Zitto Kabwe: Nyerere wangu mimi!

Zitto Kabwe: Nyerere wangu mimi!

Nyerere hakuwa na price Tag Mgongoni kwake! Wengi walijaribu kumrubuni lakini walishindwa! Nyerere alipinga siasa za ukabila na ukanda kwa nguvu zote! Nyerere alikuwa na msimamo thabit hakuyumbishwa hata siku moja! Nyerere hakutumiwa na Makaburu weupe wala weusi alikuwa anawapa za uso! Zile Transactions za Ujerumani plus Deals za Kuvuta fedha za EPA kwa Ballali, ukiongezea na Ukimya wa Buzwagi saga plus Matrillions za Uswis zinamfanya ZZK kuonekana kikaragosi cha mtoto wa kindagaten Mbele ya Nyerere... Acheni Kumtusi Baba wa Taifa... RIP Mwalimu
nadhani MBOWE ndiye anastahili kufananishwa na nyerere. watu kama nyie ni aibu kwa taifa hili.
ZZK ni mwanasiasa wa kupigiwa mfano wa nyerere kuliko mwanasiasa yeyote aliye hai hapa tanzania. unalijua hilo, bavicha wanalijua, mbowe analijua, mimi na wengine woote tunajua.
ila tunatofautiana kwa sababu nyie wengine ni walamba vinyesi vya wafalme.
huwezi kujua hili... lakini hata nyerere alikuwa natuhumiwa kuwa anamiliki mabilioni huko USWIS na tulikuja kuamini kuwa haikuwa kweli baada ya kustaafu na kurudi kuishi maisha ya kawaida kabisa. kwa mwanasiasa tuhuma ni kitu cha kawaida kabisa hasa ukiwa mwanasiasa mwenye upeo na tishio kwa wenzako kisisasa kama alivyo ZZK.
zzk ni nembo na ni tishio kwa mafisadi na vibaraka
hapendwi na yeyote kati ya wale wenye malengo mabaya
ila muda ukifika mtatambua ujinga wenu na wooote mtamsujudu
 
Siasa ya Tanzania imesheheni mashabiki wa siasa na siyo wanasiasa, wao wanashabikia watu badala ya kusimamia itikadi ya vyama vyao. Nani asiyefaham kwamba Zitto ndiye chachu ya mabadiliko ndani ya bunge kwa kuonyesha msimamo thabiti wakati wa buzwagi scandel? Baada yake ndipo wengine nao wakafuata njia. Hata sakata la tokomeza pressure ya huyu kijana iliinfluence maamuzi so mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni!
 
asante ndugu zzk kwa historia nzuri iliyo shehen sifa kwa sera ya ujamaa. pa1 sana mkuu
 
zitto nikiongozi anayejua shida za watz
huyu ndo anayefa kuwa raisi wa nchi
 
Sasa wewe ukisoma hio post ya Zitto, imemwongelea zaidi Nyerere au Zitto.
Usijibu haraka tulia kwanza.
We jifanye kuelewa sana tu lakini ukweli utabaki palepale kwamba Zitto anamwongelea Mwalimu thru first hand experience!msingi wa hoja yake hapa ni maisha Enzi za mwalimu na ametumia historia yake kujengea hoja .
watu weledi walitakiwa wajikite katika kchambua maisha ya wakati ule dhidi ya sasa si kuchambua Zito yule dhidi yaZitto wa sasa
 
Kuna shule hapo kigoma,Dawati moja wanafunzi 15. Ni aibu mpaka leo hatuna madawati, siasa bado wanapiga poroji tunamuenzi mwalimu!!!!Huu ni ujinga.
 
Kuna shule hapo kigoma,Dawati moja wanafunzi 15. Ni aibu mpaka leo hatuna madawati, wanasiasa bado wanapiga poroji tunamuenzi mwalimu!!!!Huu ni ujinga.
 
Mh! Hizi story za mtu kukumbuka details hivyo za darasa la kwanza huwa zinanitia wasiwasi sana. Kuna huyu Zitto Kabwe na January Makamba. Yani hawa wenzetu wanataka kutuaminisha kua wao swala la uongozi walizaliwa nalo kama haki yao na walioteshwa na Mungu na kuandaliwa toka vichanga!

Utakuta story za dhiki na shida, over exaggeration ya truimph over turmoil, overcoming immense obstacles in dire situations to finally emerge the messiahs to lead us to the promised land.


