Kigarama
JF-Expert Member
- Apr 23, 2007
- 2,492
- 1,230
Kwa mila na desturi za duniani kuna mgawanyo wa Kazi na Majukumu ya wanawake au wanaume. Lakini kutokana na kubadilika kwa mitizamo ya wanadamu baadhi ya vitu vinatakwa kufanywa na jinsi zote. Kwenye Orodha ifuatayo nimeweka kazi na majukumu ya wanawake na wanaume kama kuna jambo hukulibalini nalo jenga hoja.
Kama unaona kuna kazi au majukumu ya Mwanamke au mwanaume ambayo sijaorodhesha yaweke na kama yapo niliyoyaorodhesha lakini nimekosea kuweka Mhusika wake yakosoe!!
- Kubadilisha nepi za mtoto na kumuogesha (Mwanamke)
- Kuosha vyombo, kupika,kutoa vyombo mezani (Mwanamke)
- Kutandika kitanda na usafi wa chumba (Mwanamke)
- KUfua nguo za mwenza na kuzipanga Kabatini (mwanamke)
- Kusimamia nidhamu ya watoto nyumbani (Mwanaume)
- KUtunza Bustani na Mazingira ya nyumba (Mwanaume)
- Kulima shambani (Mwanamke na mwanaume)
- Kulipa ada ya shule (Mwanaume)
- Kutoa hela za matumizi nyumbani (Mwanaume)
- Gharama za matumizi ya Gari (Mwanaume)
- Kulipa bili ya chakula Hotelini au pombe Baa (Mwanaume)
- Ulinzi wa nyumba (Mwanaume
Kama unaona kuna kazi au majukumu ya Mwanamke au mwanaume ambayo sijaorodhesha yaweke na kama yapo niliyoyaorodhesha lakini nimekosea kuweka Mhusika wake yakosoe!!