Erickford4
JF-Expert Member
- May 22, 2017
- 1,133
- 1,094
Hizi CCTV camera za kawaida zinaweza kumuona mchawi? Je hizo camera zilizotumika hapo zinapatikana huku kwetu?
zinatisha kweliView attachment 530206View attachment 530207hii picha ya pili ilishawahi kuleta sokomoko hapa jukwaani hadi basi
Unanikumbusha ndugu yangu kipenzi alizama na meli kutokea tanga mwaka 2009 mpaka leo hajaonekana, kuikumbuka ile stori umenifanya leo nilie sanaAsili ilipochagua usiku iwe ndio wakati wa kulala kuna siri kubwa ilifichwa huko
Kifo kinauma sana hasa anapoondoka mtu tumpendaye sana...nafuu ni kwamba unajua kwamba kafa na hutaweza kumuona tena.....
Kuna hili la kupotea watu
-kuna watu wanapotea kisha wakaonekana wakiwa hai hata kama wana majeraha
-kuna watu wanapotea kisha wakaonekana maiti zao.. Inauma sana
-kuna watu wanapotea kisha mabaki yao yakaja kuonekana baada ya muda fulani wakiwa wameoza kabisa ama imebakia mifupa tupamoja na maumivu yote hayo lakini unajua fika kwamba hatimaye kaonekana japo mabaki
Kimbembe kiko hapa!
Kuna watu walipotea halafu wakapotea kabisa kabisa, hawajawahi kuonekana tena wala maiti zao wala mabaki yao! Yani hawakuacha alama yoyote
Mwili wa binadamu una hulka moja. Haupotei kimoja lazima kitabaki chochote cha kukutambulisha iwe mabaki iwe maiti nk....lakini unaposoma habari za unsolved mysteries ama disapearances, kuna kitu kikubwa mno utakipata humo cha kutisha
Kiza kina meno! Kiza kina roho! Kiza kina mauti! Kiza kinameza na kupoteza kabisa
Ulimwengu wa giza ni ulimwengu wa roho. Roho ya giza ikikukamata utapotea milele na hutakaa uonekane hata unyayo wako
Giza lenye roho hutengeneza maumbo ya ajabu na kuogofya, haya ndio maziraili yanayotowesha watu
Hii hutokeaje?
Scenarios ni tofauti... Mtu alikuwa karudi nyumbani salama lakini mara anaaga kuwa anatoka mara moja..hiyo ndio kwaheri.. Hutakaa umuone tena
Tumewapoteza wengi kwa style hii...hata hapa tunaweza kuwa na mifano hai(sio wa Ben), ndege ya Malaysia ni mfano mwingine mzuri tu! Haijawahi kuonekana pamoja na technology ya kisasa mno ya kuitafuta!
Uhalisia ni UPI?
Kuna roho hulishwa/hula binadamu hai kama alivyo mzimamzima! Na hazikuvizii bali unaenda kwa wito unaaga kabisa watu uliokuwa nao
-natoka kidogo
-kuna mtu namuona hapo jirani
-nimeitwa maramoja
-Mimi natangulia home nk nk
Ni wito ambao huja bila kutambua na sometimes wala hujui ni kwanini unaitwa unaitiwa nini na unaitwa nanani ama kwanini unawaacha wenzako na kuondoka mwenyewe! Cha kushangaza unaondoka ama unaenda bila hofu tena kwa kujiamini
Dunia halisi ni replica ya ulimwengu wa roho ukiona kuna fisi mla mizoga kuna roho ziko hivyo pia! Ukiona kuna simba na chui walao fresh kuna roho zipo hivyo
Ukiona kuna funza nk kuna roho zipo hivyo pia
technology ya camera kali zinazojiendesha automatically zimesadia kuweza kupiga picha kama hizi za viumbe vya ajabu usiku! Je hivi ndio hao ziraili wa kiza? Huku kwetu tungehitimisha kwa kusema kwamba kachukuliwa msukule!