WanaJF,
Wakati wabunge wa bunge la JMT na wajumbe wa bunge maalumu la katiba wakililia posho iongezwe, kwa mhe. Zitto imekuwa tofauti kwani yeye amepanga kugomea posho hiyo.
Maamuzi ya mhe. Zitto ya kugomea posho sio mageni, kwani ni mbunge wa kwanza wa bunge la JMT kuwahi kukataa posho za vikao na kusimama na msimamo huo mpaka hii leo.
Mhe. Zitto ameonekana kuwashangaa sana wabunge wanao simamia suala la kuongezeka kwa posho kwa kigezo cha kuongezeka kwa gharama za maisha. Hapa alihoji," hizo gharama za maisha zinakuwa kwa wabunge pekee?! Vipi na kwa Watanzania wengine hasa walala hoi?"
Aidha, mhe Zitto amewataka wabunge na wajumbe wa bunge maalumu la katiba kusimamia mambo ya msingi yaliyo wapeleka bungeni na kuyapa kipaumbele zaidi badala ya kuvalia njuga suala la maslahi yao binafsi.
Wakati wabunge wa bunge la JMT na wajumbe wa bunge maalumu la katiba wakililia posho iongezwe, kwa mhe. Zitto imekuwa tofauti kwani yeye amepanga kugomea posho hiyo.
Maamuzi ya mhe. Zitto ya kugomea posho sio mageni, kwani ni mbunge wa kwanza wa bunge la JMT kuwahi kukataa posho za vikao na kusimama na msimamo huo mpaka hii leo.
Mhe. Zitto ameonekana kuwashangaa sana wabunge wanao simamia suala la kuongezeka kwa posho kwa kigezo cha kuongezeka kwa gharama za maisha. Hapa alihoji," hizo gharama za maisha zinakuwa kwa wabunge pekee?! Vipi na kwa Watanzania wengine hasa walala hoi?"
Aidha, mhe Zitto amewataka wabunge na wajumbe wa bunge maalumu la katiba kusimamia mambo ya msingi yaliyo wapeleka bungeni na kuyapa kipaumbele zaidi badala ya kuvalia njuga suala la maslahi yao binafsi.