimabavu wa awamu ya tano.
Kinachohitajika ni uongozi madhubuti wa kuyaunganisha na kuyaongoza makundi yaliyoguswa na utawala wa awamu ya tano kuikabili na kuidondosha CCM.
Zitto na Lissu wamejijengea heshima na taswira ya kuwa vinara wa kuikabili serikali ya awamu ya tano. Wote wawili wamejenga ushawishi mkubwa kwenye jamii na kwa hakika wanastahili kuwa vinara wa kuyaunganisha makundi niliyoyataja kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.
Lakini, kabla ya kuutekeleza wajibu huo ambao nitaufafanua vizuri mbeleni, ni muhimu wote wawili wafahamu kuwa kuna vikwazo kadhaa vya kuvishinda. Vipo vikwazo binafsi, vikwazo vya kitaasisi na vikwazo vya dola.
Vikwazo Binafsi na vya Kitaasisi
Zitto na Lissu ni wanasisa wa muda mrefu na wanaofahamiana vyema. Mpango wowote unaowaleta pamoja ni lazima utambue kuwa wanasiasa hawa wamewahi kuhasimiana.
Wakiwa wote CHADEMA, Zitto akiwa Naibu Katibu Mkuu Bara na Lissu akiwa Mwanasheria Mkuu wa chama hicho, uhasama wao uliwahi kufikia kiwango cha juu. Hili lilionekana dhahiri kipindi cha Zitto Kabwe kuvuliwa uanachama wa CHADEMA. Kipindi hicho kilitawaliwa na matamshi ya kutoaminiana kutoka katika pande zote.
Kwa kuzingatia historia hii, si rahisi kwa mtu kuwaza kwamba Zitto na Lissu wanaweza kupatana na kufanya kazi pamoja kwenye uchaguzi mkuu 2020. Kila wazo hili linaposemwa, baadhi ya watu, ndani ya CCM na kwenye vyama vyao (CHADEMA na ACT Wazalendo) hukumbushia historia hii ya uhasama kuonesha ni mwujiza kwa Zitto na Lissu kupatana na kufanya kazi pamoja.
Kwa maoni yangu, watu wanaodhani kuwa Zitto na Lissu hawawezi kufanya kazi pamoja 2020 kwa kigezo cha historia ya uhasama na kutoaminiana baina yao na baina ya vyama vyao wameshindwa kusoma alama za nyakati. Siasa ni zao la matakwa ya nyakati. Wanamikakati katika medani ya siasa daima huumiza bongo kujiuliza kuhusu matakwa halisi ya wakati husika na kutafuta mbinu zinazoendana nao.
Historia ya dunia na hata ya hapa Tanzania imetufunza mifano chungutele ya namna matakwa ya nyakati yanavyoweza kuzika historia. Iwapo matakwa ya nyakati yanazalisha maslahi mapana, vidonda vya kihistoria huponywa kwa maridhiano na msamaha.
Ni mtu wa ajabu peke yake anayeweza kung'ang'ania kuwa mtumwa wa historia hata kama historia hiyo inamnufaisha adui na kukwaza ukombozi.
Jambo la kufurahisha, viongozi wa CHADEMA na ACT Wazalendo kwa kiasi fulani wameelewa matakwa ya wakati tulio nao. Kuna kila dalili kuwa viongozi wakuu wa vyama hivyo wameelewa kuwa tunaishi katika zama ambazo CCM ikipata upenyo itaumaliza kabisa mfumo wa vyama vingi ambao hivi sasa inaudhoofisha.
Pili, wameelewa kuwa kuikabili CCM ambayo inataka kuvizika vyama makini vya siasa, ni lazima kuzika tofauti za kihistoria na kufungua ukurasa mpya wa ushirikiano.
Kwa maoni yangu, kati ya mwaka 2017 na mwaka 2019, kazi kubwa imefanywa na viongozi wakuu wa CHADEMA na ACT Wazalendo kupunguza uhasama na tofauti za kihistoria baina ya vyama hivi viwili na viongozi wake.
Hapa nitataja mifano ya matukio makuu matano (5) ambayo kwa kweli ndio yaliyochangia kupunguza msuguano:
Tukio la Kwanza: Zitto "Punda" wa Mbowe?
Mwezi Februari 2017, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Ndugu Paul Makonda alimtaja Mwenyekiti wa CHADEMA Ndugu Freeman Mbowe kuwa mmoja wa washukiwa wanaojihusisha na biashara ya madawa ya kulevya wanaopaswa kuhojiwa.
Zilikuwa tuhuma mbaya sana ambazo bila shaka zililenga kumchafua na kumvunjia heshima Ndugu Mbowe kama ilivyokuwa kwa wengine wengi wakati wa sakata hilo.
Zitto Kabwe alichukua hatua ya kipekee kwa kushiriki mkutano wa waandishi wa habari wa Mbowe na kuongea maneno mazito ya kumkingia kifua.
Kwanza, Zitto alisema yeye anafahamiana vizuri na Mbowe kwa muda mrefu na kama Mbowe angekuwa anauza madawa ya kulevya basi yeye Zitto angekuwa ndiye "punda" wa kumbebea madawa hayo.
Pili, aliweka bayana msimamo wake kuwa shambulio dhidi ya Mbowe na CHADEMA ni shambulio dhidi ya upinzani na yeye hatakubali kuona upinzani ukishambuliwa kisha akae kimya.
Tukio hili, ambalo Zitto liliwahi kumletea rabsha kiasi ndani ya chama kwa maoni kuwa alivuka mstari na kumtetea kupita kiasi Mbowe, lilianza kupanda mbegu ya kufungua ukurasa mpya wa maelewano baina ya marafiki hawa wawili waliopishana zamani (Mbowe na Zitto) na baina ya CHADEMA na ACT Wazalendo kwa upande mwingine.
Tukio la Pili: Lema Ndani ya Mkutano Mkuu wa ACT Wazalendo.
Tarehe 25 Machi 2017, ACT Wazalendo walifanya Mkutano Mkuu wa Kidemokrasia jijini Arusha. Tofauti na matarajio ya wengi, Mbunge wa Arusha Mjini Ndugu Godbless Lema alihudhuria na kuhutubia mkutano huo.
Kwenye hotuba yake, Lema alisema anamshukuru Rais Magufuli kwa sababu kwa utawala wake wa mabavu anaviunganisha vyama vya kisiasa (ambavyo vilikuwa na uhasama) na makundi mbalimbali ya kijamii pia kama vile viongozi wa dini, wafanyabiashara, Asasi za Kiraia, wakulima n.k
Tukio hili la Lema lina umuhimu wa kipekee kwa sababu, mosi, lilikuwa ndio tukio la kwanza la kiongozi mkubwa wa CHADEMA kuhudhuria na kuhutubia tukio kubwa la ACT Wazalendo.
Pili, mjumbe alioutoa Lema ulikuwa wa kipekee. Ulikuwa ni ujumbe wa kuviamsha vyama vya siasa kwamba vinapaswa kusahau ya nyuma na kuungana ili kumkabili Rais Magufuli na serikali yake ya CCM ambao wanalenga kuviangamiza.
Tukutane wiki ijayo kwa mifano matukio matatu yaliyobaki ambayo kwa hakika yamewafanya Zitto na Lissu kujengewa mazingira ya kushinda kikwazo cha kwanza cha uhasama wao binafsi na taasisi zao.