Jambazi
JF-Expert Member
- Jan 18, 2014
- 16,654
- 18,800
Zimbabwe inasema inahitaji fedha kukabiliana na uwindaji haramu, lakini mashirika ya kutetea maslahi ya wanyama yameghadhabishwa na hatua hiyo.
Waziri wa mazingira Zimbabwe amesema tembo hao walisafirishwa kwa ndege hadi China kwenye ndege binafsi ya mizigo. Wahifadhi wanyama wanasema tembo wanahitaji uangalifu wa miaka kadhaa kutoka kwa wazazi wake na kwa hivyo kuwatenganisha tembo hao wadogo kutoka jamii zao katika umri mdogo ni kitendo cha ukatili na kitakacho kuwa na athari kubwa kwa wanyama hao.
Tembo hao wataishi katika mbuga ya wanyama karibu na mji uliopo kusini - Guangzhou. Inasemekana kwamba wanyama katika mbuga hiyo wanateswa na kuwekwa katika mzingira mabaya.
Raia wengi wa Zimbabwe wanaona tembo kama wanyama waharibifu wanaoharibu mazao na kuangusha miti.
Source: bbcswahili
Waziri wa mazingira Zimbabwe amesema tembo hao walisafirishwa kwa ndege hadi China kwenye ndege binafsi ya mizigo. Wahifadhi wanyama wanasema tembo wanahitaji uangalifu wa miaka kadhaa kutoka kwa wazazi wake na kwa hivyo kuwatenganisha tembo hao wadogo kutoka jamii zao katika umri mdogo ni kitendo cha ukatili na kitakacho kuwa na athari kubwa kwa wanyama hao.
Tembo hao wataishi katika mbuga ya wanyama karibu na mji uliopo kusini - Guangzhou. Inasemekana kwamba wanyama katika mbuga hiyo wanateswa na kuwekwa katika mzingira mabaya.
Raia wengi wa Zimbabwe wanaona tembo kama wanyama waharibifu wanaoharibu mazao na kuangusha miti.
Source: bbcswahili