Zak Malang
JF-Expert Member
- Dec 30, 2008
- 5,404
- 234
Zitto amshangaa Pinda kufunga mdomo vurugu Arusha
NAIBU Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amesema anashangazwa na ukimya wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu mgogoro wa kisiasa uliozuka mkoani Arusha na kuwa chanzo cha vurugu zilizosababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi wengine zaidi ya 20.
Kabwe, ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini alisema jana kuwa Pinda ana mamlaka ya kuingilia kati suala hilo hasa ikizingatia limetokea kwenye ngazi za kiserikali ambazo zimo chini yake.
Alisema sheria ya miji ya mwaka 1982 inampa mamlaka Waziri Mkuu kutoa agizo la kufuta uchaguzi na kuamuru kufanyika uchaguzi mwingine ulio huru na haki pindi inapobainika taratibu hazikufaatwa katika uchaguzi husika. Tatizo la Arusha na uchaguzi wa Meya ulifanywa kinyume na taratibu na sheria za uchaguzi zimekiukwa," alidai Zitto kwenye mahojiano na Shirika la Utangaza la Uingereza (BBC), jana.
Alisisitiza kwamba vurugu za Arusha ni tatizo la uchaguzi wa Meya na mwenye dhamana ya kufuta na kuamru kufanyika kwa uchaguzi mwingine ulio huru na haki ni Waziri Mkuu. Nashangaa yeye kukaa kimya wakati kila kitu kinaeleweka, alisema. Alisema miongoni mwa mambo yaliyokiukwa ni pamoja na CCM kumuingiza mbunge mmoja wa viti maalumu Marry Chatanda kupiga kura kinyume na sheria.
Alisema Chatanda ambaye ni katibu wa CCM Mkoa wa Arusha si mwakilishi wa Mkoa huo na kwamba ni mbunge anayewakilishi mkoa wa Tanga ambaye kisheria hakusitahili kupiga kura kwenye uchaguzi huo. Mgogoro wa Arusha si ugomvi baina ya CCM na Chadema wala Chadema na Jeshi la Polisi, bali umetokana na ukiukwaji wa makusudi wa sheria na taratibu za uchaguzi wa Umeya, uliowanyima madiwani wa Chadema ambao ni wengi kupiga kura, alisema Zitto.
Katika hatua nyingine mmoja wa washiriki wa maandamano hayo, Dadi Igogo alilieleza Shirika hilo la utangazaji la BBC namna alivyopigwa na polisi na kuwekwa rumenda bila hata ya kupelekwa hosptalini licha ya kuumizwa vibaya.
Alisema Polisi walikamata na kumpiga kisha kumtupa kwenye gari lao na walipokuwa wanaenda kituoni walimkanyaga na kumsababishia maumivu sehemu mbalimbali hususan, kiuno.
Alisema mara baada ya kufikishwa kituoni alitupwa rumande na kwamba licha ya kuwaomba askari hao kumpeleka Hosptali walikataa na kumlazimisha kulala humo hadi kesho yake mchana. Mimi nilipigwa na hata nilipowaomba wanapeleka hosptalini walikataa na kunilaza ndani hadi siku ya pili tulipotolewa na kupelekwa mahakamani ndipo nilipopata fursa ya kwenda kutibiwa, alisema Igogo.
Igogo ambaye awali alikuwa akifanya kazi za kisheria katika makao makuu ya Chadema alisema akiwa kituoni alishuhudia ukiukwaji wa haki za binadamu.
Nikiwa ndani, aliletwa mtu akiwa anabubujika damu lakini polisi walikataa kumpeleka hosptalini licha ya watu wengi kushauri walidharau. Mbaya zaidi alibaki huko hata mimi nilipotoka jana (juzi) yeye nilimuacha humo bila ya matibabu yoyote alisema Igogo wakati akihojiwa na BBC.
