Zifahamu njia za Uzazi wa Mpango (Family Planning Methods)

kwitandula

Member
May 24, 2020
30
35
Inaletwa kwako na mkunga,

Habari wanajukwaa, awali ya yote poleni sana na majukumu ya kila siku, leo ningependa niwape mada fupi kuhusu uzazi wa mpango, na uzazi wa mpango ninaowaletea leo ni ule wa kisasa.

Nini maana ya uzazi wa mpango
Ni njia ambazo mke na mume wanaamua kuzitumia ili kuzuia mimba zisizotarajiwa,kuweka nafasi kati ya mtoto na mtoto ambapo kiafya inashauriwa wapishane kuanzia miaka miwili(wa mwanzo atakua ameshafikia umri wa kuacha kunyonya), kumpa muda mama aliyejifungua kuujenga mwili wenye afya njema na kupumzika,uchumi n.k

Aina za njia za mpango
1. Njia za muda mfupi kama; kondomu,vidonge
2. Njia za muda mrefu kama;vipandikizi na lupu
3. Njia za kudumu(kufunga kabisa uzazi kwa mwanamke au mwanaume)

Ufafanuzi
Njia za muda mfupi ni zile ambazo mtumiaji atatakiwa atumie kila siku(vidonge) ili kuzuia mimba bila kukosa na ikitokea umesahau kunywa basi itakupasa utumie kondomu endapo utahitaji kujamiiana

Njia za muda mrefu kama vipandikizi huwekwa kwenye msuli wa mkono, kipo cha miaka mitatu na miaka mitano(vinakua viwili), kwa upande wa lupu hiki ni kijiti chenye muundo wa T-shape ambacho kinaingizwa kupitia uke na kuwekwa kwenye mji wa mimba(uterus) kinafanya kazi hadi miaka kumi na mbili

Njia za kudumu hizi kabla ya kuchagua kutumia inahitaji mwanamke au mwanaume kuamua na kuwa na msimamo na uamuzi na unaochukua kwa sababu ukishafungwa hauwezi kufungua tena na hautakua na uwezo wa kupata mtoto tena.

Note:
Kumekua na dhana potofu katika jamii juu ya utumiaji wa uzazi wa mpango hasa mwanaume anapoambiwa na mwenza wake juu ya matumizi ya njia hizi

1. Njia za uzazi wa mpango hazileti Kansa kama wengi wanavyosema sababu za kansa nyingi hadi sasa haijulikani japo kwa baadhi ya kansa kama cervical cancer(kansa ya shingo ya kizazi inasabishwa na virus-human papiloma virus na ni sexually transmitted)

2. Vipandikizi, lupu kupotelea mwilini sio kweli japo kama utaweka na Mtoa huduma ambae hana ujuzi sana hasa kwa vipandikizi muda wa kuweka anaweza kukiingiza ndani sana ambapo muda wa kutoa itachukua muda kukitoa

Ushauri
•Uzazi wa mpango unapangwa na mke na mume hivyo wote mnapaswa kuhudhuria kliniki ya uzazi wa mpango kwa ajili ya kupata elimu na kuchagua njia itakayowafaa

•mpeleke binti yako ambaye amefikia umri wa kupevuka kliniki ya uzazi wa mpango hasa yule anaeonesha dalili za mapenzi ili kuondoa aibu ya binti yako kupata mimba za utotoni usione aibu!

• huduma za uzazi wa mpango ni bure

Karibuni kwa maoni, nyongeza na maswali na ambapo nimekosea unaweza sahihisha.
 
Kwanini baadhi ya wanawake wanaotumia sindano huwa hawaingii bleed kila mwezi? Kuna mahusiano gani Kati ya kuongeza tumbo na matumizi ya sindano?

Hakuna namna nyingine mwanaume anaweza kutumia njia za uzazi wa mpango tofauti na condoms pamoja na ile njia ya kufunga moja kwa moja? Kama ilivyo kwa wanawake wananjia zaidi ya moja
 
Kwanini baadhi ya wanawake wanaotumia sindano huwa hawaingii bleed kila mwezi?
Kuna mahusiano gani Kati ya kuongeza tumbo na matumizi ya sindano?
Hakuna namna nyingine mwanaume anaweza kutumia njia za uzazi wa mpango tofauti na condoms pamoja na ile njia ya kufunga moja kwa moja? Kama ilivyo kwa wanawake wananjia zaidi ya moja

Asante kwa kuuliza ipo hivi njia zote za uzazi wa mpango zina vichocheo/hormone (estrogen na progesterone) ambazo kazi yake kubwa ni kufanya mazingira ya mji wa mimba usiwe rafiki kutungisha/kusupport mimba na kwa mwanamke kila mwezi mji wa mimba unatengeneza layers/kuta ambapo mimba isipotungishwa unajivunja ndio inatoka ile period so baada ya kutumia uzazi wa mpango ule ukuta utatengenezwa kidogo(kwa wale wanaopata matone ya damu muda wa period.

Au hautatengenezwa kabisa kwa sababu hakuna mimba inayotegemewa kukua hapo na kwa mwanamke alietumia njia ya uzazi wa mpango na asione period kabisa hiyo inamaanisha kuwa njia ya uzazi wa mpango imefanya kazi vizuri
Note: hii ni kwa njia zote sio sindano pekee.

Kuhusu kuongeza tumbo na sindano sijaona utafiti uliothibitisha hilo japo kama nilivyosema awali hizi njia zina vichocheo ukiachana na lupu so itategemea na mwili wa mtumiaji na sababu nyingine.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Asante kwa kuuliza ipo hivi njia zote za uzazi wa mpango zina vichocheo/hormone(estrogen na progesterone) ambazo kazi yake kubwa ni kufanya mazingira ya mji wa mimba usiwe rafiki kutungisha/...
Vipi kuhusu njia za uzazi kwa mwanaume haujanijibu. Niongeze swali lingine dogo; Kwanini inachukua muda sana mwanamke kushika mimba baada ya kuacha kutumia sindano?
 
Vipi kuhusu njia za uzazi kwa mwanaume haujanijibu.
Nionge swali lingine dogo; Kwanini inachukua muda sana mwanamke kushika mimba baada ya kuacha kutumia sindano?
Sindano ina dozi kubwa kulinganisha na njia nyingine hivyo kuisha kwake mwilini unachukua muda kidogo na kwa kawaida mwanamke anayetumia njia ya uzazi wa mpango wa sindano hatakiwi kuchoma sindano zaidi ya nane
 
Vipi kuhusu njia za uzazi kwa mwanaume haujanijibu.
Nionge swali lingine dogo; Kwanini inachukua muda sana mwanamke kushika mimba baada ya kuacha kutumia sindano?
Mwanaume hana mji wa mimba wa kubeba ujauzito njia zote za uzazi wa mpango kazi kuu ni kufanya mazingira ya mji wa mimba usiwe rafiki kutungisha mimba
 
Vipi kuhusu njia za uzazi kwa mwanaume haujanijibu.
Niongeze swali lingine dogo; Kwanini inachukua muda sana mwanamke kushika mimba baada ya kuacha kutumia sindano?
Ni kawaida mwanamke asipopata ujauzito kwa kipindi cha miezi 10 hadi mwaka mmoja baada ya kuchoma sindano ya mwisho kama nilivyosema sindano ina dozi kubwa 150mg kwa sindano ya msuli na 104mg kwa sindano ya chini ya ngozi zaidi ya muda huo itabidi akawaone wataalamu wa afya uchunguzi zaidi
 
Ni kawaida mwanamke asipopata ujauzito kwa kipindi cha miezi 10 hadi mwaka mmoja baada ya kuchoma sindano ya mwisho kama nilivyosema sindano ina dozi kubwa 150mg kwa sindano ya msuli na 104mg kwa sindano ya chini ya ngozi zaidi ya muda huo itabidi akawaone wataalamu wa afya uchunguzi zaidi
Kwa maelezo yako maana yake ni kwamba sindano ni njia yenye matokeo ya haraka lakini pia upande mwingine madhara yake ni makubwa ukilinganisha na njia nyingine za uzazi?

Je, inaruhusiwa mwanamke kubadilisha njia ya uzazi ya wa mpango nyingine baada ya kumaliza hizo sindano nne?

Na je, ikitokea imechukua muda mwanamke kushika mimba baada ya matumizi ya sindano dawa gani anaweza kutumia ili kurahisisha zoezi la kushika mimba?
 
Kwa maelezo yako maana yake ni kwamba sindano ni njia yenye matokeo ya haraka lakini pia upande mwingine madhara yake ni makubwa ukilinganisha na njia nyingine za uzazi?...
Njia yeyote ya uzazi mpango haina madhara ila ni maudhi madogo madogo na si kila mwanamke atakaetumia atachelewa kupata ujauzito,kama nilivyojibu awali baada ya kutumia sindano kutopata ujauzito kwa kipindi cha miezi kumi hadi mwaka mmoja ni hali ya kawaida zaidi ya hapo nenda hospital kwa ajili ya uchunguzi zaidi shida inaweza kuwa sio sindano ila matatizo mengine.

Pia mwanamke anaetumia sindano anatakiwa achome mwisho nane tu which means njia ya sindano atumie kwa miaka miwili baada ya hapo achague njia nyingine ya uzazi wa mpango kama nilivyoainisha kwenye uzi.na matokeo ya njia zote ni ya haraka ila wanawake wengi wanapenda sindano kwa sababu anachoma kila baada ya miezi mitatu ukilinganisha na matumizi ya njia nyingine na namna ya uwekaji wake/utumiaji
 
Swali kuhusu njia ya uzazi w mpango kwa mwanaume bado sijaeelewa nakazia swali kinamna hii.

Hamna njia itakayofanya mwanaume atoe sperm ambazo zitashindwa kurutubisha yai.... Yaan maan yangu ni hii sitaki mwenza wangu atumie njia ya uzazi wa mpngo ila nataka mimi ndio nishindwe kumpa ujauzito.

Achana na njia ya kukata mirija kwa mwanaume au condom hana sindano ambayo utaua zile sperm au kufanya zisiwe na uwezo wa kurutubisha yai.
 
Njia ya vidonge bado ina utata.... Hamna vidonge ambavyo unatumia kabla ya tendo ? Ukiacha vile unameza tuu mwezi mzima
 
Swali kuhusu njia ya uzazi w mpango kwa mwanaume bado sijaeelewa nakazia swali kinamna hii

Hamna njia itakayofanya mwanaume atoe sperm ambazo zitashindwa kurutubisha yai.... Yaan maan yangu ni hii sitaki mwenza wangu atumie njia ya uzazi wa mpngo ila nataka mimi ndio nishindwe kumpa ujauzito

Achana na njia ya kukata mirija kwa mwanaume au condom hana sindano ambayo utaua zile sperm au kufanya zisiwe na uwezo wa kurutubisha yai
Modern family planning METHODS kwa mwanaume ni hiyo tu vasectomy,kondomu na kwa upande wa natural ni withdrawal
 
Back
Top Bottom