Ukistaajabu ya BMK, utaona ya Bunge la jamhuri. Actually, leo ndio nimepata sura halisi ya bunge let likoje.
Kuna haja ya kurefine sana sifa za wagombea ubunge ili tupate watu sahihi kwa majukumu ya bunge.
Leo kwa sababu suala linaloongelewa ni la kitaalamu, u kilaza wa wabunge wengi ambao wanatoka ccm umejianika. Hawanahoja wanaishia kuongea kwa jazba, kulazimisha ili mradi wanatetea wanaccm wenzao bila hata kuona wanavyojichora kwamba ni vilaza.
Wabunge wa upinzani, japo ni wachache wanaongea hoja nyingi kwa vielelezo.
Maskini wabunge wa ccm hata hawafahamu maana wala umuhimu wa vielelezo. Sijui ccm inatumiaga vigezo gani kupata wabunge wake. Ni vigumu kuelea kama waliochangia leo ni wabunge au ni kitu gani.
Wengi wameshindwa kutofautisha authenticity ya taarifa ya CAG, na taarifa isiyokuwa na authenticity yoyote aliyowasomea muhongo. Wanaona zote ni taarifa tu maadamu mtu kasema. Hata pale Mhongo alipo attach wrong references kuwahadaa, hawalitambui, wao wanaona ni vielelezo tu.
Kweli ni fedheha kubwa kuona mtu anapewa kuchangia katika suala kama lile lenye evident disparities na illegalities anaanza kusema, tuweke ka utaratibu kwa kulindana kwa sababu kufukuzana huku leo kwangu leo kwako. Lugha zile zile za ccm zilizolifikisha taifa hapa.
Kwa kweli components za wabunge wa ccm ni fedheha kwa taifa na aibu kubwa.
Lakini, nakumbuka Mama Makinda alisema kwamba bunge lina diversity kubwa. Ninaimani atakumbuka hili na kwamba kwa kuzingatia uhalisia na unyeti wa suala lililoko mezani, na uwezo wa ufahamu wa wabunge kwa jambo la kitaalam kama lile,, na athari zake kwa taifa ndani na nje ya nchi, ninaamini uongozi wa bunge hautaliamua kishabiki kama vile wanafanyaga.
Ninaamini wataamua maamuzi ya kitaalam bila kujali wingi wa kura zinazopigwa kwa sababu suala hli liko juu ya uwezo wa ufahamu wa wabunge wengi wa ccm ambao ni wengi.
Ninajua uongozi wa bunge utaamua maamuzi ya kuishauri serikali ushauri sahihi wa kitaalam na si kishabiki kama inavyoonekana kwenye michango. Na kwamba uongozi wa serikali utaamua maamuzi sahihi ya kuwawajbisha wote waliohusika katika migawo,, waliofanikisha na hata waliozembea ili kuweka msingi safi wa uendeshaji serikali kwa kesho na pia kwa ajlii ya image ya serikali.
Kinyume cha pale ni aibu kubwa na fedheha!.
Unafikiri kwa nini Chenge amelazamisha kwenye katiba pendekezwa mbunge ukisha jua kusoma na kuandika kama Nchambi na Lusinde hiyo ni tiketi tosha. Ccm wanafaidika sana na wabunge wa hivi ni rahisi kuwatumia na kuwatumikisha bila kuhoji.