Zitto akosoa utafiti wa Twaweza

Zitto akosoa utafiti wa Twaweza

Mbingo

JF-Expert Member
Joined
Mar 20, 2014
Posts
411
Reaction score
230
Ni dhahiri mwanasiasa huyu machahari hapa Tz na msomi kijana amekosoa huu Utafiti kwa hoja

1. Eti mitandao ya kijamii 1% na TV 4% radio 64% wakati tunajua mitandao ya kijamii ndio inaongaoza kuzungumzia siasa na hata kumkosoa Mkuu wa kaya.

2. Eti mkuu anakubalika kwa 96%, huo Utafiti utakuwa ulifanyikia kule kwenye sangara na watu wasiofanya kazi yoyote maana mtu anayefanya kazi yoyote ameshaparuriwa. Ukweli ni kuwa huyu mkuu 45% zinamtosha warudie tena huo Utafiti.

Maisha ni magumu jamani kwa sababu za matamko yake.....!!!!
 
Ni kweri kabisa kumpa mkuu wa kaya 96% ya kukubarika ni uongo usio na shaka hata kidogo kwani kila unapopita watu humsema mkuu kwa ubaya tena ni ktk kila idara waislamu wanamlalamikia mkuu kuwa ni mdini mno wapo wanaosema kuwa mkuu ni mtu anaeangalia sana watu wa kanda ya ziwa wapo wanaosema kuwa mpenda makuu na mfano wa hayo mimi nasema lau kama zitto ingekua simkabari ningesema hata hiyo 45% amempendelea ila kwa kuwa nina imani na zitto nakuliana na % alizompa
 
Hamna linalonistahajabisha kwa sasa, kwani safari hii mfumo unaendeshwa na "Mr. To proud"

Haitaji kusikia hata raia atakelia ana njaa, otherwise utakua unamjaribu.

Lugha nzuri masikioni mwake kwa sasa ni Mtukufu, nalala nao mbele, uchumi umepanda, wananchi wanakuoenda sana piga kazi, tumewakomesha, hamna siasa inafanyika nchini, n.k
 
Hata mtu aliyepata elimu ya chekechea anajua kwamba utafiti huu ni famba

Wananajisi taaluma zao
 
Nyumbani kwetu watu 11 hatumkubali
Mtaani sijui ila ukienda pale kariakoo wanaomkubali hawatazidi 10 kati ya maelfu ya walio hapo Kariakoo
 
Zitto anatakiwa kujua Kisanyansi huwezi kupiga jambo bila ya kufanya experiments au source of information yako kuwa verified sasa nitashangaa sana wanaojiita wasomi kupiga tafiti bila ya kufanya tafiti kwani utafiti unapingwa kwa utafiti lakni kisiasa mtu yeyote anaweza kupinga jambo lolote na pia ikakubalika kwani siasa ni mchezo wa walio wengi wape hata kama wte hawajuh au wamefata mkumbo tu watanzania tuache kutumia macho na masikio yetu kufanya maamuzi tutumie akili ,mioyo yetu na tuinvest katka nguvu ya akili si nguvu ya mwili watanzania wanajua kila kisemwacho katika mitandao kimesemwa na watanzania wote kitu ambacho c kweli
 
Ni kweri kabisa kumpa mkuu wa kaya 96% ya kukubarika ni uongo usio na shaka hata kidogo kwani kila unapopita watu humsema mkuu kwa ubaya tena ni ktk kila idara waislamu wanamlalamikia mkuu kuwa ni mdini mno wapo wanaosema kuwa mkuu ni mtu anaeangalia sana watu wa kanda ya ziwa wapo wanaosema kuwa mpenda makuu na mfano wa hayo mimi nasema lau kama zitto ingekua simkabari ningesema hata hiyo 45% amempendelea ila kwa kuwa nina imani na zitto nakuliana na % alizompa

Kama utafiti umefanyika kwenye Ofisi za CCM na UVCCM mnategemea nini?
 
Wafuasi wa Zito mnapiga kelele fanyeni utafiti wenu msilete makelele bila data
 
watu kibao wako mahakamani kwa kumkashifu mtukufu...... kunajaaga siku ya kesi!!!
bila shaka nyomi hii huja kushangilia kuona jamaa hawa wakifungwa!
 
Utafiti hukanushwa kwa utafiti na siyo kwa hisia au kudhani.

Hujafanya utafiti nyamaza usiseme kitu, huna mamlaka.

UKWELI NDIYO HUO
 
Ni dhahiri mwanasiasa huyu machahari hapa Tz na msomi kijana amekosoa huu Utafiti kwa hoja

1. Eti mitandao ya kijamii 1% na TV 4% radio 64% wakati tunajua mitandao ya kijamii ndio inaongaoza kuzungumzia siasa na hata kumkosoa Mkuu wa kaya.

2. Eti mkuu anakubalika kwa 96%, huo Utafiti utakuwa ulifanyikia kule kwenye sangara na watu wasiofanya kazi yoyote maana mtu anayefanya kazi yoyote ameshaparuriwa. Ukweli ni kuwa huyu mkuu 45% zinamtosha warudie tena huo Utafiti.

Maisha ni magumu jamani kwa sababu za matamko yake.....!!!!
Respondents wa TWAWEZA si ni wale ambao wako listed na TWAWEZA na WALISHAWAWEZESHA kwa kuwanunulia SIMU na POWER BANKS? Nahisi hata hela ya vifurushi vya kuongea na data huwa wanawanunulia. Na ikitokea wanataka kusikika wanawapigia simu kuwauliza maswali wanayotaka. Sasa mtu 'unayemhudumia' kila wakati si ataongea yale anayodhani WEWE MHUDUMIAJI unapenda kusikia? Sampling yao si random kwa sababu wana idadi ya watu fulani (labda 2000) ambao wako fixed, na walishawawezesha na kila mara wanasample humo humo.
 
Back
Top Bottom