There stories of tribulation and truimph are sure to make the likes of Job, Moses and Jesus envious to say the least.
Wanataka tuwafikire kama wao ni watu pekee sana na waajabu wakati waliyoyapitia kama yana ukweli kuna waTZ wengi sana wamepitia lakini hawatumii kama kete ya kupata kula/kura!

Hehehe ngoja mimi nitakuja na story yangu muone jinsi nilivozaliwa kwenye zizi la ngombe huku nikimsaidia mama yangu kujifungua mimi, nilivoanza kunywa uji wa mchanga na nilipofikisha miaka mi5 nikaanza kulima na kulisha kijiji!

Mkuu umenifurahisha...!! mie stori yanngu ingejuwa kali kweli!! Maana kulala njaa siku tatu ilikuwa kawaida sana tena nikiwa darasa la saba!! na nilifaulu!! lkn ya nini hayo ..... Nyerere alikuwa mtoto wa chifu hata kwenda shule alipendelewa kwa sababu ya kuwa mtoto wa chifu!!...lkn hakuwahi kusema vitu wanavyosema hawa vilaza!!!....
 
Mwaka 1984 nilianza darasa la kwanza katika Shule ya Msingi Kigoma, katika mji wa Kigoma. Nakumbuka kupelekwa Shule siku ya kwanza na mama yangu mzazi Bi Shida Salum (Mungu amrehemu) nikiwa sina viatu yaani pekupeku wala begi la mkononi, nilikuwa nimebeba mfuko wa nailoni.

Nakumbuka usiku wa kuamkia siku ya kwanza kwenda shule, sikulala kwa furaha na hamu ya kuwa msomi, nilijisikia fahari kuanza shule japokuwa sikuwa na kitu chochote cha zaida zaidi ya kaptula ya shule na shati liloshonwa kwa kitambaa cha sanda. Pia nilianza shule nikiwa nimechelewa kwa mwaka mmoja maana wenzangu walianza wakiwa na miaka 7. Mwaka 1983 nilipopelekwa shule mkono wangu haukuweza kushika sikio upande wa pili, ambacho kilikuwa kipimo cha kuandikishwa darasa la kwanza.

Hali ya maisha wakati huo ilikuwa mbaya sana. Nakumbuka kwenda shuleni nikiwa sina kitu tumboni au siku nzima nilikunywa uji usio na sukari. Uji wenyewe ulikuwa ni wa unga wa njano uliotokana na mahindi ya njano ambayo tuliambiwa nchi yetu ililetewa kama msaada kutoka nchini marekani.

Shule yetu kama zilivyokuwa shule nyingi za wakati huo hatukuwa na madawati ya kutosha na vyumba vya madarasa vilikuwa vichache sana. Ilikuwa ni kawaida kwa wadogo (darasa la kwanza mpaka la tatu) kusomea chini ya mwembe na kukaa juu ya matofali. Hali hiyo ilipelekea kaptura yangu ya shule kuwekwa viraka vingi maana ilikuwa inachanika mara kwa mara. Nyakati nyingine ilibidi kwenda shuleni na shati likiwa halijakauka hasa siku za alhamis, siku ya usafi na iwapo nikiwa zamu ya mchana kwani nilikuwa nina shati moja tu tena lililotokana na kitambaa cha sanda.

Kwa dhahiri, watoto wa masikini na matajiri tulikuwa shule moja, darasa moja hata wote kukaa kwenye matofali. Watoto watawala na watawaliwa tulicheza mpira pamoja, kuruka dana na hata kuruka kamba. Hatukujisikia wanyonge kwa sababu hatuna viatu au kuvaa kaptura zenye viraka na mashati ya sanda. Kamwe sikumbuki kudharauliwa shuleni sababu ya uduni wa maisha yangu.

Heshima ilitokana na uwezo wako darasani na kupitia hilo nilipata marafiki wa kutoka madaraja yote ya maisha. Nakumbuka mtoto wa Mkurugenzi wa Maendeleo Mkoa wa Kigoma ndugu Daniel Masanja ndiye alikuwa rafiki yangu wa karibu na kwa kuwa sikuwa na hata pesa ya kununua bajia wakati wa mapumziko, yeye alikuwa ananinunulia.
Huko baadaye, ada yangu ya kidato cha kwanza ililipwa na Mzee Sebastian Kasomi ambaye mwanaye Kasomi Mabula alikuwa rafiki yangu mkubwa mara alipohamia shuleni kwetu akitokea mjini Shinyanga. Mzee Kasomi alikuwa Mkuu wa idara ya Kodi ya Mapato mkoani Kigoma.

Licha ya uduni wa maisha watoto wengi tuliishi kwa matumaini makubwa sana. Mwalimu wetu Mkuu ndg. Daniel Andulile alikuwa mkali sana kwa watoto wote bila kujali daraja la maisha la wazazi wao. Alikuwa anatucharaza viboko kwa makosa na utundu bila ubaguzi. Alisisitiza sana kusoma kwa bidii ili kujenga Taifa. Dhana hii ya kujenga Taifa iliingizwa kwenye akili zetu na sisi kumeza bila kujali maana yake. Wakati mwingine tulikuwa tunarudi nyumbani huku tukijadili kitoto kuwa tunajenga Taifa. Kila siku mwendo wa kilometa Sita kwenda na kurudi shuleni.

Elimu hii isiyo ya kibaguzi sasa najua ilitokana na sera za Baba wa Taifa Mwalimu Julius Kambarage Nyerere. Jitihada zangu darasani ndio ziilikuwa kipimo cha utu wangu na sio uwezo wa kiuchumi wa wazazi wangu.. Elimu iliyompa fursa sawa za kuendelea na kusonga mbele mtoto aliyekuwa kigoma, kantalamba au Dar es salaam. Elimu iliyokuza ndoto, kuinua ari na kujenga matumaini ya kila mtoto wa kitanzania. Elimu iliyovunja na kusambaratisha matabaka ya kiuchumi na dhamana.

Elimu iliyojenga uzalendo na hamasa ya kutumikia taifa letu kwa misingi ya haki, uadilifu na upendo.
Sikuwahi kukutana na Mwalimu Nyerere isipokuwa niliwahi kumwona akiwa ndani ya gari nikiwa nimepanga mstari barabarani alipofanya ziara mkoani kwetu mwaka 1987 nikiwa darasa la nne. Lakini nilikuwa kama ninaishi naye kutokana na namna nilivyotaka kuwa kama yeye. Nikiwa darasa la pili nakumbuka katika mkebe wangu ( mathematical set) mkuu kuu niliweka picha ya kukatwa kutoka kwenye gazeti ya Mwalimu na Kawawa. Na nilijisikia fahari kuwa na picha zao, mara zote nilipokuwa nafungua mkebe kutoa kalamu nilijisemea kimoyomoyo, “siku moja nitakuwa kama wewe”

Licha ya maisha magumu tuliyokuwa tunaishi, maisha ya kupanga mawe kwenye mstari wa kununua mahitaji muhimu kama sukari, sabuni na mafuta kutoka duka la ushirika, maisha ya kushindia uji wa yanga na kutembea mwendo mrefu kwenda shuleni, niliishi kwa imani kubwa kuwa mimi na watoto wengine tupo sawa. Usawa katika kupata elimu, usawa katika kucheza na usawa katika ndoto na matumaini. Nimemaliza elimu ya Chuo Kikuu, ndoto niliyoruhusiwa kuwa nayo kwa sababu ya sera za Ujamaa, za Mwalimu Nyerere.

Ujamaa haukuwa katika usawa wa elimu tu ambapo kila mtoto alipata elimu bure na bora katika Shule za umma bila ubaguzi bali pia namna jamii iliishi. Mtoto alikuwa analelewa na jamii nzima. Ukifanya makosa mtaani mzazi yeyote anakuadhibu ili kukurekebisha. Ukifanya jambo jema, mzazi yeyote anakupongeza.

Mwaka 1985 mwezi Novemba nilipokuwa natoka shuleni, karibia na Benki ya Taifa ya Biashara Tawi la Obed Katikaza, nilikutana na Mama Colleta Furugunya tuliyekuwa tunaishi mtaa mmoja na nikimwita bibi Colleta. Aliponiuliza matokeo yangu ya mtihani wa kumaliza muhula wa pili wa darasa la pili kwa kujiamini nikampa karatasi yangu ya matokeo.

Nilikuwa nimeshika nafasi ya tatu darasani nyuma ya Ramadhan Kalukula na Haki Manyaga. Bibi Colleta alinishika mkono mpaka duka la Viatu, Bora Shoes na kuninunulia jozi yangu ya kwanza ya viatu. Viatu vile viliitwa Asante Salim, aliyekuwa Waziri Mkuu wa mwisho wa Mwalimu Nyerere ambaye alikuwa anajaribu kubadili hali mbaya iliyokuwepo. Hivyo ndivyo nilivyopata viatu vyangu vya kwanza vya shule. Shukrani kwa sera nzuri ya ujamaa, mshikamano na upendo.

Hizo ni enzi.


