Zitto, imetosha sasa

Tatizo hapa ni Zitto kusemea hili jambo au ni NSSF kupewa Kiwira?

Inawezekana kwamba tunapinga kwa sababu Zitto kasema au tunakubali kwa sababu Zitto kasema.

Sisi, mimi na wewe, tunasemaje?

Na Zitto hawezi kutoa amri, naamini hilo analijua na nafasi yake ya kushauri kama kamati anaifahamu. Mawazo yake ndio ya kujadiliwa. Kwa nini anasema hivi na sio vile.

Mwisho, tunawasiwasi na NSSF kutokana na uwezo au tunawasiwasi kuna watu watakula hapo katikati?

Kama ni sababu ya pili, basi tuna tatizo zaidi. Kwa nini mtu ambaye tunawasiwasi nae ndie amekabidhiwa fedha zetu na ndie anaendelea kupokea makato yetu? Kwa nini tusisafishe huo uozo tunaoungelea?

Nitarudi nikishaielewa vizuri hii mada.
 
I dont understand. Kwanza hapa umeme umekatika, washeni Dowans halafu tumzime.:hug:
 
[B said:
Lu-ma-ga[/B];1748530] Augustino Lyatonga Mrema ameamrisha kukamatwa kwa afisa wa Halmashauri ya Rombo eti kwa ubadhirifu

"boundaries" za majukumu ya kamati za bunge. waziri wa nishati na madini, kuwa ni nani kati ya William Ngeleja na January Makamba.

 
Kwanza niliposikia kuwa Zitto ametoa ushauri huo nilihisi kizunguzungu! Haya Mashirika yanawakamua wananchi na sasa wanataka wawakamue hata kwenye umeme?? Kwanini wasishauri Kiwira apewe mtu au kampuni yenye uzoefu katika masuala ya umeme? Mfuko wa hifadhi ya jamii na kufua umeme, tena wa makaa ya mawe, wapi na wapi? Hapa kuna jambo limefichika!
 
Hii ni camouflage lakini ushauri wangu ni kuwa mkiendelea mtaanguka zaidi sababu yake. Kwenu nyie upinzani ni kuchukia kila kitu kinachofanywa na Serikali.
 
Hii ni camouflage lakini ushauri wangu ni kuwa mkiendelea mtaanguka zaidi sababu yake. Kwenu nyie upinzani ni kuchukia kila kitu kinachofanywa na Serikali.

Fuatilia hotuba mbalimbali za viongozi wa CDM kwenye maandamano, yalikuwa ni ya ku-identify problems na kusuggest solutions. CCM kwa upande wake inaona tu watu wanaandamana wanahatarisha amani. Kinalalamika tu kwa kila jambo. CCM imekuwa kama chama cha upinzani.
 
Kaka majimshindo,

Anachosema Taifa kwanza mi nimekielewa vzuri. sidhani anakataa uwekezaji,anachozungumza ni yeye Zitto kushadadia suala hilo la NSSF kupewa hiyo kitu, na kama ukiangalia ni kweli sasa kuna mkanganyiko kati ya kamati za bunge na wizara husika kimajukumu/madaraka. Kamati zinaonekana kuwa ndio executives sasa, hata issue ya Makamba January.

All in all Zitto Zuberi si yule ambaye nilitokea kumkubali sana hapo awali kwa ukali wake dhidi ya mafinyango ya serikali/CCM. I wonder what has changed him, kama ni mafisadi ndo walivo basi nomaaaaa!
 
ndiyo maana uenyekiti wa kamati nyeti za bunge ulipangwa na kupangika vilivyo,lakini katika kutekeleza majukumu lazima tuwamulike,hatukuwa na uwezo wa kuwazuia mkalie hivyo viti wale ambao hatukiridhika na uwezo wenu
 

Ndg;
those are politician they have a strategy to create public attention.
Kwa nini aite waandishi wa habari kutoa ushauri kwa shirika ambalo anajua mahali zilipo ofisi zake? na endapo utachunguza waweza gundua hajawahi hata kupeleka hayo mapendekezo in writing!!
NA HUO NDIO UBABABISHAJI UNAOTUWEKA HAPA TULIPO!!
HATUNA UTARATIBU!! TUNAJIENDEA TU KAMA KONDOO MALISHONI!!!
 
