TIQO
JF-Expert Member
- Jan 8, 2011
- 13,787
- 2,078
Shida yetu ndiyo hiyo kuishi kwa tetesi. Nyerere aliwahi kuwauliza waandishi wa habari wa Kenya kuwa 'je wewe ukisikia kuwa mimi babako utakubali?' Hii ilikuwa ni baada ya kumuuliza kwamba yeye wana ugomvi na mzee Kenyatta. Watu wanazusha mambo bila ushahidi wowote na sisi tunashadadia na kuyabeba mzobemzobe kana kwamba ndiyo kweli. Na tunatumia muda mwingi kujadili mambo ya kuzushwa na muda mfupi kabisa kujadili ukweli. Bahati mbaya kazi ninayoifanya inanitaka kila mara nifanye argument on the basis of evidence. Kama hakuna ukweli uliyo bayana sishughuliki na jambo hilo.
Inategemeana unamaanisha nini unaposema mttu wa karibu na Zitto. Kama unamaanisha urafiki, yes, ni rafiki yangu kwa miaka mingi kabla hata sijaijua CHADEMA na wala hakuna mtu anayeweza kunichagulia marafiki.
Sawa mkuu ila hili kundi la PM7 masalia bado wapo mtaacha lini kuwasapoti?