Zawadi nono - iphone 5

Zawadi nono - iphone 5

Charles Mkubya

JF-Expert Member
Joined
Aug 27, 2009
Posts
206
Reaction score
161
Ndugu zangu wana JF, nimewiwa kuwashirikisha katika hili nikiamini naweza pata msaada toka kwa members wa JF. Nimeibiwa simu yangu jumanne ilopita (18 Feb 2014) eneo moja maarufu kwa jina la darajani kuelekea mataa ya chang'ombe mida ya saa moja jioni. Simu iloibiwa ni IPHONE 5 nyeusi na bahati nzuri nilifanikiwa kuwasiliana na APPLE, na kwa sasa iko kwenye Lost Mode hivyo itamuia vigumu mtu yoyote kuitumia kwa namna yoyote ile achilia mbali kuifanyia flashing. Mara ya mwisho imeonekana usiku wa tukio maeneo ya KEKO mtaa wa mapinduzi. Kwa yeyote atakaefanikiwa kuipata kwa namna yeyote ile kuna zawadi ya laki moja taslimu (100,000) sababu najua alieiba atahitaji kuiuza kwa watu au ameshaiuza kwa mtu na anaweza kuwa member wa JF. Ukiiwasha tu utakutana na ujumbe wangu na number yangu ya simu jinsi ya kunipata. Sitohitaji kujua nani kaiba au nani kamuuzia nani na hii itakuwa baina yangu na huyo atakaefanikiwa kunirejeshea. Number yangu ya simu ni 0785690479, natanguliza shukrani zangu kwa JF members nikiwa na imani kuna siku nitatoa mrejesho wa mafanikio, Asanteni sana.

Charles Mkubya.
 
Sijui kama naruhusiwa kutoa pole, Ok Pole sana ndugu yangu. Naamini utaipata tu, kwasasa naamini iko kwa mafundi wa kibongo wakiamini wataweza kuiflash.....utaipata tu. Amini hivyo
 
Sijui kama naruhusiwa kutoa pole, Ok Pole sana ndugu yangu. Naamini utaipata tu, kwasasa naamini iko kwa mafundi wa kibongo wakiamini wataweza kuiflash.....utaipata tu. Amini hivyo

Asante sana Elli. Naamini hivyo
 
Sijui kama naruhusiwa kutoa pole, Ok Pole sana ndugu yangu. Naamini utaipata tu, kwasasa naamini iko kwa mafundi wa kibongo wakiamini wataweza kuiflash.....utaipata tu. Amini hivyo

Mkuu, ile simu niliipata. Asante kwa kunipa moyo, kuna uzi nimeweka wenye heading umewahi kuibiwa iphone 5! Nikaona unaweza usione bora nikupa mrejesho. Thanx.
 
ooohhh hongera sana unawesa kuntueleza uliipataje? ili tujifunze pia
Mkuu, ile simu niliipata. Asante kwa kunipa moyo, kuna uzi nimeweka wenye heading umewahi kuibiwa iphone 5! Nikaona unaweza usione bora nikupa mrejesho. Thanx.
 
Ndugu zangu wana JF, nimewiwa kuwashirikisha katika hili nikiamini naweza pata msaada toka kwa members wa JF. Nimeibiwa simu yangu jumanne ilopita (18 Feb 2014) eneo moja maarufu kwa jina la darajani kuelekea mataa ya chang'ombe mida ya saa moja jioni. Simu iloibiwa ni IPHONE 5 nyeusi na bahati nzuri nilifanikiwa kuwasiliana na APPLE, na kwa sasa iko kwenye Lost Mode hivyo itamuia vigumu mtu yoyote kuitumia kwa namna yoyote ile achilia mbali kuifanyia flashing. Mara ya mwisho imeonekana usiku wa tukio maeneo ya KEKO mtaa wa mapinduzi. Kwa yeyote atakaefanikiwa kuipata kwa namna yeyote ile kuna zawadi ya laki moja taslimu (100,000) sababu najua alieiba atahitaji kuiuza kwa watu au ameshaiuza kwa mtu na anaweza kuwa member wa JF. Ukiiwasha tu utakutana na ujumbe wangu na number yangu ya simu jinsi ya kunipata. Sitohitaji kujua nani kaiba au nani kamuuzia nani na hii itakuwa baina yangu na huyo atakaefanikiwa kunirejeshea. Number yangu ya simu ni 0785690479, natanguliza shukrani zangu kwa JF members nikiwa na imani kuna siku nitatoa mrejesho wa mafanikio, Asanteni sana.

Charles Mkubya.


Hi hi hao apple una wasiliana nao vipi?
 


Mkuu,
Shukrani kwa kilisha nyuma(feedback) japokuwa sijauona huo Uzi wako mwingine.
 
Tupe maarifa ya kuwasiliana na apple mkuu maana hatuwezi jua yanaweza kutufika na kwenye ki-apple changu!!
 
Tupe maarifa ya kuwasiliana na apple mkuu maana hatuwezi jua yanaweza kutufika na kwenye ki-apple changu!!

Kijome, ni kupitia icloud. Katika simu yako kuna account ya icloud, ingia sign up, then kuna kitu kimeandikwa find my phone, iweke on/active hiyo option. Kama ukiibiwa unaingia ktk computer au simu yoyote, unaingia icloud kwa details zako, utakuta options nyingi ikiwa ni pamoja na kui-lock simu/lost mode au pia kama unavitu muhimu sana waweza kufuta kila kitu kilichomo ingawa kwa hii option hutakua na uwezo wa kuiona popote inapowashwa. Unapoifunga kuna option ya kuandika ujumbe unaotaka ikiwa ni pamoja na kusema simu imeibiwa ikipatikana na yeyote akutafute vipi. Naweza nisiwe muelezaji mzuri lakini ukiingia google search icloud, maswali yako yote yatapata majibu pale.
 
nokia, samsung na wengine wana hizo facilities?
 
Back
Top Bottom