GE2025 ZEC yawasihi waandishi wa habari kuepuka lugha za chuki wakati wa kampeni

GE2025 ZEC yawasihi waandishi wa habari kuepuka lugha za chuki wakati wa kampeni

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

tonicimmobility

JF-Expert Member
Joined
Jun 17, 2025
Posts
493
Reaction score
1,038
Vyombo vya habari na waandishi wa habari wameshauriwa kuepuka kutumia lugha za chuki, uchochezi au zinazoweza kugawa jamii kwa misingi ya ukabila, dini au itikadi katika kipindi hiki cha kuelekea kampeni za uchaguzi.

SnapInsta.to_545282004_1326691022147239_8781104926640816702_n.jpg
Soma pia: ZEC: Vyama Visivyosaini Maadili ya Uchaguzi Havitaruhusiwa Kufanya Kampeni

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), Jaji George Joseph Kazi, alitoa wito huo wakati akifungua mafunzo ya siku moja kwa wahariri wa vyombo vya habari, waandishi, wapiga picha pamoja na wachukuaji wa maudhui ya mitandao ya kijamii yaliyofanyika katika ofisi za tume hiyo, Maisara.

Amesisitiza kuwa katika kipindi cha uchaguzi taarifa za upotoshaji zinaweza kusababisha madhara makubwa kwa jamii, hivyo waandishi wanapaswa kuhakikisha wanathibitisha ukweli wa taarifa zote kabla ya kuzipa nafasi kwenye vyombo vya habari au mitandaoni.
 
Back
Top Bottom