Zanzibar sio Nchi! Eti ni nini?

Zanzibar sio Nchi! Eti ni nini?

Angalia nchi nyingine zenye population ndogo - sio kigezo peke hicho. List of countries by population - Wikipedia, the free encyclopedia

Nadhani suali la jawabu yako umejipa mwenyewe kwenye hii orodha uliyoweka hapa, KWANI ZANZIBAR HAIMO hata kwenye mabano angalau tukasema ni sehemu ya Tanzania. Au kama unataka kujiridhisha zaidi angalia hapa nchi za Afrika zinazotambulika: List of sovereign states and dependent territories in Africa - Wikipedia, the free encyclopedia.

Wazanzibari kujidai kuwa wana nchi ni ndoto tu. Kwa nini hamfanyi kama ambavyo wengine wanaota kudaiTanganyika yao?.

Kwa ufupi, wale wenye ndoto za Uzanzibari na Utanganyika ni kuwa wamerogwa, na waliowaroga (Nyerere na Karume) wameshakufa. Kubalini matokeo.
 
Petu Hapa
labda utuambie kipi hujaelewa mwenzetu kwenye hayo majibu ya wadau hapo juu tukusaidie kufafanua mkuu
NB zingatia post ya chigwiye
Ukifuata katiba, Zanzibar sio nchi ila ni sehemu ya jamhuri ya muungano wa Tanzania. Hili sio geni wala la kutugwa - na wala hamna mtu anayepinga hili. Swala la hapa, ni hali halisi inayoendelea - tanganyika imefanikiwa kujivuta na kuwa tanzania bara - na kubebwa na mikoa yake 25, na tunaitwa tanzania bara - mara nyingi Tanzania tu.

Sasa, Tanzania visiwani - ambayo imejulikana zaidi kama zanzibar ama visiwa vya unguja na pemba imeendelea kuwepo na kujitambulisha kama zanzibar. Katiba yetu ya muungano inatambua mikoa mitano, na eneo lote hilo kwa jumla yake tunaita Tanzania visiwani - wengine wakiita mamlaka/ama serikali, yenyewe inataka kutambulika zaidi ya hapo. Sasa hatuwezi kulazimisha tu, kwamba katiba iliandikwa basi ndio iwe. Tunaongelea uhalisi na historia, ambayo zanzibar inadai yenyewe lingekuwa taifa, na huu muungano unawakandamiza kwa namna tofauti.

swala langu, sasa hii zanzibar - yenye mikoa mitano - ni kisiwa, malaka tu, ama serikali tu?
 
Unajua Zanzibar kuwa au kutokuwa nchi inategemea wewe binafsi unatafsiri neno "nchi" katika context gani. Kama ukitafsiri neno nchi katika context ya kisiasa kwa kanuni za Umoja wa Mataifa, basi Zanzibar si nchi. Kama ukitafsiri neno nchi kwa mintilafu ya kimsaafu kama Biblia na Kurani, basi Zanzibar ni nchi, maana Mwenyezi Mungu aliumba mbingu na nchi - na nchi haikuwa na mipaka. Na pia kama unataka kutafsiri nchi katika misingi ya Katiba ya JMT basi si Zanzibari wala Tanganyika zilizo nchi. Na pia kama unataka kuangalia mambo katika context ya kiu-Zanzibari na Kiu-Zanzibara basi Zanzibar ni nchi. Sasa chaguo ni lako na sisi wenye akili hatuhitaji kubishana na wewe juu ya hili!
 
Unajua Zanzibar kuwa au kutokuwa nchi inategemea wewe binafsi unatafsiri neno "nchi" katika context gani. Kama ukitafsiri neno nchi katika context ya kisiasa kwa kanuni za Umoja wa Mataifa, basi Zanzibar si nchi. Kama ukitafsiri neno nchi kwa mintilafu ya kimsaafu kama Biblia na Kurani, basi Zanzibar ni nchi, maana Mwenyezi Mungu aliumba mbingu na nchi - na nchi haikuwa na mipaka. Na pia kama unataka kutafsiri nchi katika misingi ya Katiba ya JMT basi si Zanzibari wala Tanganyika zilizo nchi. Na pia kama unataka kuangalia mambo katika context ya kiu-Zanzibari na Kiu-Zanzibara basi Zanzibar ni nchi. Sasa chaguo ni lako na sisi wenye akili hatuhitaji kubishana na wewe juu ya hili!

Hayo ndio maneno!

sijazoea kuongea na wakubwa na wataalamu wanojua sheria tu. Majibu yao wao huwa yamepagwa na ushahidi wa kutosha kusema lile walikusidiao wao. Watarudi vipengele fulani fulani katika maandiko ya kale basi kusema tu kwamba walichosema ni sahihi. Napenda kuangalia uhalisia wa sasa na kusikiliza tafsiri zilivyo katika uhalisia wake. Majibu yako matatu katika tafsiri ya nchi yote ni sahihi - na ndivyo nimekuwa nionavyo mimi!

sasa, swala je, tafsiri hizo zinaweza ishi kwa wakati mmoja, na kukubali nguvu zake jinsi zilivyo? Pale katiba inapokuwa juu ya uzanzibari na dini, wazanzibari waridhie ama?
 
zanzibar ni kisiwa cha utalii

Ha ha ha ha ha! Utalii wenyewe wa Zanzibar uko wapi? Watalii wenyewe wanaungaunga kutoka Bara. Muungano ukifa na utalii wasahau - hiyo ndio habari japo chungu masikioni. Sana sana hilo ni shamba la karafuu tu.
 
