Uchaguzi 2020 Zitto mbona haongelei “Grand coalition” tena kama zamani?

Quinine

JF-Expert Member
Jul 26, 2010
21,271
47,271
Nilitegemea baada ya mgombea urais wa JMT Tundu Lissu kupitia CHADEMA kumuunga mkono mgombea urais wa Zanzibar kupitia ACT Wazalendo, Seif Sharif Hamad, ungejitokeza na kupongeza na pengine kushauri Membe naye amuunge mkono mgombea wa CHADEMA, hujafanya hivyo, labda pengine ni mapema mno bado unaangalia upepo au bado kuna mazungumzo yanaendelea.

Kuna tetesi kuwa huenda unausaliti upinzani kwa kulazimisha Membe agombee ili kuzigawa kura za upinzani, hilo sina uhakika, na kuna wengine wanasema bifu lako na CHADEMA bado halijaisha, kuna wengine nao wanasema ACT Wazalendo ni tawi la CCM wamemleta Membe huko kwa lengo maalumu. Hayo yote nakuachia wewe na wasomaji wataamua.

Nia yangu hasa ni kujua wewe binafsi kama kiongozi mkuu wa chama, kwa vile huko nyuma umeonekana kuwa mstari wa mbele kuvishauri vyama vya upinzani kushirikiana au kuungana, una msimamo gani hasa baada ya jana Membe kusema ‘HATOKI MTU HAPA’.
 
Nilitegemea baada ya mgombea urais wa JMT Tundu Lissu kupitia CHADEMA kumuunga mkono mgombea urais wa Zanzibar kupitia ACT Wazelendo Seif Sharif Hamad, ungejitokeza na kupongeza na pengine kushauri Membe naye amuunge mkono mgombea wa CHADEMA, hujafanya hivyo, pengine ni mapema mno bado unaangalia upepo au bado kuna mazungumzo yanaendelea...
Ana buy time ya hatima ya wabunge wa ACT huko zanzibar. Kwa trend ambayo naiona mimi, huyu jamaa karata yake iko Zanzibar na Kusini kule. Aikishajihakikisha wabunge wake wanarudi, expect Membe anatangaza kumuunga mkono TL.

Zitto hayuko there for presidential expectation, yeye anataka wabunge ndugu yangu. Ruzuku chifu inatafutwa, na expect ACT ikwa KUBU this year, stay tuned.
 
Nilitegemea baada ya mgombea urais wa JMT Tundu Lissu kupitia CHADEMA kumuunga mkono mgombea urais wa Zanzibar kupitia ACT Wazalendo, Seif Sharif Hamad, ungejitokeza na kupongeza na pengine kushauri Membe naye amuunge mkono mgombea wa CHADEMA, hujafanya hivyo, labda pengine ni mapema mno bado unaangalia upepo au bado kuna mazungumzo yanaendelea...
Mkuu vipi katika ubunge nao?.
 
Hilo jambo lipo na wala usiwe na shaka nalo ni kimbunga kumbakumba ,kabla ya kipyenga cha mwisho lala salama hilo litatokea,
 
Kwa leo na kesho mbona mapema sana ,msiwe na kiherehere wacha hali iliyopo kwa huku Tanganyika iendelee hivihivi,siku ACT wakitangaza kwa CCM itakuwa kama baragumu la kiyama.
 
WAIKORU,

Hahaha hujui hawa ndio UVCC a.k.a JESHI LA AKIBA, asije vipi na Bashiru kawaamuru WABWABWAJE hovyo hovyo popote na kokote?!
 
Sasa kuanzie nyie chadema, na zito wenu bila kiki na maigizo hamna kitu. Zito amemterekeza mshenga wake, yeye mwenyewe kule Kigoma ccm wamemshika pabaya, kiufupi hachomoki. Sasa mnataka afanyejee
 
Jana Membe ameweka wazi kwamba atapambana hadi mwisho au hapo Ufipa hamuelewagi kiswahili!
Hahaha membe anatafuta ukuu wa mkoa, Anna Mugwila alifanya hivyo hivyo, na alihudhuria Diamond Jubilee kusema uchaguzi ulikuwa huru na haki sasa ni mkuu wa mkoa.

Membe kesha kata pumzi, ACT haikubaliki bara ni ccm hao, waende Zanzibar waongeze nguvu.

Anapiga kampeni kistaarabu atapewa ukuu wa wilaya akabobee huko.
 
Unataka aseme hapa ili u paste kwa msajili wako wa vyama vya upinzani siyo!!
 
Ana buy time ya hatima ya wabunge wa ACT huko zanzibar. Kwa trend ambayo naiona mimi, huyu jamaa karata yake iko Zanzibar na Kusini kule. Aikishajihakikisha wabunge wake wanarudi, expect Membe anatangaza kumuunga mkono TL. Zitto hayuko there for presidential expectation, yeye anataka wabunge ndugu yangu. Ruzuku chifu inatafutwa, na expect ACT ikwa KUBU this year, stay tuned.
KUB itaamuliwa na viti maalum kma ilivyokua 2010 na 2015 hakuna shortcut. CUF ilizidiwa na CHADEMA mbunge mmoja tu 2015 ila viti maalum CUF 8 CHADEMA 36 na ndio KUB ikawa imebebwa hivyo.

Unless utokee muujiza Membe amzidi kura Lissu hku bara sioni kivp KUB itaenda ACT
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom