Zitto Kabwe timiza ahadi ya chama chako ya kuishitaki Serikali/ TCRA

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Jul 5, 2012
13,171
23,976
Tarehe 20 Januari 2020, Chama cha ACT-Wazalendo kupitia Katibu Mwenezi wake, Ado Shaibu kiliitisha mkutano wa waandishi wa habari na kuahidi kuwa iwapo serikali kupitia TCRA itazima laini za simu za mkononi kwa wananchi ambao wametuma maombi au wale ambao NIDA imewapatia vitambulisho, ACT-Wazalendo wataipeleka serikali/TCRA mahakamani.

Ni ukweli kuwa mpaka sasa wananchi wengi katika makundi ambayo ACT-Wazalendo wameyataja wameishazimiwa simu zao.

Naomba ACT-Wazalendo mtimize ahadi yenu kwa kwenda kuishitaki TCRA/ Serikali mahakamani ili ''haki ya waliozimiwa simu zao ipatikane''.

ACT-Wazalendo kumbukeni kuwa ahadi ni deni hasa pale ambapo unatoa ahadi bila kuombwa!

Kutimiza ahadi yenu ya kuishitaki serikali mahakamani kutajenga imani kwa wapiga kura kuwa mkiahidi mnatekeleza!

VIDEO ya Katibu Mwenezi, Shaibu wakati akitoa ahadi ya kuishitaki TCRA/Serikali mahakamani
 
Haina sababu tena maana TCRA imeanza kuzima line zile ambazo NIDA wametoa namba lakini watu hawajaenda wenyewe kusajili. Na hilo ni sawa, maana ni uzembe kama umepata namba lakini hutaki kusajili.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haina sababu tena maana TCRA imeanza kuzima line zile ambazo NIDA wametoa namba lakini watu hawajaenda wenyewe kusajili. Na hilo ni sawa, maana ni uzembe kama umepata namba lakini hutaki kusajili.

Sent using Jamii Forums mobile app
Kuna baadhi ya watu wanalalamika kufungiwa simu zao wakati wameishatuma maombi NIDA!
 
Haina sababu tena maana TCRA imeanza kuzima line zile ambazo NIDA wametoa namba lakini watu hawajaenda wenyewe kusajili. Na hilo ni sawa, maana ni uzembe kama umepata namba lakini hutaki kusajili.

Sent using Jamii Forums mobile app

Hii comment imezima uzi..... hoja ya msingi sana umeijibu, ACT walikuwa wanasema kama NIDA Ina jukumu la kutoa vitambulisho na haijatoa na wanawajibishwa wananchi then ipo hoja ya kushtaki......

Kama mtu kapewa kitambulisho na ajaenda Kusajili mwenyewe sasa ni mwehu tu ndo ataenda kushtaki....... kwenda mahakamani si sawa na mtu kurudi Nyumbani kalewa kapiga mke na kuitwa kwa Baba mkwe.......

Kwenda mahakamani ni facts.....
 
Kuna baadhi ya watu wanalalamika lufungiwa simu zao wakati wameishatuma maombi NIDA!
@MsemajiUkweli vipi tena ndugu yangu? Hao si ndio walewale wanaopenda kuilaumu serikali hata kwa ujinga wao wenyewe!
Kama umetuma maombi na namba imetoka zipo njia za kuuliza mtandaoni kujua namba yako lakini huwezi kutuma fomu zako tarehe 19/Jan ukataka kulaumu kuwa mbona mie nimetuma fomu nimefungiwa. Huo ni ujinga.
Kuna mahali NIDA ni wazembe lakini pia kuna mahali sisi nasi ni wazembe pia.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom