Ojuolegbha
JF-Expert Member
- Sep 6, 2020
- 740
- 479
Mbunge wa Jimbo la Nkenge, tarehe 09 Agosti, 2023 ameendelea na ziara yake ya Jimbo katika Kata ya Kassambya iliyopo Wilayani Missenyi, Kagera.
Katika ziara yake amehudhuria Kikao cha ndani CCM Kata ya Kassambya, amewapongeza viongozi wa CCM wa Kata hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kukisaidia Chama Cha Mapinduzi na Serikali kuwaongoza Wananchi. Katika Kikao hicho Mhe. Mbunge wamewakabidhi viongozi vitendea kazi ikiwemo Bendera za Chama, Sare za Chama (T-shirt), Karatasi (Ream papers), Kalamu, Mipira kwa ajili ya Michezo, Runinga Kwa ajili ya Wazee wa Bunazi
Pia Mbunge Kyombo amefanya mkutano wa hadhara na Wananchi wa Kata ya Kassambya na kusikiliza kero zao. Mbunge Kyombo amewaeleza Wananchi waendelee kukiamini Chama Cha Mapinduzi kwani chama hicho kina dira na Mipango mizuri ya Kuleta Maendeleo kwa Taifa la Tanzania.
Wananchi wa Kata ya Kassambya wamemshukuru Mhe. Mbunge Kwa kazi kubwa ya Uwakilishi anayofanya Bungeni na kuhaidi kutoa ushirikiano wao kila wakati kwa Maslahi mapana ya Taifa. Pia, Wananchi hao wamemkabidhi Mhe. Mbunge Zawadi ya Mbuzi ikiwa ni ishara ya kuendeleza Umoja na Ushirikiano.
Mbunge Florent Kyombo amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya ya Kuleta Maendeleo katika Nchi yetu.View attachment 2714393View attachment 2714394View attachment 2714397View attachment 2714395View attachment 2714396View attachment 2714398View attachment 2714399View attachment 2714400
Katika ziara yake amehudhuria Kikao cha ndani CCM Kata ya Kassambya, amewapongeza viongozi wa CCM wa Kata hiyo kwa kazi kubwa wanayoifanya katika kukisaidia Chama Cha Mapinduzi na Serikali kuwaongoza Wananchi. Katika Kikao hicho Mhe. Mbunge wamewakabidhi viongozi vitendea kazi ikiwemo Bendera za Chama, Sare za Chama (T-shirt), Karatasi (Ream papers), Kalamu, Mipira kwa ajili ya Michezo, Runinga Kwa ajili ya Wazee wa Bunazi
Pia Mbunge Kyombo amefanya mkutano wa hadhara na Wananchi wa Kata ya Kassambya na kusikiliza kero zao. Mbunge Kyombo amewaeleza Wananchi waendelee kukiamini Chama Cha Mapinduzi kwani chama hicho kina dira na Mipango mizuri ya Kuleta Maendeleo kwa Taifa la Tanzania.
Wananchi wa Kata ya Kassambya wamemshukuru Mhe. Mbunge Kwa kazi kubwa ya Uwakilishi anayofanya Bungeni na kuhaidi kutoa ushirikiano wao kila wakati kwa Maslahi mapana ya Taifa. Pia, Wananchi hao wamemkabidhi Mhe. Mbunge Zawadi ya Mbuzi ikiwa ni ishara ya kuendeleza Umoja na Ushirikiano.
Mbunge Florent Kyombo amemshukuru Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kazi kubwa anayoifanya ya Kuleta Maendeleo katika Nchi yetu.View attachment 2714393View attachment 2714394View attachment 2714397View attachment 2714395View attachment 2714396View attachment 2714398View attachment 2714399View attachment 2714400