Zanzibar safi!

Zanzibar safi!

Siri ya sifuri

JF-Expert Member
Joined
Sep 21, 2018
Posts
2,580
Reaction score
2,224
Habari wakuu?

Katika harakati zangu zakutafuta maisha bora nikatua zangu mjini Zanzibar nikitokea mkoani Tanga, wilaya ya Pangani Magharibi, Mtaa wa Kongowea. Kyle Zanzibar makazi yangu yakawa mtaa wa Shaurimoyo mkabala na shule ya msingi, Katika kutafuta marafiki ndio nikakutana na wakazi wengi wa mkoa wa Tanga kutoka wilaya tofauti, nanilichofaham baadae ni kwamba, wenyeji wengi wa mkoa wa Tanga wanaoishi Zanzibar ni mafundi ujenzi. kuna waliohamia kabisa na kuna wanaokwenda kufanyakazi na kurudi, niseme ni kambi.

Nilikua na kawaida ikitokea MTU wa Tanga amkuwa na shughuli kama harusi au msiba naenda kujumuika nae, kuna utaratibu ulionivutia kwenye harusi nao ni huu"Mkienda kuposa huwa mnaandaliwa CHAKULA cha wote ila bwana harusi anaandaliwa cha kwake peke yake, anawekewa samaki kwenye kisahani, wakati wote wa mlo huwa ndugu wa mke au baba mkwe wake kama yupo wanamfuatilia jinsi anavyomla yule Samaki, wajua kwanini!?

Hawataki amgeuze, wanachotaka wao kuona ukimaliza upande mmoja unaondoa mwiba ambao ndio uti wa mgongo wa samaki unaotenganisha upande mmoja na mwingine kisha ndio umalizie kula upande wa pili, ikitokea umemgeuza basi itakua ndio umejinyima mke wewe mwenyewe, wanasema huna maadili hufai hata kidogo kumuoa binti yao, eti utaenda kumgeuza" utamlakotekote"basi hata kama ulikuja kutoa mahari utarudi nayo, hawaipokei na ikitokea umeoa mke thamani zote ndani yanyumba ni Mali ya Mwanamke, siku mkiachana anabeba kila kitu anaacha nyumba nyeupe, kwa maana kwamba mwengine utakae kwenda kumuoa atakuja navyake, na ikitokea umekamatiwa na binti"msichana"basi kutawekwa mkataba mahakamani na hutaweza kumuacha chini yakipindi cha miaka 5 na ukikaidi unakamatwa na kufungwa.

Hiyo ndiyo Zanzibar bwana
 
Gazeti halina vituo na uongo mtupu hii znz ya kwenu labda
Kwa mwanamke anatakiwa kua na kila kitu mfano kabati,viombo n.k kabla hajaolewa au akichumbiwa ndo lazima awe navyo akaanzie maisha

Huko kula samaki sikajawahi ona

Na mahakama sijawahi ona nachpjua ukikamwatwa ni ndoa ya mkeka hapohapo jspo hyo mambo yamepungua siku hizi

Kwanza unguja kumeharibika skuhizi kama bara tu

Hii kamba uliotaka tufunga imekatika
 
Goddess, hivyo anavyokuanavyo akiolewa na avyonunua au anavyonunuliwa akiwa kwenye ndoa akiachika anaviwacha?hiyo moja, pili ukikamatiwa na kufungishwa ndoa ya mkeka unaweza kumuacha muda wowote? Naomba muongozo maana nilichoandika ninauhakika nacho, na kuna mahakama ya Kadhi inayotambuliwa na Serikali unayoshgulikia masuala ya Ndoa na mirathi unalijua hilo?
 
hivyo anavyokuanavyo akiolewa na avyonunua au anavyonunuliwa akiwa kwenye ndoa akiachika anaviwacha?hiyo moja, pili ukikamatiwa na kufungishwa ndoa ya mkeka unaweza kumuacha muda wowote? Naomba muongozo maana nilichoandika ninauhakika nacho, na kuna mahakama ya Kadhi inayotambuliwa na Serikali unayoshgulikia masuala ya Ndoa na mirathi unalijua hilo?
Naona tutachanganyana tu mzee mm niwa kusini paje, bwejuu hayo makorokoro yote hakuna huku sjui unaongelea fasi uliopo ww
 
Naona tutachanganyana tu mzee mm niwa kusini paje, bwejuu hayo makorokoro yote hakuna huku sjui unaongelea fasi uliopo ww
Tuanzie,Kinyasini,Paje, Bwejuu,Kiwengwa,Pwani mchangani, Turudi Mahonda,Donge,Mkokotoni kote huko utamaduni wao unafanana labda tu uniambie hivi sasa hawatilii maanani na kwamba Zanzibar ya Leo sio ya Jana hapo ntakuelewa.
 
Naona tutachanganyana tu mzee mm niwa kusini paje, bwejuu hayo makorokoro yote hakuna huku sjui unaongelea fasi uliopo ww
Ila huko unapoishi wewe Paje,Bwejuu na miji mingi ilyopo pembezoni mwa bahari inawezekana kubadilika kwasababu imevamiwa na Wabara, Makahaba wengi sana hivi sasa, show za week-end kwenye mahoteli zimeharibu jamii, kuna siku niliwasikia wazee Paje msikitini wanalalamika kwamba, watoto wao wanaenda kujiuza Jambiani.
 
Mm sikua naongelea ya jana no ya leo hio
Hata avater yako unaonekana wa Leo, vipi hapo Kinazi upepo, night club, na hiyo hoteli nyingine ya pembezoni show zinaendelea!? Maana nakumbuka mziki wa Maana ulikua unapigwa kila Alhamisi au j5 kama sikosei, na Vipi Mzee Raza anaendelea kufuga ngamia hapo Paje?
 
Back
Top Bottom