Vijana mnanifurahisha mnavyomkaushia Majimshindo, hahahaaaaa Safi sana. Kuna wawili watatu ambao inabidi kuwakumbusha kuwa kuna watu humu ndani haifai kujibizana nao wala kuongea nao. BIG UP.

Kwa wanaomtetea Zitto kwa hili, naona hawaelewi tatizo liko wapi.

Tatizo si kuwa hatuna imani na NSSF. Ukweli mbona umeandikwa tangu jana?

NSSF hawana wataalamu wa kufua umeme ila wana hela zetu sisi. Sasa watakapoamriwa kutengeneza umeme/kuchimba makaa ya mawe basi watakuwa na option mbili: Kuchukua wabia wa serikali ambao ni TANESCO au kuchukua mbia mwingine ambaye ni ********.

Huyo ****** wengi wetu tuna wasiwasi kuwa atakuwa Richmonduli aka Dowans ambaye milele ofisi zake zipo Mirambo Street na kampuni mama ni CASPIAN. Huyu bwana huyu ni kama Boomerang. Kila ukimrusha na kumtupilia mbali, yeye anakurudia. Na hapo ndipo mzizi wa fitina kalala maana UFISADI wote wanaotaka kuufanya basi utaanzia hapo.

Barabara ya Chalinze hadi Msata ilikuwa ijengwe na Wakorea. Ila wakalazimishwa wawe na Sub-contactor ambaye alikuwa ni shirika la JKT kama sikosei na huku Kikwete Mdogo akiwa kajipachika kama kupe. Cha ajabu, hela zote walipewa hawa Wabongo ambao ni Sub-Contactor na jamaa wakalala mbele na hela. Matokeo yake ni kuwa hadi leo haijajengwa wala kipande (kupanulia). Mkorea kalizwa maana hajapata hata senti tano pamoja na kuingia Bongo na vifaa vyao.

Hii ndiyo Bongo ambao inabidi kuwamulika hawa jamaa kwelikweli. Sintashangaa hawa wanaokuja kutetea hapa na kuonyesha kuwa akina Zitto na Makamba wanafanya kazi kwelikweli, ndiyo hao hao wanaozisubiri hela zitoke. HAKUNA KULALA mwaka huu. Tutakupigieni kelele hata kama mtakuja JF na kusema huu ni USHENZI, UTOTO, UPUUZI, UJINGA na kila aina ya tusi mnalolifahamu. Wengine tukiwa JKT tumetukanwa sana na hatutajali sana.

Kama mkija na mapendekezo ya KUIPA NGUVU Tanesco na kuwaachia hatimaye wenyewe wafanye kazi na nyie mkisimamia tu, tutakuwa na nyie milele. Tanesco wamekuwa wakisumbuliwa tangu Mkapa aje na ile kampuni yake ya South Africa na wakala hela mwishoni mkawafukuza. Mkaja na mbinu nyingine nyingi tu na hadi leo mmeshaona kula kwenu kuko TANESCO tu.

Ingekuwa vema KUPIGA marufuku hawa wawezekaji wengine wa UMEME na Tanesco wabaki peke yao na huku akina Zitto, Makamba, Shelukindo nk nk wakisimamia tu. Kama kazi/umeme hauzalishwi, si mfukuzani tu CEO wa Tanesco na mlete mwingine? Badala ya kuwasikiliza akina CEO, kwa nini msiwalete Wahandisi na wao watoe maoni yao?

Kibaya kinachoniudhi hapa Tanzania ni hii tabia ya viongozi waliosoma mambo ya ABUSHIRI na Tip Tip, kukaa na kuamua mambo ya Umeme, barabara, mitambo, viwanda nk wakati hata Mwanga wa nini kinaongelewa hawana. Heri wizara ya Nishati angeliwekwa Prof. Mwandosya maana akikaa na Wahandisi wenzie, wanapeana mambo in detail. Sasa hawa akina Makamba, ukiwauliza hata Transformer inavyofanya kazi hajui. Ukimwuuliza Jet Injine inafanya kazi vipi hajui. Na huyu ndiye aagize mitambo ya umeme nje au kutafuta kampuni la kuzalisha umeme Tanzania. Kweli tatizo la umeme ni Tanzania ni UONGOZI (by Mwanakijiji).
 
