Zitto kugomea posho ya laki 3!!!

Zitto kugomea posho ya laki 3!!!

Status
Not open for further replies.

HAMY-D

JF-Expert Member
Joined
Sep 18, 2011
Posts
7,146
Reaction score
3,829
WanaJF,

Wakati wabunge wa bunge la JMT na wajumbe wa bunge maalumu la katiba wakililia posho iongezwe, kwa mhe. Zitto imekuwa tofauti kwani yeye amepanga kugomea posho hiyo.

Maamuzi ya mhe. Zitto ya kugomea posho sio mageni, kwani ni mbunge wa kwanza wa bunge la JMT kuwahi kukataa posho za vikao na kusimama na msimamo huo mpaka hii leo.

Mhe. Zitto ameonekana kuwashangaa sana wabunge wanao simamia suala la kuongezeka kwa posho kwa kigezo cha kuongezeka kwa gharama za maisha. Hapa alihoji," hizo gharama za maisha zinakuwa kwa wabunge pekee?! Vipi na kwa Watanzania wengine hasa walala hoi?"

Aidha, mhe Zitto amewataka wabunge na wajumbe wa bunge maalumu la katiba kusimamia mambo ya msingi yaliyo wapeleka bungeni na kuyapa kipaumbele zaidi badala ya kuvalia njuga suala la maslahi yao binafsi.
 
Wewe ni Mwehu , waambie majani ili wako waache kuwaibia wtz....
 
Sometime ninamkubali sana Mh. Zitto kwa kuishi kulingana na misimamo/maneno yake. Kuna sehemu huwa natofautiana naye, ila hapa namkubali 100%.
 
Zitto anaonyesha njia, tumuunge mkono!
Just Imagine kuna watu bado wanaendelea kulipwa mshahara wao wa mwezi japo hawapo kazini kwa kuwa wapo dodoma kwenye bunge la katiba, still wanalipwa posho laki tatu kwa siku na bado eti wanadai laki tatu haitoshi!.
 
WanaJF,

Wakati wabunge wa bunge la JMT na wajumbe wa bunge maalumu la katiba wakililia posho iongezwe, kwa mhe. Zitto imekuwa tofauti kwani yeye amepanga kugomea posho hiyo.

Maamuzi ya mhe. Zitto ya kugomea posho sio mageni, kwani ni mbunge wa kwanza wa bunge la JMT kuwahi kukataa posho za vikao na kusimama na msimamo huo mpaka hii leo.

mhe. Zitto ameonekana kuwashangaa sana wabunge wanao simamia suala la kuongezeka kwa posho kwa kigezo cha kuongezeka kwa gharama za maisha. Hapa alihoji, hizo gharama za maisha zinakuwa kwa wabunge pekee?!!! Vipi na kwa Watanzania wengine hasa walala hoi?

Mkuu mbona kuna wengi wameishazikataa. Nafikiri comments zako zingekuwa na mshiko zaidi kama ungelichuka muda kidogo kupata references zingine zaidi. Kumbuka kuna baadhi ya vyama vimeshatoa msimamo tayari wa kukataa nyongeza, na wewe unaongelea mtu mmoja tu!! Labda ndizo kampeni za chini chini unazozijua au vipi?
 
Bora agomee hiyo, na yule akili ng'ombe aliyesema wanunuliwe tablets na serikali anastahili achapwe mijeredi barabara.
Hiyo ukipiga idadi kwa wabunge wote kwa mwaka inatosha kabisa kuleta maji ya kunywa shule za sekondari..
 
Mkuu mbona kuna wengi wameishazikataa. Nafikiri comments zako zingekuwa na mshiko zaidi kama ungelichuka muda kidogo kupata references zingine zaidi. Kumbuka kuna baadhi ya vyama vimeshatoa msimamo tayari wa kukataa nyongeza, na wewe unaongelea mtu mmoja tu!! Labda ndizo kampeni za chini chini unazozijua au vipi?

