Zifahamu athari za kucheza kamari! Tafadhali chukua hatua

Michael Chairman

JF-Expert Member
Apr 11, 2015
922
581
Kubeti ama kucheza kamari umekuwa mchezo maarufu sana hapa nchini , na unaweza ukasema ni madawa ya kulevya mapya yaliyoibuka.

wachezaji wengi wa mchezo huu huamini kwamba watabahatika wakiachagua namabari Fulani au wakitumia uwezo Fulani (ushilikina) , na wengine wameenda mbali humuomba Mungu awasaidie kushinda mchezo waliouchagua.

Pamoja na kwamba kila kitu kinafaida na hasara mchezo huu wa kubeti unazo hasara nyingi sana ukilinganisha na faida atakayoipata mchezaji na hata mchezeshaji moja ya hasara kubwa anayoipata mchezaji hudhani kuwa akishinda fedha za kamari amaeshinda fedha za mwekezaji wa mchezo huu kumbe hali halisi hushinda fedha za wachezaji wenzake yaani wacheza kamari wengine na hii hutengeneza mazingira ya (win -lose mind ) na SI (win -win mind).

watafiti wamebaini kuwa kuna athari kubwa sana kwa binadamu kuendekeza kucheza kamari ama kubeti na athari hizi ni muhumu kuzitilia maanani kwani kutokufanya hivyo ni kwa hasara yako tu na si kuna hasara inakwenda kwa mwingine. Baadhi ya Athari hizo zinaelezwa kuwa ni pamoja na .....

1. Kushuka moyo.
hii inatokana na mchezaji kupata matokeo ama mkazo wa kile amabacho hakukitalajia ama kushindwa au kushinda na mara kwa mara huwa ni kushindwa kunako mpelekea kuwa na mawazo mengi na kukosa raha, kukata tama , kujiona yeye si kitu kutokana na kushindwa kwenye mchezo huo.

2. Kuamini na kutegemea bahati nasibu kuwa ndiyo nanga ya mafanikio kwenye maisha.
michezo hii inawafanya wachezaji kuondoa matumaini kwenye juhudi na maarifa katika kufanya kazi na kuwa wabunifu kubuni vitu vipya ama bidhaa mpya na badala yake huegemeza juhudi zao kwenye kutegemea bahati nasibu ndiyo mkombozi wao katika kufanikiwa kimaisha na hii inawafanya wengi kuchelewa kimaisha kutokana na kuwekeza muda miwingi huko.

3. Huwachochea watu wapende fedha kupita kiasi.
kupenda fedha si kosa ama dhambi bali kupenda kupita kiasi na kuifanya hiyo ndiyo kila kitu huwafanya wengi wa watu kujiingiza kwenye michezo michafu au mazingira mabaya , kisa tu anataka kupata fedha. Pia kubeti kumewafanya wengi wa wachezaji kupenda kupata fedha nyingi kutokana na kubeti huko na wamejikuta wanapoteza fedha nyingi badala ya kupata nyingi.

4. Kuwa mraibu ama mlevi wa kupindukia.
kitendo cha kucheza kamari na kuendelea kucheza hukufanya uwe mraibu mlevi usiysikia kitu chochote na mwisho wa kila kitu ni wewe na kamari ama na kubeti , hivyo ni muhimu sana kama umeuanza mchezo huu acha mara moja kabla haujachelewa na mambo yakawa mabaya zaidi.

my take ....ukizoea vya kunyonga vya halali hutaviweza....
nini maoni yako kuhusiana na hili...?
th
 
Kubeti ama kucheza kamari umekuwa mchezo maarufu sana hapa nchini , na unaweza ukasema ni madawa ya kulevya mapya yaliyoibuka.
wachezaji wengi wa mchezo huu huamini kwamba watabahatika wakiachagua namabari Fulani au wakitumia uwezo Fulani (ushilikina) , na wengine wameenda mbali humuomba Mungu awasaidie kushinda mchezo waliouchagua.
Pamoja na kwamba kila kitu kinafaida na hasara mchezo huu wa kubeti unazo hasara nyingi sana ukilinganisha na faida atakayoipata mchezaji na hata mchezeshaji moja ya hasara kubwa anayoipata mchezaji hudhani kuwa akishinda fedha za kamari amaeshinda fedha za mwekezaji wa mchezo huu kumbe hali halisi hushinda fedha za wachezaji wenzake yaani wacheza kamari wengine na hii hutengeneza mazingira ya (win -lose mind ) na SI (win -win mind).
watafiti wamebaini kuwa kuna athari kubwa sana kwa binadamu kuendekeza kucheza kamari ama kubeti na athari hizi ni muhumu kuzitilia maanani kwani kutokufanya hivyo ni kwa hasara yako tu na si kuna hasara inakwenda kwa mwingine. Baadhi ya Athari hizo zinaelezwa kuwa ni pamoja na .....
1.kushuka moyo.
hii inatokana na mchezaji kupata matokeo ama mkazo wa kile amabacho hakukitalajia ama kushindwa au kushinda na mara kwa mara huwa ni kushindwa kunako mpelekea kuwa na mawazo mengi na kukosa raha, kukata tama , kujiona yeye si kitu kutokana na kushindwa kwenye mchezo huo.
2.kuamini na kutegemea bahati nasibu kuwa ndiyo nanga ya mafanikio kwenye maisha.
michezo hii inawafanya wachezaji kuondoa matumaini kwenye juhudi na maarifa katika kufanya kazi na kuwa wabunifu kubuni vitu vipya ama bidhaa mpya na badala yake huegemeza juhudi zao kwenye kutegemea bahati nasibu ndiyo mkombozi wao katika kufanikiwa kimaisha na hii inawafanya wengi kuchelewa kimaisha kutokana na kuwekeza muda miwingi huko.
3.huwachochea watu wapende fedha kupita kiasi.
kupenda fedha si kosa ama dhambi bali kupenda kupita kiasi na kuifanya hiyo ndiyo kila kitu huwafanya wengi wa watu kujiingiza kwenye michezo michafu au mazingira mabaya , kisa tu anataka kupata fedha. Pia kubeti kumewafanya wengi wa wachezaji kupenda kupata fedha nyingi kutokana na kubeti huko na wamejikuta wanapoteza fedha nyingi badala ya kupata nyingi.
4. kuwa mraibu ama mlevi wa kupindukia.
kitendo cha kucheza kamari na kuendelea kucheza hukufanya uwe mraibu mlevi usiysikia kitu chochote na mwisho wa kila kitu ni wewe na kamari ama na kubeti , hivyo ni muhimu sana kama umeuanza mchezo huu acha mara moja kabla haujachelewa na mambo yakawa mabaya zaidi.
my take ....ukizoea vya kunyonga vya halali hutaviweza....
nini maoni yako kuhusiana na hili...?
th
Hii Topic ya Maana sana na inawahusu vijana wa kileo wazee wa mikeka
 
Back
Top Bottom