Kama Zanzibar ni Nchi,basi na Mafia nayo ni nchi....lakini kama Mafia ni wilaya,basi Zanzibar nayo ni wilaya.
 
Zanzibar ni sehemu ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania ambayo ina mamlaka ya kujiamulia mambo yake ya ndani kama uvuvi, kilimo, maji ya kunywa nk! Hivyo kimataifa Zanzibar haina mamlaka wala haki ya kijiwakilisha. Zanzibar haiwezi kuwa na jeshi lake la ulinzi vinginevyo itahesabiwa imeasi na adhabu ya muasi inafahamika. Rais wa Zanzibar hawezi kuwa amiri jeshi wa majeshi ya ulinzi na usalama.

Ni amri jeshi mkuu wa KMKM, Valentia na mafunzo. Ina maana hujui hilo.

 

Nafikiri watu inabidi wafikiri nje ya box. Kwani kwa aneijua katiba kila kitu kimebainishwa kuwa Mkoa ni nini na mkuu wake, Wilaya, kata tarafa na hata kijiji na kitongoji au mtaa.

Kwa mantiki hiyo kwa Issue ya Znz ilitakiwa iliseme hilo. Kama iliweza kusema kuhusu mkoa, wilaya, kata,tarafa, kijiji n.k kwanini Znz isitajwe.

Kwa mantiki yoyote kama imebainisha ni sehemu ya Jamhuru a muungano wa Tanzania. Basi kuwa sehemu ina maana ni kama kitu kamili kwa maana nyengine ni Nchi.

Hilo sifikirii kama mtu anaweza kupinga na kwa kutumia kigezo hicho ndipo Katiba ya Znz ikabainisha wazi katika ibara ya 3 na 4 kuwa ni nchi yenye mamlaka kamili na kuweka mipaka yake kama nchi.

jamani acheni kufikiria karibu kuweni wawazi na kufikiri nje ya box.
 
Muungano tunaweza kuuongelea kwa hisia tofauti na tukasema yote tunayotaka kusema. Lakini sasa naona kuna haya maneno maneno ya kusema Zanzibar si nchi. Je hii dhana ni sahihi ? kutoka kipengele kipi cha katiba? Ama ni kwa hisia hisia zetu tu? Iwapo ni hisia tu, ni haki kweli kuvua utambulisho wa eneo kikejeli kejeli kweli. Na kama sio nchi, Zanzibar ni nini sasa? Mkoa? wilaya ama ni kitu gani?
Kwa nini kung'ang'ania kujua kama Zanzibar ni nchi au kitu kingine? Ni vizuri kuainisha faida na hasara za muungano ulioipelekea Tanganyika kupoteza uhalali wake na Zanzibar kubakia kujidai na kutafuta makuu zaidi.
 
Itambulike Serikali ya zanzibar ni serikali - na wala sio kwa kejeli wala kufanya mzaha - Zanzibar inahistoria yake - sio ya kimkoa wala wilaya. Hakuna wilaya yoyote ama mkoa uliofanya kikao cha muungano ili wajiite tanganyika. historia yetu na mipaka yetu ya kikoloni ndio imejenga utanganyika, na historia hiyo ndio inayoitofautisha zanzibar - na kujenga muungano. Hatuwezi kudharau vitu hivi, kirahisi rahisi tu. Kufunika funika tu kwa kuwa tunapenda muungano.

Ndani ya katiba yetu, tunatambua kabisa zanzibar sio mkoa wala wilaya - kwa ukosefu wa maneno ama uoga wa kujitawala tumeita Tanzania Zanzibar - na ikasemwa kwamba Rais atashauriana kwanza na "Rais wa Zanzibar kabla ya kuigawa Tanzania Zanzibar katika Mikoa, Wilaya au maeneo mengineyo" katiba. Kwahiyo, zanzibar yenyewe sio mkoa wala wilaya !
 
Kwa nini kung'ang'ania kujua kama Zanzibar ni nchi au kitu kingine? Ni vizuri kuainisha faida na hasara za muungano ulioipelekea Tanganyika kupoteza uhalali wake na Zanzibar kubakia kujidai na kutafuta makuu zaidi.

yaani hii ndio ile wanaita "kurudia imani yako". Unaijua lakiini inapaswa uiseme tena ili usisahau - ukumbuke! Swala hilo nimekuwa nawauliza watu naokutana nao - wanaoutaka muungano, wasioutaka, ama ata wale ambao hauwasumbui wala kujali. Majibu yanakuwa magumu sana! Umoja wa Afrika! Usalama! Uchumi! Geographia! ....
 
Acha hizo wewe, ni kiuchochoro cha wala urojo tu.
 
Tuvunje muungano wadau mnasemaje? Halafu tutapata majibu ya doubt zetu zote ..tanganyika oyeeeeeeeeeee
jibu zanzibari ni kisiwa cha marashi ya karafuu suala la zanzibar nchi au sio nchi logically ni contradiction sasa ili kuondoa hiyo contradiction na tupate tautology tuvunje mungano tu ...mtajua kama ilikuwa nchi au sio nchi
nawasilisha
 
CUF ndio wanaiharibu zanzibar Jusa juzi anaongelea mambo ya bahari wakati wazanzibar wana mgao wa umeme kila siku lakini haongelea ambao unawathiri watoto wa shule,wafanyabiashara
 
Back
Top Bottom