Zijue faida 6 za kula pilipili

Ben Zen Tarot

JF-Expert Member
Dec 13, 2014
3,907
6,700
Maalumu kwa wale watu wapenda na watumiaji wa pilipili ambao hutumia bila kufahamu faida zinazotokana na kiungo hiki chenye ladha ya uchachu na ukali lakini ndiyo kiungo chenye kuongeza hamu ya kuendelea kula chakula.

Capsaicin ndiyo kiambata ambacho huipa pilipili ladha yake ya uchachu pamoja na kazi yake ya kuongeza ladha ya chakula.

Kwa mujibu wa tafiti mbalimbali zilizofanywa na wanasayansi wamegundua faida 6 zitokanazo na ulaji wa pilipili kwenye mwili wa binadamu, kama zifuatazo.

Hupambana na maumivu na uvimbe

Capsaicin huziondolea nguvu neuropeptides ambazo ndizo husababisha maumivu na kuvimba kwa sehemu mbalimbali mwilini.

2. Huzuia kuziba kwa mishipa ya pua

Capsaicin inajulikana kwa kupambana na kazi mbalimbali za bakteria mwilini ambazo nyingi husababisha kuathirika kwa sehemu ya wazi iliyopo kwenye mifupa hasa kwenye pua, pamoja na kazi yake ya kuunguza/ kuchemsha mwili, pia husaidia kuunguza ute unaoweza kusababisha kuziba kwa pua hivyo kuondoa, kupunguza kabisa maumivu ya sehemu hii ya mwili.

3. Husaidia mmeng’enyo wa chakula na kuondoa gesi

Husaidia kusisimua sehemu zinazozalisha enzymes mbalimbali tumboni hivyo kukifanya chakula kisibaki kimehifadhiwa tumboni kwa muda mrefu kikisubiri hadi pale ambapo enzymes hizi zitakapo zalishwa, pia huua bakteria wanaoweza kushambulia chakula hiko kisichomeng’enywa hivyo kupunguza uwezekano wa tumbo kujaa gesi.

4. Huulinda moyo

Ulaji wa pilipili kwa wingi huufanya moyo uwe imara sana katika kufanya kazi yake, husaidia pia kupunguza msukumo wa damu, kuunguza cholesterol na kuzuia kuganda kwa damu pamoja na kazi hizi huzinyima nguvu gene zinazosababisha kuziba kwa mishipa inayotoa damu kwenye moyo na kuisambaza sehemu mbalimbali za mwili hivyo kuondoa uwezekano wa kupatwa na shambulio la moyo na kiharusi.

5. Husaidia kutunza uzito sahihi wa mwili

Utafiti unasema utumiaji wa pilipili husaidia kusisimua protini aina ya TRPV1 ambazo ndizo hufanya kazi ya kutunza uzito sahihi wa mwili , kulinda kiasi cha sukari kinachofaa na mafuta yanayosababisha kuongezeka kwa uzito.

6. Husaidia kupambana na saratani ya tezi dume

Pilipili huingilia gene zinazopelekea uwepo wa tezi dume, Utafiti uliopo mpaka saivi unaonesha kuwa zaidi ya 80% ya seli zinazosababisha saratani hii hufa baada ya kuwekewa kemikali hii ya pilipili.

pl.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi napenda sana pilipili ila nisisikia watu wanasema ukila sana unakuwa katika rist ya kupata kansa ya koo,sijui vipi hii
Kama inafyeka saratani ya tezi dume na ya koo inafyekwa pia,hata hivyo si kweli kwamba inasababisha saratani ya koo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom