Jumakidogo
R I P
- Jul 16, 2009
- 1,851
- 417
Kumekuwa na dalili za kuendelea ama kutokea machafuko makubwa zaidi upande wa pili wa nchi yaani Tanzania visiwani, imefikia hatua nyumba za ibada kuchomwa moto na wageni hasa wanaotoka upande wa bara kutishiwa kutimuliwa. Hizi ni dalili tosha kuwa wenzetu hawautaki muungano. Mpaka sasa najiuliza faida ya aina hii ya muungano ni nini? Kwa nini tunalazimisha muungano huu usio tija? Kabla ya muungano Zanzibar walikuwa nani? Viongozi wetu wana maslahi gani kwa aina hii ya muungano ambao unaelekea kuwa na dalili zote za umwagaji wa damu? Kwa vyovyote vile, nchi moja ambao watu wake wanaamini kuwa nchi ya ni ya kidini haiwezi kuwa na muungano wa kweli na chi isiyo ya kidini. Nadhani imefikia wakati sasa Wazanzibar waachiwe nchi yao kama wanavyotaka. Wahenga wanasema; 'mdai chake hupewa!'