GE2025 ZEC kutumia bilioni 12 katika shughuli zote za Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025, Vyama 17 Kushiriki

GE2025 ZEC kutumia bilioni 12 katika shughuli zote za Uchaguzi Mkuu Oktoba 2025, Vyama 17 Kushiriki

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Richer

JF-Expert Member
Joined
Jun 9, 2025
Posts
1,446
Reaction score
2,093
Licha ya ratiba ya uchukuaji wa fomu za uteuzi wa nafasi za urais, uwakilishi na madiwani kuanza leo, lakini kwa nafasi ya urais vyama vya siasa vimeandika barua za kuomba kuchukua fomu kuanzia Agosti 30, 2025.

Wakati mchakato huo ukiendelea, Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), inatarajia kutumia Sh12 bilioni katika shughuli zote za Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu

Akizungumza leo Agosti 28, 2025 Mkurugenzi wa Uchaguzi Zanzibar, Thabit Idarous Faina amesema dimba la uchukuaji fomu litafunguliwa na Chama cha Mapinduzi (CCM) ambacho mtiania wake wa urais atachukua fomu Agosti 30, saa 4: 00 asubuhi katika ofisi za Tume hiyo

1756387080232.png

Siku hiyohiyo pia Chama cha National League for Democracy (NLD) kitachukua fomu saa 5:00 asubuhi, Chama cha Alliance for African Farmers Party (AAFP) kitachukua fomu saa 6:00 mchana na Chama cha Wananchi (CUF) kitachukua fomu saa 7:00 mchana na saa 8:00 mchana kitachukua Chama cha Tanzania Labour Party (TLP) huku saa 9:00 alasiri watafunga siku hiyo kwa kutoa fomu kwa chama cha NRA

Kwa mujibu wa Faina, Agosti 31, 2025 wataanza na chama cha NCCR Mageuzi saa 3:00 asubuhi, saa 4:00 asubuhi itakuwa ni Chama cha ACT Wazalendo huku saa 5:00 asubuhi watakuwa na chama cha Kijamii CCK, kikifuatiwa na Chama cha DP ambacho kitachukua fomu saa 6:00 mchana

Amesema katika uchukuaji wa fomu lazima mwombaji apate namba maalumu ya malipo (control number) kwa ajili ya kulipia na tayari vyama vyote 17 vimeshachukua namba ya malipo kwa ajili ya fomu hizo

Chanzo: Mwananchi_official
 
Back
Top Bottom