Zinduka: Siasa inanunua watu, Polepole naye kanunuliwa

Polepole ni kuwadi wa Jk na ni mtumwa wa Tiss.Ndio ameanza kuvua ngozi ya mabaka baka ya kondoo na kuonyesha sura yake ya mbwa mwitu.

Katika hilo kwa watu kama huyo polepole kuna kitu huwa najiuliza,iweje mtu/watu wamejitoa mhanga kukuletea ukombozi kwa hoja zinazoeleweka halafu bado wanakataliwa na wanakubali kuendelea kuibiwa na CCM?

Nasisitiza kuwa hakuna maendeleo bila mabadiliko.
 
Huyu kijana nilikua namkubali sana ila kanichefua hadi natamani niifute ID yake huku JF!
Nasikia uchungu sana kuona kijana mwenzangu mwenye fursa ya kusimamia ukweli na vijana wenzie kuiga mfano wake anapogeuka MPIGA DILI!
 
Wadau, kama channel 10, itaendelea kuleta wachambuzi ambao ni bias , kama Humphrey polepole, ni lazima tuikache hii TV kama tulivyo ikataa TBC na star TV , huyu jamaa kutumwa ila amekula vidonge vyake humu jamii forum na walio mpigia simu wamemchana, huyu jamaa siyo mchambuzi huwezi kumshambulia MTU eti ni fisadi , kwamba mwaka 1995 Mwalimu nyerere alimkataa, kama alikuwa fisadi kwanini alipewa uwazili Mbele ya macho ya nyerere, Polepole anasema eti kama CCM ingepitisha mgombea mwenye tuhuma angetembea tanzania nzima kuzungumza ukweli , kapigiwa simu akaulizwa kuwa Maghufuli ni msafi? Tuhuma za kuuza nyumba za taifa ? Repoti ya CAG ? Hakujibu anabaki kusema Lowasa ni fisadi? Nafikili watanzania kwa umoja wetu watu kama hawa akina polepole tuwakatae na kuwapuuza ikiwezekana kuwazomea kabisaa , na Television zinazo leta watu wa namna hii tuzichukie na tusifuatilie vipindi vyao, Tunataka mabadiliko kama ukawa siyo wasafi waache wachukue nchi pengine itakuja kuzaliwa kitu kingine Mbele ya safali siyo ccm ituaminishe kuwa ndio wako safi wakati ni mbwa mwitu na fisi wakubwa eti taiga kubwa kama hili liongozwe na mawazo ya Nape , magufuli na kinana watanzania tunamatatizo mengi ccm mnataka mtuaminishe na tuyasahau matatizo yetu wakati Wa uchaguzi, hamtatuweza hii ni mwendo mdundo mpaka kieleweke, kama Prof.Lipumba amezingua , na Dr.Slaa bado analegalega lakini watanzania bado wanaamini katk mabadiliko ndio kwanza watu wanaongezeka itakuwa Humphrey polepole mchumia tumbo alie tumwa na CCM hamtamzuia Lowasa kuiona ikulu hii ni safari ya mabadiliko nje ya CCM , mwendo mdundo mpaka Ikulu, UKAWA PAMOJA TUTASHINDA.


Tatizo tumefungwa akili zetu nut! Hazifikirii mbele wala nyuma. Ukweli siku zote huuma!! Tunashabikia UKAWA UKAWA bila kuingia ndani. Kila kitu anachosema MBOWE mnashangilia. ACHENI TABIA ZA KASUKU
 
Mkuu umeshindwa na wewe kuangalia Alama ya Nyakati ungemuelewa tu...Kwa sasa Habari ya Mjini, watu wana H A M U ya
m a b a d i l I k o na hata liwekwe jiwe watu wako radhi! Ni sawa mama siku zake za kujifungua zikifika haizuiliki! Ni nyakati za viongozi na wananchi kuwa makini kwa maneno matendo!

Alaah.. kumbe wana HAMU... nilidhani WAMEDHAMIRIA na WANAYATAKA mabadiliko.
 
Dah kumbe mnapenda kusifiwa tu kukoselewa hamtaki kweli nina amin zzk nae alikuwa anasimamia ukwel mkamuita msaliti dah sasa nan atawasemelea mabaya yenu sasa hakuna kizuri bila kuwa na ubaya!!watz tumeshaelewa tukutane october!
 
mbona hakusema kukurupuka kwa magufuli kuhusu samaki imasababisha tulipe samaki na meli sasa akiwa rais atakurupuka vingapi kama si hata kutuingiza migogoro na majirani zetu?
 
