Zijue tabia za Mtanzania halisi

Zijue tabia za Mtanzania halisi

Ni washirikina sana na hawapendi maendeleo ya mtu mwingine .

Ni waigaji sana na hawapemdi watu wengine wanaojipenda wao Kwa wao

Ile ya eti watanzania ni wakarimu jidanganyeni ila vingine vyote nisawa na sio sisi tu mahali pengine baadhi ya vitu wanafanya
 
(1) Kukojoa nyuma ya nyumba.

(2) Mke kulala karibu na ukuta

(3) Kuweka mifagio nyuma ya mlango.

(4) Ukitajirika, watu husema una chumba cha kulala cha siri ambacho hakuna mtu anayeingia.

(5) Unapozeeka unashukiwa kuwa ni mchawi.

(6) Unapooga, watakuuliza ikiwa unaenda mahali fulani.

(7) Kuweka baadhi ya vyombo kando mahususi kwa ajili ya wageni.

(8) Kuhesabu vipande vya nyama ili kuhakikisha vinatolewa kwa usawa.

(9) Hakuna kifo cha asili kinachotokea katika Afrika. Adui yako daima ndiye chanzo.

(10) Kuhesabu pesa baada ya kutoa kutoka kwa ATM.

(11) Kuoa mrembo ni sawa na kuolewa na kahaba.

(12) Kutoa viatu wakati wa kutembea kwenye matope na kuingia ndani ya nyumba.

(13) Kuna baadhi ya sehemu maalum za nyama ya kuku ambazo zimetengwa kwa ajili ya mume k.m paja la kuku.

(14) Kununua nguo mpya kunapokuwa na sikukuu

(15) Mtu anapopewa maikrofoni, kwanza hupulizia hewa ndani yake au kuigonga kwa kidole ili kuona ikiwa inafanya kazi licha ya mtumiaji wa awali kuwa ametumia maikrofoni sawa.

(16) Kufagia kiwanja kizima hata wakati sehemu zingine si chafu.

(17)Kuangalia kushoto na kulia wakati wa kuvuka barabara ya njia moja.

(18) Kuweka chupa tupu ya plastiki baada ya kunywa maji kwa matumizi ya baadaye

(19) Kuweka kiti maalum ndani ya nyumba kwa ajili ya mume.

(20).Kujisikia fahari wakati wa kukaa karibu na mzungu ndani ya basi.

Ongezea zingine.....
tabia kama hizi kwa kingereza zinaitwa stereotypes. zinatofautiana kutoka jamii moja kwenda nyingine, raia wa nchi moja na nyingine. hata raia wa mataifa ya wazungu, wana stereotype zao.

kwa mfano mimi nashangazwa na wanaigeria kupitia ile tabia yao ya kuzungumza kwa punch kubwa na kusonya.
 
tabia kama hizi kwa kingereza zinaitwa stereotypes. zinatofautiana kutoka jamii moja kwenda nyingine, raia wa nchi moja na nyingine. hata raia wa mataifa ya wazungu, wana stereotype zao.

kwa mfano mimi nashangazwa na wanaigeria kupitia ile tabia yao ya kuzungumza kwa punch kubwa na kusonya.
Na hujawaona wengine wakicheka sana mpaka alale chini
 
Simu ikilia hata kama upo kawaida wengi hudanganya kuwa yuko sehemu tofauti

Kuna mtoto aliniambia uncle yaani baba muongo sijapata kuona

# Misibani watu kushindana kutoa sauti kwa kulia hii huniacha hoi

# Kuweka mikono kichwani ukipatwa na janga
Hii nayo huwa naona kwa wengi hata Senga ndio zake
 
Kurudia kupima nyama kwa Mangi baada ya kutoka buchani ili kuhakiki kama kweli imefika kipimo.
Kununu chakula mfano mchele kilo mbili ila ufungwe tofauti hata kama unaenda kupikwa kwa pamoja eti ukifungwa kilo moja moja utakuwa mwingi.
 
Kurudia kupima nyama kwa Mangi baada ya kutoka buchani ili kuhakiki kama kweli imefika kipimo.
Kununu chakula mfano mchele kilo mbili ila ufungwe tofauti hata kama unaenda kupikwa kwa pamoja eti ukifungwa kilo moja moja utakuwa mwingi.
Kupiga mswaki halafu unapiga unakuwa kama vile unatapika unatoa kabisa na sauti naichukia hii tabia mpaka basi.
Kumuagiza mtu kitu au mtoto halafu unamwambia amwambie muuzaji fulani ndio kanituma ili uongezwe.
 
Hiyo namba 2 ,nilazima kwani mwanamke anahitaji ulinzi analalaje mwazoni kitanda unataka akiiona nge au nyoka akuvuruge
 
Ile unaosha vyombo mtu akaongeza vingine ni full kununa na kulalamika😂😂😂
Kwa waoshaji vyombo ..sufuria zinaoshwa mwishoni.

Katika ufuaji nguo Kama soksi..braa..vest mashati kufuliwa mwanzoni😂
 
Kurudia kupima nyama kwa Mangi baada ya kutoka buchani ili kuhakiki kama kweli imefika kipimo.
Kununu chakula mfano mchele kilo mbili ila ufungwe tofauti hata kama unaenda kupikwa kwa pamoja eti ukifungwa kilo moja moja utakuwa mwingi.
Hii ni muhimu, wagogo wauza nyama Buchani wezi sana. Kuna siku nilienda kupima sehemu nyingine nikakuta robo nzima wameiba, mbona niliwarudia Buchani na wakakubali kuiongeza 😅
 
--Kitanda kuwekwa ukutani.

--Ukinywa soda unaitazama Kila baada ya kupiga funda Moja.
 
Back
Top Bottom