Zelensky asema vita vinakuja nchini Urusi

Zelensky asema vita vinakuja nchini Urusi

Umkonto

JF-Expert Member
Joined
Dec 27, 2018
Posts
3,238
Reaction score
5,621
My take!

Je, Zelensky anawaza nini mpaka kuamua kuanza kushambulia Urus wakati anajua kabisa Putin alishaonya hataki Urusi ishambuliwe?

Putin na Zelensky fanyeni mazungumzo hatutaki vita vikubwa.

Habari kamili.

Rais wa Ukraine Volodymr Zelensky ameonya kwamba vita vinakuja nchini Urusi baada ya shambulio la mapema la ndege zisizo na rubani kwenye mji mkuu wa Moscow.

Bw Zelensky alisema mashambulizi dhidi ya eneo la Urusi ni "mchakato usioepukika, wa asili na wa haki kabisa" wa vita kati ya nchi hizo mbili.

Wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema ndege tatu zisizo na rubani za Ukraine zilidunguliwa siku ya Jumapili, na mbili zilianguka kwenye afisi.

Uwanja wa ndege wa Vnukovo, kusini magharibi katikati mwa jiji, pia ulifungwa kwa muda mfupi.

Meya wa jiji hilo Sergei Sobyanin alisema maeneo ya mbele ya majengo mawili ya ofisi yaliharibiwa kidogo.

Picha kutoka eneo la tukio zinaonyesha kuwa madirisha kadhaa yameharibiwa kwenye kona ya majengo, na uchafu umetawanyika chini.

Chanzo: BBC Swahili

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
 
My take!

Je, Zelensky anawaza nini mpaka kuamua kuanza kushambulia Urus wakati anajua kabisa Putin alishaonya hataki Urusi ishambuliwe?

Putin na Zelensky fanyeni mazungumzo hatutaki vita vikubwa.

Habari kamili.

Rais wa Ukraine Volodymr Zelensky ameonya kwamba vita vinakuja nchini Urusi baada ya shambulio la mapema la ndege zisizo na rubani kwenye mji mkuu wa Moscow.

Bw Zelensky alisema mashambulizi dhidi ya eneo la Urusi ni "mchakato usioepukika, wa asili na wa haki kabisa" wa vita kati ya nchi hizo mbili.

Wizara ya ulinzi ya Urusi ilisema ndege tatu zisizo na rubani za Ukraine zilidunguliwa siku ya Jumapili, na mbili zilianguka kwenye afisi.

Uwanja wa ndege wa Vnukovo, kusini magharibi katikati mwa jiji, pia ulifungwa kwa muda mfupi.

Meya wa jiji hilo Sergei Sobyanin alisema maeneo ya mbele ya majengo mawili ya ofisi yaliharibiwa kidogo.

Picha kutoka eneo la tukio zinaonyesha kuwa madirisha kadhaa yameharibiwa kwenye kona ya majengo, na uchafu umetawanyika chini.

Chanzo: BBC Swahili

Sent from my Infinix X612 using JamiiForums mobile app
Mtu anapigwa chumbani kwake safi kabisa Zelesky!! hakika ww ni mwanaume wa kweli, kwa Hali ilipofikia ilikuwa hakuna namna maana kama kupigwa Ukraine keshapigwa makombora karibu ya aina yote sidhani kama Kuna silaha ambayo Mrusi hajaitumia Ukraine labda Nuclear tu ni muda muafaka na yy Aanzee kupokea kichapo ndani mwake maana Ukraine haina Cha kupoteza kwasasa.
 
 
Sasa hivyo vidrone viwili vitatu vitabadilisha nini?

Kaipiga BELGOROD tu kidogo kwa kutumia mamluki wa Kirusi, Leo hii watu wapo kwenye mipango ya kuipiga Kharkov.