Zitto Z. Kabwe

Chanzo: Zitto na Demokrasia

Mamna kitu .ukikua utaacha utoto tu
 
Kuna mahali kagusia kantalamba hebu wanaoifaham hyo shule waseme kidogo

Ipo Sumbawanga Mjini, ni shule upande chuo cha ualimu TTC, miaka ya 70s ilikuwa ni seminari ya kanisa katoriki, walipita watu wengi hapo mashughuli, akiwepo Mizengo Pinda na wakina Pengo. Sasa inamilikiwa na serikali ni boarding kwa ajiri ya Boys tangu mwaka 2005, mwanzo ilikuwa mchanganyiko wake kwa waume. Ni Moja kati ya shule mashughuli zilizotaifishwa na serikali mkoani Rukwa kutoka kwa RC. Ina sifa y akukusanya wanafunzi wengi kutoka pembe mbalimbali za nchi hii. Kipindi furani ilijaza wakimbizi watusi kwa wahutu(Zzk), wengi wakitokea Mishamo na Katumba (Mpanda sasa Katavi) lakini pia wanakigoma wengi wamesoma hapo ni mashughuri sana. Ukitaka asili ya jina niulize tena asante.
 
Ipo Sumbawanga Mjini, ni shule upande chuo cha ualimu TTC, miaka ya 70s ilikuwa ni seminari ya kanisa katoriki, walipita watu wengi hapo mashughuli, akiwepo Mizengo Pinda na wakina Pengo. Sasa inamilikiwa na serikali ni oarding kwa ajiri ya Boyza tangu mwaka 2005, mwanzo ilikuwa mchanganyiko wake kwa waume. Ni Moja kati ya shule mashughuli zilizotaifishwa na serikali mkoani Rukwa. Inasifa y kukusanya wanafunzi wengi kutoka pembe mbalimbali za nchi. Kipindi furani ilijaza wakimbizi watusi na wahutu, wengi wakitokea Mishamo na Katumba (Mpanda sasa Katavi) lakini pia wanakigoma wengi wamesoma hapo ni mashuhuri sana. Ukitaka asili ya jina niulize tena asante.

Nivizuri kama pia ungenijuza na jina lake lina maana gani.
 
Nivizuri kama pia ungenijuza na jina lake lina maana gani.
Kantalamba ilimekuwa modified tu, matamshi halisi ni katalambwa au pantalambwa("ka" from red, inasimama kuonyesha udogo, " Pa" from red inasimama kuonesha pahala, au mahali). Sasa maana yake ni kwamba maeneo hayo kulichimbwa shimo kama handaki ambamo Majemedari wa jeshi la kifipa walijificha hapo, sasa juu ya hilo shimo lilokwenda eneo kubwa(extended in term of canal like structure) kuliwekwa mfuniko dhaifu( miti midhaifu na kufukiwa udongo). Lengo ilikuwa ni kumshinda adui kirahisi ambao ni Wangoni, maana mfipa na Mgoni wamepigana vita sana , ikiwa kupinga uvamizi wa Mngoni kwenye nchi ya Ufipa. Ikumbukwe kuwa Ngoni Migration ikuwa na njia kuu tatu, Moja ilitua Mngongoma( Songea leo chini ya kiongozi Mbonani na badae Chief Songea nk), Njia ya Pili(route) ilikuwa kuelekea Sumbawanga(Fipa land) chini ya Zwangendaba(Kafa na kuzikwa Mwaka 1845 Matai-Rukwa) ambaye alikuwa adui mlengwa hapa, Njia ya tatu ilikuwa na Mputa Maseko aliyeenda Uhololo-Kati mwa Tanzani. Lengo la huo mfereji ni kwamba adui akikanyaga anatumbukia hivyo mkiwa ndani akiwa amepagawa na ajari then mnaanza kumshambua. Mwisho mngoni alishinda na kilichowaponza wafipa ni ukarimu baada ya kusema tuwakubari adui tuishi nao, wakiwa hawajajiandaa wakashambuliwa. KANTALAMBA SHORTLY MEANS PASIPOVUKIKA NA MALENGO YA HAPO HAYAKUBADILIKA KWANI MKOLONI HASA MJERUMANI ALIDUNDWA HAPO VIZURI SANA KWANI PALITUMIKA PIA KUPINGA UKOLONI. Ajabu serikaLi imeruhusu kujengwa mji pahali hapa mwaka 2000's nakupoteza historia nzima, shimo juzi limefukiwa na mabepari wamejenga mahekalu yao. God Bless RUKWA
 
tabia hii iliendelea mpaka miaka ya 1990's.....sidhani kama sasa ipo
 
Back
Top Bottom