Hata ukiniuliza sasa hivi ni nini jukumu la bunge nadhani nitapata sifuri na kichwa kitaniuma hadi nikalazwe hospitali
 
WENYEVITI KAMATI ZA BUNGE, ACHENI KUWAGASI MAWAZIRI NA KUTUKERA WANANCHI
KWA UPAYUKAJI NA KUBWABWAJA MIDOMO KILA DAKIKA


Wenyeviti wa Kamati za Bunge, jamani nyinyi si Mawaziri chonde waacheni mawaziri wafanye kazi zao Tanzania nzima ila kwenu nyinyi eneo lenu la kazi ni mle mle ndani ya bunge na wala hatutaki kuwasikia sauti zenu mkirandaranda huku mitaani na mikogo ya ajabu.

Nyote msiojua kazi ya mwenyekiti wa kamati yoyote ya bunge basi nendeni mkachukue darasa kule Bumbuli kwa Mzee Shelukindo na jinsi UPAYUKAJI NA KUDANDIA KILA JAMBO KANA KWAMBA MMEKUA VIRANJA KATIKA DARASA LA MAWAZIRI usivyohitajika. Mtakomaaga lini nyinyi watu?? Ukimuona Lowassa Gongolamboto utadhani ama ni Waziri wa Ulinzi au wa Mambo ya Ndani.

Ukimuona Februari Ma-Ropes ndio kabisaa utadhani siku hizi William Ngeleja hana kazi tena. Ukimtazama Zitto Kabwe aka Mzee wa Michongo ya HILA ndio kabisa utadhani wizara ya fedha kiongozi wake si yule tunayemfahamu siku zote - jamani tulieni na muache UBONGO FLAVA wenu katika kazi za umma.

Japo mkanda mzima Uwenyeviti wa kamati mbalimbali bungeni ulivyotolewa na malengo yake hasa bado yanatafutiwa majibu lakini upayukaji na mikogo ya kujihisi rais waziri anapokuja kwako au wakuu wa mashirika muache. Kama unafanya kazi vizuri, hata ukiwa kimya, sisi wananchi tutajua tu na wala msilazimike kuwa PUBLI NUISANCE kiasi hiki kila leo kwa vyombo vya habari!!

Hata hivyo wakati tunapoendelea kutafuta majibu juu ya mpango mzima Uenyeviti wa Kamati Mbalimbali za bunge na jinsi zilivyogawiwa kama chapati kwa wateule, mpaka hivi sasa wengine tayari tumeshaguswa akilini kwamba wateule hawa wengi wao ni VIBARAKA AMBAO KUNGETAMANIKA WAPEWE UWAZIRI KAMILI kwenye serikali hii ya kifisadi na uchakachuaji lakini kwa kuona NOMA kwetu sisi wananchi ndio mkapewa short-cut hiyo ambayo wengine tayari mnadhania kwamba ni mabosi wa mawaziri kama si marais kwa nafasi zenu hizo.

Huruma kweli Zitto, February Ma-Ropes na Lowassa kwa mienendo yenu hii!!!!
 
Uongozi wa nchi hii ni wa ajabu sana.
Hivi hakuna job discriptions za hawa wenyeviti, mawaziri na hata wataalam katika fani mbalimbali?
Sasa hivi hawa wenyeviti wa kamati za bunge hasa hawa waliowekwa na mafisadi ni waropokaji sana kana kwamba wao ndio wasemaji wakuu, wakutoa amri za utekelezaji, wataalamu nk. Wanatia kichefuchefu. Hii kasi, ari ya kutufilisi kweli ni zaidi ya mlivyodai.
Ushauri wangu kwa hawa vijana ni kuwa uchawi hufundihswa tangu utotoni lakini kuupractice ni mpaka ufikie umri mkubwa (kungwi) angalia kama kuna akina mama vijana wanauuawa kule shinyanga. Ninyi mumepewa ufisadi kama baba zenu lakini kasi hiyo hamfiki, mtaliwa nyama kabla ya wakati.
 
Hivi Kiwira kununuliwa na NSSF kuna tatizo lipi? au Kiwira ibaki ikijifia bila mtaji na wapewe wawekezaji wa nje bila ubia na Taasisi au mashirika ya ki Tanzania ndio vyema?

