nngu007
JF-Expert Member
- Aug 2, 2010
- 15,862
- 5,797
na Mauwa Mohammed, Zanzibar
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeanzisha mpango wa utoaji wa gesi ya kupikia bure kwa wananchi kama moja ya hatua za kudhibititi ukataji wa miti katika maeneo yote nchini hapa.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Kilimo na Maliasili, Mansoor Yussuf Himidi, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Darajani Mjini Zanzibar kuhusu maadhimisho ya siku ya upandaji miti.
Alisema jukumu la usimamizi wa rasilimali za misitu ni la wananchi wenyewe hivyo amewataka kuendeleza tabia ya kuitunza.
Mansoor alisema mwaka huu 2011 wizara hiyo imeandaa upandaji miti kitaifa katika eneo la Bumbwini Mafufuni, Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kusini Unguja.
Alibainisha kuwa jumla ya hekta 959 hukatwa kwa mwaka lakini zinazopandwa ni hekta 450 kwa mwaka hivyo kuna kila sababu ya wananchi kufahamu juu ya umuhimu wa upandaji wa miti nchini. Alisema upandaji wa miti utafanyika Aprili 16 mwaka huu kwa upandaji wa mikoko na mikandaa ili kuimarisha ikolojia ya misitu nchini hapa. Mradi wa utoaji gesi bure uitwao Hifadhi ya Miti Asili Zanzibar (HIMA) unagharamiwa na serikali ya Norway hapa nchini na utatumia jumla ya sh milioni nne kwa muda wa miaka minne.
SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) imeanzisha mpango wa utoaji wa gesi ya kupikia bure kwa wananchi kama moja ya hatua za kudhibititi ukataji wa miti katika maeneo yote nchini hapa.
Hayo yalielezwa na Waziri wa Kilimo na Maliasili, Mansoor Yussuf Himidi, wakati akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Darajani Mjini Zanzibar kuhusu maadhimisho ya siku ya upandaji miti.
Alisema jukumu la usimamizi wa rasilimali za misitu ni la wananchi wenyewe hivyo amewataka kuendeleza tabia ya kuitunza.
Mansoor alisema mwaka huu 2011 wizara hiyo imeandaa upandaji miti kitaifa katika eneo la Bumbwini Mafufuni, Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kusini Unguja.
Alibainisha kuwa jumla ya hekta 959 hukatwa kwa mwaka lakini zinazopandwa ni hekta 450 kwa mwaka hivyo kuna kila sababu ya wananchi kufahamu juu ya umuhimu wa upandaji wa miti nchini. Alisema upandaji wa miti utafanyika Aprili 16 mwaka huu kwa upandaji wa mikoko na mikandaa ili kuimarisha ikolojia ya misitu nchini hapa. Mradi wa utoaji gesi bure uitwao Hifadhi ya Miti Asili Zanzibar (HIMA) unagharamiwa na serikali ya Norway hapa nchini na utatumia jumla ya sh milioni nne kwa muda wa miaka minne.