Zitto Kabwe: Rais wanaokusifia tu hawakusaidii

Zitto Kabwe: Rais wanaokusifia tu hawakusaidii

Rais Wanaokusifia tu hawakusaidii. Umefanya vema kusikiliza tunaokukosoa. Tuna nia njema na tunatimiza uzalendo wa hali ya juu ambao ni kukosoa. Hatusemi wasikusifie, hapana.
Proffesional ya mwanasiasa ni sifa tuuu
 
Kosa kubwa wanafunzi na walimu walijiandaa na kufanya mitihani kwa mfumo wa wastani sasa wamepewa matokeo kwa mfumo wa division hili lazima lilete fail ya kutosha tu
 
Kukosoa bila ya kuonyesha njia nako hakufai. Penye kustahili sifa atapewa na anpokosea ataambiwa tu. Ni vizuri akiwa msikilizaji mzuri na mtandaji makini!
 
Nakushukuru Zito kabwe kwa kuanzisha uzi huu! binafsi nilishauweka facebook ila response yake ilikuwa ni kukosolewa na kutukanwa kumbe mimi ndiyo mwenye mapenzi mema na inchi kuliko hao wanaomsifia tu kwa kila jambo. Tatizo letu Tanzania hatuna ajenda ya kitaifa kila jambo limeegemea kwenye mitazamo ya kiitikadi za vyama vyetu matokeo yake hata lingekuwa jema ilimradi linamhusu mtu wa CCM au UKAWA litaonekana si jema hapo ndiyo tatizo lilipo, lakini ingefika wakati tukaachana na itikadi zetu tukaweka utaifa wetu mbele mtu hawezi ona shida kukosolewa kwani hata rais ni binadamu siyo malaika
Shida ya viongozi wa Tanzania hawana mawazo yao mapya ya kutekeleza ila wanaiga ya kiongozi aliyeko madarakani. Inatakiwa kiongozi anayeteuliwa kushika uwaziri awe na upeo na kuweza kuchanganua matatizo yanayosibu wizara yake na kuyatatua kitaalam. ufisadi upo kwenye mashirika yote ya umma kinachotakiwa ni usimamiaji vizuri raslimali za wizara. Kustukiza kuachisha kazi si suluhu kwani walikuwepo kwenye serikali iliyopita sasa hayo majipu ndiyo wanayaona sasa? Waziri awe na msimamo wake hata kama anapingana na kiongozi wake ni kiasi cha kutoa maelezo ya kina sababu zake za kupinga. Hakuna haja ya kujadili hotuba kama wewe huna mchango madhubuti wa mawazo yako nini kifanyike ili nchi iweze kupiga hatua mbele si kutoa maagizo ambayo hayatimiliziki kwa sababu ya ukosefu wa hela za maendeleo. Hakuna haja ya kusafiri na kutumia masurufu mengi wakati unajua ya kuwa budget ya mwaka uliomalizika haikugawanywa ipasavyo. Viongozi waache kwa kasuku
 
Uzi haujitoshelezi!!! no facts no attachment; no background!!! nothing!!!!

Queen Esther

Rais Wanaokusifia tu hawakusaidii. Umefanya vema kusikiliza tunaokukosoa. Tuna nia njema na tunatimiza uzalendo wa hali ya juu ambao ni kukosoa. Hatusemi wasikusifie, hapana. Wawe na kiasi
 
MMM hawa ni WANAFIKI.

Lini uliwahi kuona mwandishi Wa hii mada (kibo) amemsifia Rais Magufuli.

Pia hilo alilosema Mhe. Zitto ambalo limeshughulikiwa baada ya kumkosoa Mhe. Rais Je, umeliona ??

Kwa jukwaa la GT's tulitegemea mada Kama hii iwe na background information at least na some few facts, otherwise it is an empty message. UNAFIKI KWA KWENDA MBELE!!!

Queen Esther

Mimi naamini hata wanaokosoa nao wawe na kiasi. Sidhani kama watu watafanya mashindano ya nani anakosoa zaidi na nani anasifia zaidi.
 
ni vigumu kumpima Magufuli kwa siku mia moja kwani nchi ilikuwa imevurugika na mafisadi na wauasi wao walikuwa wanatamba ila ameanza kwa kuwatumbua majipu tusubiri alete bajeti yake na tuone utekelezaji wa bajeti yake maana ameingia kakuta bajeti imeshapitishwa na pia nchi haina fedha badala yake watu wanashindana kuiba na kutumbua kile kilichokuwapo
 
Back
Top Bottom