Kwani mnafikiri yeye hataki cheo katika serikali ya magufuli? Kikwete amemwonjesha asali alipomteua kwenye tume sasa anataka kuchonga mzinga!
 
kama umemuelewa polepole kachukue katiba ya warioba ambayo ndio chanzo wa haya yote utaelewa ana maanisha nini katika uteuzi wa mgombea ndo uje useme hayo yote.katiba ile imekiukwa

na hiyo ndio point ya Prof lipumba kujiuzuluu
 
Pasco, njoo uutendee haki huu uzi maana naona Polepole anahukumiwa kwa kutoa maoni yake kama Mtanzania huru
Mkuu Mzito Kabwela, tuna tatizo kubwa la waabudu watu humu, ambao wanawaonaale anaoaabudu ni miungu atu!, wakikosolewa tuu, unaonekana umefanya kosa la kumkufuru mungu!.

Ila pia Watanzania wameichoka CCM mpaka basi, hivyo kitendo cha yule 'jamaa yangu' ambaye alipokuwa CCM alionekana ni shetani, lakini sasa amehamia Chadema, amegeuka malaika!, tena ni malaika wa ukombozi, kwa wote wenye shauku na kiu ya ukombozi, mtu yoyote akikumbushia enzi za ushetani wa malaika huyu, kunapelekea wewe sasa ndio uonekane shetani!, hivyo kutafsiri anachofanya Polepole ni ushetani!.

Pasco
 
Mkuu Mzito Kabwela, tuna tatizo kubwa la waabudu watu humu, ambao wanawaonaale anaoaabudu ni miungu atu!, wakikosolewa tuu, unaonekana umefanya kosa la kumkufuru mungu!.

Ila pia Watanzania wameichoka CCM mpaka basi, hivyo kitendo cha yule 'jamaa yangu' ambaye alipokuwa CCM alionekana ni shetani, lakini sasa amehamia Chadema, amegeuka malaika!, tena ni malaika wa ukombozi, kwa wote wenye shauku na kiu ya ukombozi, mtu yoyote akikumbushia enzi za ushetani wa malaika huyu, kunapelekea wewe sasa ndio uonekane shetani!, hivyo kutafsiri anachofanya Polepole ni ushetani!.

Pasco

kaka umeandika vizuri sana
 
Tatizo Ndg Zetu Hawa Upande Wa Pili Ukawa Hawapendagi Kukosolewa Mbna Ccm Mnaikosoa Wanakubal Nyie Vp Kujiona Perfct Mda Wote
 
Alipokuwa upande wenu akiwananga CCM hamkusema mmemnunua shiingi ngapi ila alivyoanza kuwananga na nyinyi ndo mnaona kanunuliwa ..nyie mnastahili kucharazwa bakora sana, mbona hamumkashifu Mbowe kununuliwa kama mafungu ya nyanya?
 
Hivi Magufuli aliamka siku moja na kuamua kuuza nyumba za serikali? Serikali ya Tanzania kuanzia Nyerere ilishawahi kuuza nyumba zake?
Kama mantiki yako ya kufiriki ni hiyo basi hata Lowassa hakuamka siku moja na kuamua kuwa Richmond iwepo. Ni mchakato uliohusisha wakuu mbalimbali serikalini akiwemo mkuu kuliko wote.
 
Awali Polepole aliposema kuwa CCM ikimpitisha Lowassa atazunguka nchi nzima kupinga wote mlishangilia na kumuita jembe, leo hii kwa sababu Lowassa KANUNUA Chadema mnaona mtu yoyote akipinga ni kosa!
walifikiri ni fisadi ,ila keshafafanua na kama mna ushahidi peleka mahakamani
 
Kama katiba ya Warioba ndiyo anayoisimamia huyu Pole pole mbona ameshindwa kujibu hoja juu ya tuhuma za Magufuli za Uuzaji wa nyumba za serikali na juu ya upotevu wa Tsh. Billion 262 katika wizara yake ambazo hazionyeshi kazi yeyote iliyofanyika na fedha hizo na hii imetokana na ripoti ya CAG na hata Bungeni Magufuli alishindwa kujibu hoja hiyo je kwa tuhuma hizo huyo Magufuli anafaa kugombea Urais kupitia CCM kuringana na katiba ya Warioba?
Aliyeshinikiza nyumba ziuzwe kwa bei ya hawara ni pamoja na huyu lowassa mnayempigia debe hapa kajinunulia na sasa kazipangisha anakula kodi.tuweke kumbukumbu sawa ili tusijelaumiana mbele ya safari
 
Kama hutaki kuitazama ni wewe unayependa kusikia kitakachokufurahisha sisi tutaingalia Sana Tu as long as mafisadi wanasemwa wazi bila aibu.
 
Back
Top Bottom