Beatrice Kamugisha
JF-Expert Member
- May 18, 2019
- 761
- 6,985
Zanzibar tuliaminishwa watu awapigi mpunga ila nimefuatilia madudu yanayoibuliwa na Rais aliyepo nikabaini binadamu hasa waliosoma wanatumia vyema taaluma zao kufanya ubadhirifu kuliko kuwatumikia wananchi. Baada ya tumbuatumbu kuwa kali wazee wameanza kumlalamikia Rais Mwinyi kwamba anafukua sana makaburi. Nikajiuliza wanapata wapi ujasiri wakusema Rais anafukua makaburi? Je ukiiba regime hii ndo ulindwe na regime unayofuata?
Lakini pia Kama eneo dogo Kama Zanzibar panaweza kuwa uchochoro wakuoba Mali za umma, vipi kuhusu bara?
Lakini pia Kama wazee wa CCM wanaweza kuhoji kwanini Rais anafukua makaburi kila watoto wao wamefutwa kazi au kushushwa vyeo kwanini spirit hii isiwaguse na masikini ambao wakituhumiwa tu jela?
Mhe. Rais ukiacha kufukua makaburi utakuwa umeacha kurejesha Mali za umma zilizoibwa na hivyo kukiuka kiapo chako. Wezi haki yao ni kushtakiwa,kufilisiwa na fedha kurejeshwa kwa umma bila kujali waliiba lini
Lakini pia Kama eneo dogo Kama Zanzibar panaweza kuwa uchochoro wakuoba Mali za umma, vipi kuhusu bara?
Lakini pia Kama wazee wa CCM wanaweza kuhoji kwanini Rais anafukua makaburi kila watoto wao wamefutwa kazi au kushushwa vyeo kwanini spirit hii isiwaguse na masikini ambao wakituhumiwa tu jela?
Mhe. Rais ukiacha kufukua makaburi utakuwa umeacha kurejesha Mali za umma zilizoibwa na hivyo kukiuka kiapo chako. Wezi haki yao ni kushtakiwa,kufilisiwa na fedha kurejeshwa kwa umma bila kujali waliiba lini