Chanzo: Mwananchi JUMAPILI
NAIBU Katibu Mkuu wa Chadema, Zitto Kabwe amesema anashangazwa na ukimya wa Waziri Mkuu Mizengo Pinda kuhusu mgogoro wa kisiasa uliozuka mkoani Arusha na kuwa chanzo cha vurugu zilizosababisha vifo vya watu watatu na kujeruhi wengine zaidi ya 20.
Kabwe, ambaye ni Mbunge wa Kigoma Kaskazini alisema jana kuwa Pinda ana mamlaka ya kuingilia kati suala hilo hasa ikizingatia limetokea kwenye ngazi za kiserikali ambazo zimo chini yake.
Alisema sheria ya miji ya mwaka 1982 inampa mamlaka Waziri Mkuu kutoa agizo la kufuta uchaguzi na kuamuru kufanyika uchaguzi mwingine ulio huru na haki pindi inapobainika taratibu hazikufaatwa katika uchaguzi husika. Tatizo la Arusha na uchaguzi wa Meya ulifanywa kinyume na taratibu na sheria za uchaguzi zimekiukwa," alidai Zitto kwenye mahojiano na Shirika la Utangaza la Uingereza (BBC), jana.
Alisisitiza kwamba vurugu za Arusha ni tatizo la uchaguzi wa Meya na mwenye dhamana ya kufuta na kuamru kufanyika kwa uchaguzi mwingine ulio huru na haki ni Waziri Mkuu. Nashangaa yeye kukaa kimya wakati kila kitu kinaeleweka, alisema. Alisema miongoni mwa mambo yaliyokiukwa ni pamoja na CCM kumuingiza mbunge mmoja wa viti maalumu Marry Chatanda kupiga kura kinyume na sheria.
Alisema Chatanda ambaye ni katibu wa CCM Mkoa wa Arusha si mwakilishi wa Mkoa huo na kwamba ni mbunge anayewakilishi mkoa wa Tanga ambaye kisheria hakusitahili kupiga kura kwenye uchaguzi huo. Mgogoro wa Arusha si ugomvi baina ya CCM na Chadema wala Chadema na Jeshi la Polisi, bali umetokana na ukiukwaji wa makusudi wa sheria na taratibu za uchaguzi wa Umeya, uliowanyima madiwani wa Chadema ambao ni wengi kupiga kura, alisema Zitto.
Katika hatua nyingine mmoja wa washiriki wa maandamano hayo, Dadi Igogo alilieleza Shirika hilo la utangazaji la BBC namna alivyopigwa na polisi na kuwekwa rumenda bila hata ya kupelekwa hosptalini licha ya kuumizwa vibaya.
Alisema Polisi walikamata na kumpiga kisha kumtupa kwenye gari lao na walipokuwa wanaenda kituoni walimkanyaga na kumsababishia maumivu sehemu mbalimbali hususan, kiuno.
Alisema mara baada ya kufikishwa kituoni alitupwa rumande na kwamba licha ya kuwaomba askari hao kumpeleka Hosptali walikataa na kumlazimisha kulala humo hadi kesho yake mchana. Mimi nilipigwa na hata nilipowaomba wanapeleka hosptalini walikataa na kunilaza ndani hadi siku ya pili tulipotolewa na kupelekwa mahakamani ndipo nilipopata fursa ya kwenda kutibiwa, alisema Igogo.
Igogo ambaye awali alikuwa akifanya kazi za kisheria katika makao makuu ya Chadema alisema akiwa kituoni alishuhudia ukiukwaji wa haki za binadamu.
Nikiwa ndani, aliletwa mtu akiwa anabubujika damu lakini polisi walikataa kumpeleka hosptalini licha ya watu wengi kushauri walidharau. Mbaya zaidi alibaki huko hata mimi nilipotoka jana (juzi) yeye nilimuacha humo bila ya matibabu yoyote alisema Igogo wakati akihojiwa na BBC.
Chanzo: Mwananchi JUMAPILI