Mwambieni aache kutumia bwimbwi
Moscow kimewaka leo, Ukraine alikuwa anatumia ujumbe kwamba hata Moscow tuna uwezo wa kufika ila Leo Amir jeshi mkuu ametangaza rasmi kwamba wataishambulia Moscow rasmi kwahiyo tarajieni yasiyotarajiwa.
 
Sasa hivyo vidrone viwili vitatu vitabadilisha nini?

Kaipiga BELGOROD tu kidogo kwa kutumia mamluki wa Kirusi, Leo hii watu wapo kwenye mipango ya kuipiga Kharkov.

Mwambieni aache kutumia bwimbwi
Binaadam hata ukimpatia ukampiga kwa manati unammaliza, so usidharau 'vidrone viwili vitatu'.
Russia ni Guvu nyingi maarifa hakuna, ndiyo maana yupo busy akipigana na Majengo. Wakati mwenzake anafanya tallying ya askari na vifaa vya Russia anavyoangamiza.
Ndiyo maana Russiaa akitoa update ya mashambulizi yake huwa anaonyesha majengo na vifusi alivyobomoa, wakati Ukraine akitoa update huwa anaonyeshaa askari waa Russia alio waua, na vifaa na silaha alivyo viteketeza.
Umeona tofauti hapo?
 
Sasa hivyo vidrone viwili vitatu vitabadilisha nini?

Kaipiga BELGOROD tu kidogo kwa kutumia mamluki wa Kirusi, Leo hii watu wapo kwenye mipango ya kuipiga Kharkov.

Mwambieni aache kutumia bwimbwi
Pamoja na hayo nimetokea kumkubali sana Zalensky, anakomaa mwanzo mwisho. Vita ikiisha na nchi ikawa salama, huyu jamaa ajengewe sanamu kubwa km shujaa.
 
Ukraine hana cha kupoteza. Unaanzisha vita wakati nyumba yako ya vyioo
Kabisa jamaa hawana Cha kupoteza maana kama kupigwa wamepigwa vya kutosha na Kila aina ya silaha ya Mrusi ulikuwa ni ujinga wa kiwango Cha juu sana kujilinda bila kushambulia ndani ya Urusi.
 
Huyo Zelenesk ni comedian anapiga vigorofa viwilu vitatu afu yeye anapondwa mpa kilio wanakisikia Washington
Kumbuka katika zile superpower countries, Urusi yupo.
Kama ameipiga vilivyo na lengo lake ni kuichukua Ukraine. Mbona mpk sasa bado?
Wangekuwa wale Islamic state, sasa hivi wangekuwa wanajilipua kwa mabomu Urusi. Jamaa anavaa mabomu, anaenda kujilipua kwenye makundi ya watu
 
Sasa hivyo vidrone viwili vitatu vitabadilisha nini?

Kaipiga BELGOROD tu kidogo kwa kutumia mamluki wa Kirusi, Leo hii watu wapo kwenye mipango ya kuipiga Kharkov.

Mwambieni aache kutumia bwimbwi
Zele Ana viwanda.
200 vya kutengeneza drones!
Utashuhudia maajabu ya Vita vya drones!
 
Mtu anapigwa chumbani kwake safi kabisa Zelesky!! hakika ww ni mwanaume wa kweli, kwa Hali ilipofikia ilikuwa hakuna namna maana kama kupigwa Ukraine keshapigwa makombora karibu ya aina yote sidhani kama Kuna silaha ambayo Mrusi haijaitumia Ukraine labda Nuclear tu ni muda muafaka na yy Aanzee kupokea kichapo ndani mwake maana Ukraine haina Cha kupoteza kwasasa.
Ule msafara wa 64km sijui ulipotelea wapi.

Wakapeleka Hostomel Airport Paratropers hadi karibu na Kyiv kwa umbali wa 10km ila waliuliwa wote


Eti leo Urusi anapigwa kwake na drone Beaver ambayo development haijakamilika kisawa sawa.

Hii vita ikienda hadi mwakani nina uhakika itakuwa piga nikupige
 
Back
Top Bottom