Naona mkuu umesoma uzi wangu ila umeshindwa kuuelewa. Ambacho nimesema ni kuwa Zitto yeye atopokea kabisa posho, sio kwamba akubali posho iongezwe, lah hasha, yeye atopokea kabisa. Nadhani sasa utakuwa umenielewa.
 
Mkuu
mbona kuna wengi wameishazikataa. Nafikiri comments zako zingekuwa na
mshiko zaidi kama ungelichuka muda kidogo kupata references zingine
zaidi. Kumbuka kuna baadhi ya vyama vimeshatoa msimamo tayari wa kukataa
nyongeza, na wewe unaongelea mtu mmoja tu!! Labda ndizo kampeni za
chini chini unazozijua au vipi?
Ungekuwa SMART ungewataja hao wabunge wengine na hivyo vyama ambavyo wame/vimekataa hiyo posho.
 
Naona mkuu umesoma uzi wangu ila umeshindwa kuuelewa. Ambacho nimesema ni kuwa Zitto yeye atopokea kabisa posho, sio kwamba akubali posho iongezwe, lah hasha, yeye atopokea kabisa. Nadhani sasa utakuwa umenielewa.

Mkuu hapo penye blue vipi unasemaje?

 
Naona mkuu umesoma uzi wangu ila umeshindwa kuuelewa. Ambacho nimesema ni kuwa Zitto yeye atopokea kabisa posho, sio kwamba akubali posho iongezwe, lah hasha, yeye atopokea kabisa. Nadhani sasa utakuwa umenielewa.
za kwenye briefcase nyekundu hazijaisha tu?
 
ZITTO ni mzalendo pekee aliyebaki kwenye bunge hilo. Jana nimesoma post ya Joshua Nassar aliyopost kwenye ukurasa wake wa facebook, ni post ya NATAKA SITAKI.
 
KUKATAA HELA SI MCHEZO..PONGEZI ZAKE..
spider-man2_pole_468.jpg
 
Zitto anaonyesha njia, tumuunge mkono!
Just Imagine kuna watu bado wanaendelea kulipwa mshahara wao wa mwezi japo hawapo kazini kwa kuwa wapo dodoma kwenye bunge la katiba, still wanalipwa posho laki tatu kwa siku na bado eti wanadai laki tatu haitoshi!.

Kuna haja ZITTO awe Rais wa nchi hii.
 
mim ingekuwa vyema kama wangepelekwa kwenye vijiji maskin waogee maji ya tope madhani akili itawakaa sawa... kama ni kweli basi nampongeza Mh Zitto
 
Xaf xana shukrani zimfikie mheshimiwa zito na Mungu amtie nguvu katika kupigania maslahi ya watanzania
 
ZITTO ni mzalendo pekee aliyebaki kwenye bunge hilo. Jana nimesoma post ya Joshua Nassar aliyopost kwenye ukurasa wake wa facebook, ni post ya NATAKA SITAKI.

zitto posho zake zinatoka kwa ighondu kupitia kimei kwenye briefcase nyekundu na rushwa za mashirika ya umma..zitto is filthy rich
 
Joshua Nassari anataka ziongezwe. Hawa chadema ni tatizo kweli!!!

Source: Nipashe
 
Xaf xana shukrani zimfikie mheshimiwa zito na Mungu amtie nguvu katika kupigania maslahi ya watanzania

Huyo ndio Zitto, mzee wa Walkie the Talkie. Ni miongoni mwa wanasiasa wachache wenye uwezo wa kusimamia misimamo yao kwa vitendo. Kwenye hili suala la posho, Tanzania itamuheshimu sana kijana huyu.
 
Naona mkuu umesoma uzi wangu ila umeshindwa kuuelewa. Ambacho nimesema ni kuwa Zitto yeye atopokea kabisa posho, sio kwamba akubali posho iongezwe, lah hasha, yeye atopokea kabisa. Nadhani sasa utakuwa umenielewa.

Zitto anachotaka ni umaarufu tu. Yeye ameshashiba za mafisadi
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom