Ziara ya Rais Magufuli mkoa wa Simiyu; Aamuru hospitali ya bajeti ya tsh. 46bn ijengwe kwa tsh. 10bn

Slas Nature

Member
Oct 18, 2013
36
72




Magufuli, Simiyu: Niwaahidi hatutowaangusha, nimekuja kuwashuku na nafikiri shukrani zangu mmezipokea.

-Magufuli, Simiyu: Yale yetu tuliyoyaahidi kwenye ilani ya chama cha mapinduzi tutayatimiza.

-Magufuli: Ukichukua hatua zozote wapo watakaolalamika, sitabadilika, msimamo wangu uko palepale, tunataka kutengeneza Tanzania mpya.

-Magufuli: Bariadi inaongoza kwa kutengeneza pamba, dhahabu zipo, hifadhi kubwa ya taifa, Kwanini Tanzania tuwe maskini?.

-Magufuli: Kila mmoja anapenda maisha mazuri na huduma nzuri, sisi viongozi tuna wajibu wa kutekeleza.

-Magufuli: Haijawahi kutokea Tanzania kupanga bajeti 40% kwenda kwenye maendeleo, lazima kuna watu wamekwazika.

-Magufuli: Mnaosikia wanalalamika walikua wananufaika na hizo fedha, ilifikia mahali hatuna hata ndege.

-Magufuli: Mnaosikia wanalalamika walikua wananufaika na hizo fedha, ilifikia mahali hatuna hata ndege nchi ya watu milioni 50.

-Magufuli: Hakuna nchi yoyote duniani iliyofanikiwa kwenye utalii bila kuwa na shirika lake la ndege, tumeamua kuinua utalii.

-Magufuli: Nilikua naongea na waziri, tuone uwezekano wa kujenga kiwanja cha ndege hapa Bariadi mwaka kesho.

-Magufuli: Katika maendeleo machungu lazima yawepo, niwaombe radhi walioumia lakini ni kwa ajili ya maendeleo ya Simiyu.

-Magufuli: Anaetangaza njaa ni Rais, mie ndio nimepewa jukumu la kuwaongoza watanzania.

-Rais Magufuli: Wataandika lakini sitasikiliza, siasa tuziacha, twende na ukweli.

-Rais Magufuli: Nataka niwaeleze ukweli, nimesomewa ripoti hospitali itatumia bilioni 46, hiki kitu hakiwazekani.

-Rais Magufuli: Nasema haiwezekani, nataka hospitali hiyo ikamilike sio kwa pesa hizo mlizozipanga. Ntaleta bilioni kumi jengo liishe.

-Rais Magufuli: Kama yupo kiongozi wa TBA anaweka estimates kubwa, mfukuze kazi, barabara ikifunguliwa ajali zitaongezeka, hospitali lazima.
 
Hivi sasa TBC1 iko live ikirusha mkutano wa hadhara wa Raisi Magufuli huko mkoani Simuyu.

Tukirudi nyuma tuliambiwa kurusha live vikao vya Bunge ni gharama na pia watu wanatakiwa wafanye kazi.

Sasa leo ikiwa ni siku ya kazi kwanini ziara ya Raisi Magufuli inarushwa live kutoka huko Simiyu?

Je,hapa hakuna gharama?


Hii ni nchi ya ajabu sana!
 
Hahaha hiii ndo bongo aisee
Tupo busy kubadilisha malaika wawe mashetani patamu apo
Kila siku tunapanga timu
Hatufungi wala nn
 
Mbona akiwa Kagera hizi Tv hazikwenda live ama kunani ( )??
 
Hivi sasa TBC1 iko live ikirusha mkutano wa hadhara wa Raisi Magufuli huko mkoani Simuyu.

Tukirudi nyuma tuliambiwa kurusha live vikao vya Bunge ni gharama na pia watu wanatakiwa wafanye kazi.

Sasa leo ikiwa ni siku ya kazi kwanini ziara ya Raisi Magufuli inarushwa live kutoka huko Simiyu?

Je,hapa hakuna gharama?


Hii ni nchi ya ajabu sana!
Wanaweweka mbele ubinafsi .....pia wanaogopa kukosolewa.....
 
Nakaa vizuri nimsikilize.

Nimependa aliyoongelea juu ya ng'ombe, mtu analipwa kusrma ng'ombe 17,000 wamekufa na njaa na inatangazwa...swali lake alipokufa wa kwanza, then wapili, watatu...elfu moja hadi 17,000 kwanini hakufikiria kuwapandisha hata ng'ombe elfu moja kuanzia hapo akawauze ili ajipatie pesa

So ni kwamba alikaa ajasubiri wote wafe sababu hana maji na chakula...


Ya jengo la hospitali nayo hiyo kali, mbavu zangu billion 46 wakati majengo udsm block nyingi za floor nne nne zimejengwa kwa billion 10. So kasema atawapa billion 10 na chuo hawakihitaji wanafunzi wakasome Bugando, UDOM etc waje wafanye kazi pale ndipo pa kuanzia.

JPM uzidi kubarikiwa, na wale walijiumauma na ya maji lol
 
Back
Top Bottom