Nawashangaa sana wanaoona kuwa NSSF haipaswi kuwekeza Kiwira.

Hapa issue ya Msingi na ambayo hata wewe unajifanya hujaiona ama kwa makusudi au tu we ni kilaza ni kwa nini NSSF???may be Zitto angesema Mifuko ijitolee kuwekeza na si ku pendekeza NSSF,hii ni Logic kabisa,Mawazo ya Zitto kupendekeza NSSF ipewe Kandarasi hiyo yanatofauti gani na Force za Lowassa Kuipa Richmond Kandarasi,tofauti yake ni kuwa Lowassa alikuwa PM na Zitto ni just Mwenyekiti wa Kamati tu,lakini Maudhui yao unawezakusema kuwa ni sawa,Lowasa alitaka na alishinikiza Richmond ipewe Kandarasi ya Kufua Umee,alikuwa na Personal interest pale, je Zitto akitaka NSSF ipewe hiyo Kandarasi tumueleweje??
Ifikie Mahali hata Mkeo unayempenda vp akikosea umwambie ukweli na sio kumchekea chekea tu
 
Zitto,
mimi nasema hivi tamaa mbaya huwa mwisho wake ni mbaya.tamaa zako za kupenda ukubwa na mambo makubwa mwisho wake siyo mzuri.anayejiinua mwenyewe Mungu humshusha daima sitashangaa kama tayari umeshahaidiwa mabilioni kama ya TANAPA.
 
Wakuu, nadhani mpango wa NSSF kununua Kiwira haukuanzishwa na Mh. Zitto, mbona hatuwasakami hao hao NSSF wanaotaka kuwekeza kwenye mradi wa kujenga bomba la gesi toka Mtwara kwenda Mombasa na Mwanza?, mradi wa kujenga UDOM, magorofa ya Mchikichini, daraja la Kigamboni etc, etc, etc...

Mimi si msemaji wa mh. Zitto isipokuwa naamini kabisa yeye binafsi amekuwa mshabiki wa suala hili kutokana na performance ya NSSF kwenye miradi yao mingine waliyokwisha fanya.

Pia imani yake inaweza kuwa inachangiwa na uwezo wa kifedha wa NSSF ukilinganisha na wawekezaji wengine ambao malengo yao makubwa ni kuchota pesa za mradi badala ya kuwekeza pesa. Mfano mzuri ni hiyo kampuni iliyoshindwa hapo Kiwira iliyokuwa ikimilikiwa na comradi Nkapa....

Mwisho nawaombeni tumuache kijana afanye kazi...ingawaje kumkosoa ni vizuri lakini ingekuwa vizuri zaidi kumkosoa pale alipo haribu na sio kumfuatilia kwa kila jambo. Kwanza kumbukeni huyu ni member mwezetu hapa jamvini, tusimfanye achukie na mwisho ajitoe jamvini...:washing:
 

NSSF DAMU
Join Date11th March 2011Last Activity

Naona umeamua kujiunga JF Kusafisha Mambo.
Ila tumia akili ndugu,hapa Tanzania ni NSSF tu ndo wanauwezo wa kuwekeza kiwira????
HATA HIYO YA ZITTO KUWAPIGIA CHAPUO NI RUSHWA TOSHA.... LOH
 
Nafikiri pia si kusema mifuko ijitolee. Ila la muhimu ni kuwa waje na maelezo yote kuwa NSSF watakuwa na ubiya na fulani. Na fulani huyo awe na utaalamu wa kutengeneza umeme ambalo kwa Tanzania wanabaki Tanesco peke pake.

Kwangu mie ingelikuwa busara zaidi kufanya kwamba:

"NSSF wanatoa hela na KUSIMAMIA na TANESCO wanazalisha umeme na kurudisha hela NSSF."


Hali ikiendelea hivi, basi Ikulu, Serikali na Bunge wafukuzwe na NSSF wapewe hiyo mihimili.
 
Mkuu hata mm sikuona tatizo mawazo ya zitto juu ya kiwira lakini inashtua kuona wenye mawazo tofauti kushambuliwa na kamati ya zitto tena tukiamini kwa baraka zake! Nilishatabiri bado kuna kitu nyuma ya zitto na mwisho wa siku atatushangaza! The means justify the end.Tanzania nakupenda sana na tutakufia bila woga.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…