Zamu ya Mangula imefika

Zamu ya Mangula imefika

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,140
Reaction score
18,004
Zamu ya kuahidi halafu kupoteza ushahidi.Kuahidi kupambana na rushwa ndani ya CCM yetu halafu kuishia kupongeza wagombea watakaopita kwa rushwa. Zamu ya kuwainua mikono juu wagombea watakaopenya kwa mlungula huku wakipigiwa chapuo ya kushika nyadhifa tamutamu nchini.

Imefika zamu yake. Zamu rasmi ya Comrade Phillip Mangula, Makamu wa Mwenyekiti wa CCM Taifa. Mangula ameahidi rasmi kuwa atakula sahani moja na watoa na wapokea rushwa ndani ya CCM hasa wakati wa kura za maoni. Kura za maoni ya Urais, Ubunge na Udiwani. Ni hapo mwakani. Mwaka wa uchaguzi mkuu nchini.

Wagombea watarajiwa wameshajindaa. Wamekusanya mamilioni yao kwenye sandarusi kuingia kwenye mchakato wa kura za maoni na uchaguzi mkuu wenyewe. Wako tayari kuuza nyumba, magari, mashamba na rasilimali zao nyingine kupata mamilioni ya uchaguzi. Tayari kushindana na kushinda.Tayari kufa au kupona.

Comrade Mangula ametangaza wakati mzuri. Wakati ambao maandalizi yanafikia ukingoni ili mechi ianze. Wakati ambao mbinu mbivu na mbovu zitatumika kupatikana kwa ushindi chamani na uchaguzini. Waliomtangulia Mangula katika kauli kama yake walishindwa kuisimamia na kupata ushindi kwa kauli na matendo yao.Kuvua gamba kukapotelea gizani.

Comrade Mangula ataweza kukomesha rushwa ndani ya CCM uchaguzini? Tusubiri tuone na kusikia!


Mzee Tupatupa wa Lumumba, Dar es Salaam
 
Huyo mzee msanii sana, kazi kuyatishia nyau maccm menzie.

Vipi miezi 6 ya maccm walarushwa haijafika?

Vipi siku90 za kujivua gamba hazijafika?

Maccm kwa ma kamati, eti kamati ya maadili...

Mzee mwenyewe hana maadili atamuajibisha nani?
 
ccm huwezi kuwatengamisha na rushwa
 
Kilichosalama ccm ni bendera tu wanachama, washika hatamu wote hoi kwa rushwa, ufisadi, uroho,nk
 
NAONGEA NA WEWE MJOMBA.
Mjomba kila siku unahutubia wazee wa Dar es salaam hivi lini utaandaa mkutano na vijana wa Dar es salaam au mjomba hautuamini. Tatizo la wazee wanakushangilia chochote utakachosema ila unge tuhutubia sisi vijana.

nadhan ungejiandaa vema zaidi ya ufanyavyo sasa. Jana nilikusikia shilingiyetu uliita pesa ya madafu wazee walishangilia, dosari zipo wizara ya nishati we ukamfukuza kazi yule wa.

wizara ya ardhi bado walishangilia sana, ulisema ni kweli kodi ya bilion 21.6 haikukatwa kwenye malipo ya IPTL hukusema nini kifanyike bado walishangilia, ulisema asilimia 70 ya hisa.

za MECMA ziliuzwa kwa PAYPERLINK baada ya kufilisiwa..tena STANDARD CHARTERED BANK walilinunua deni hilo then PAYPERLINK waliziuza hisa b kwa kampuni ya PAP kinyemela bila kujali zuio toka mahakama ya malkia hapo hata mzee ambaye hata.

hakuelewa naye alishangilia, mjomba kuna wakati unaogopa lawama wakati tumekupa sisi dhamana..
Mjomba hii tabia ikiendelea hakika hiki Chama kitakufia mikononi. Nakumbuka usemi wako akili za kuambiwa changanya na zako

#2015 #sio#mbali!
 
Makamba alisema ndani ya CCM kila mtu alitoa rushwa tofauti ni viwango tu, ukiongelea rushwa CCM hakuna atakae pona labda Mangula mwenyewe.
 
Mimi kazi yangu this time ni udalali tu, Muda si mrefu viwanja vya pinda Kigamboni vinaingia sokoni.

Miguu arobaini kwa ishirini milioni tatu.
 
!.... Ccm Rushwa Ni Mahala Pake, Kamwe Huwezi Tenganisha Hivi Vitu Viwili
 
VUTA-NKUVUTE, Wewe mzee tupatupa ni hatari kama si hatari, unaona mbali sana, unakijua chama chako vizuri sana, yaliyo mpata mzee Mangura wote tumeona, lazima wakutafute. you are a leader, a manager and visionary kwa nini wasikutafute uwasaidie
 
We mzee tupatupa ni hatare kama si hatari, unaona mbali sana, unakijua chama chako vizuri sana, yaliyo mpata mzee Mangura wote tumeona, lazima wakutafute. you are a leader, a manager and visionar kwa nini wasikutafute uwasaidie
Mimi siishi Tanzania, ila naishi hapa old Europe kwa miaka mingi sasa tayari nina wajukuu hapa ila napenda sana makala zako na post zako ningependa sana tuongee, sababu pia unaandika kiswahili cha misamiati mizuri, napenda watoto wangu na wajukuu zangu wajue kiswahili, bado nawafundisha kwa kutumia vitabu vya Bulicheka, kama wimbo wa kisichana chini ya mti alisuka kitunga, na Maganga hodari kavuka ziwa nyasa, lakini wewe nakuona upo vizuri sana kwenye kiswahili na misamiati yake.pia muda mwingine natumia vitabu vya mzee mmoja pale chuo kikuu yule mwingereza aliye amua kuwa mbongo makengeza jina kama hilo yupo kitivo cha lugha. ningeomba ni beep tuongee bado nitaweka jina lako anoniem.
 
We mzee tupatupa ni hatare kama si hatari, unaona mbali sana, unakijua chama chako vizuri sana, yaliyo mpata mzee Mangura wote tumeona, lazima wakutafute. you are a leader, a manager and visionar kwa nini wasikutafute uwasaidie
Oke anaitwa mzee Mabara. Namjua sana sababu alifanya kazi na shemeji yangu ambaye sasa yupo nje ya nchi.Niliishi hapo nilisoma hapo kabla sijahamia ugaibuni miaka hiyo.
 
Back
Top Bottom