Zamani ilikuwa raha

Zamani ilikuwa raha

nzalendo

JF-Expert Member
Joined
May 26, 2009
Posts
12,682
Reaction score
14,067
Kwenda sekondari ilikuwa ni heshima kwa jamii inayokuzunguka. Wakati wa kwenda shule husindikizwa na kundi la watu huku umesaidiwa sanduku. Tulipanda treni.

Tiketi tulitunza kwani nauli tulirejeshewa baada ya safari. Makonda wa treni (tt) walikuwa ni wahindi.

Mwl.alipohamishwa shule ilipikwa pilau, pia mashairi yaliimbwa.

Picha tulipiga studio tena baada ya kusevu kwa muda mrefu.... Tofauti na siku hizi ''selfie''.

Tulisikiliza RTD, kwa miziki idhaa ya biashara.

Range rover haikuruhusiwa ku paki benki. Peugeot 504 iliaminika ni gari ya wahuni/majambazi.
Namba za serikali ilikuwa stb, stc, std, stg. Za wahisani ilikuwa tx - plate number nyekundu.

Sikukuu ya saba saba ilifana sana kitaifa ilifanyika. Na mikoa mingine ilishiriki pia.

Vitabu madaftari shule za msingi ilikuwa bure. Daftari likijaa unapeleka kwa mwl.wa darasa anakupa jipya
ole wako karatasi zikutwe pungufu, viboko vilitawala mashuleni na nidhamu ilikuwepo pia.

Wanafunzi shule ya msingi baadhi walikuwa wananyoa ndevu.

Inaendelea hapa
 
-Matibabu ilikuwa bure. Hospitali za binafsi hazikuwepo labda za misheni.
-Ukivaa chupi ilikuwa ni dili kubwa!
-Hakukuwa na skini taiti
-Viatu ilikuwa tunanunua Bora
-Nyumba 10 alikuwa anaheshimika kama hakimu. Ukigombana na mkeo anakwenda kushitaki na kulala kwa mjumbe
-Ukimwi ulikuwa hakuna zaidi ya kisonono na kaswende
-Wasichana wa kazi walikuwa bwerere siku hizi ni shida!
-Hakukuwa na magril kwenye milango na madirisha
-Nyerere alikuwa kama Mungu
-Kawawa alikuwa alionekana kama kichekesho kwa stori za "Kawawa funika kikombe"
-Tulifanywe tuamini kuwa Kambona ni adui wa nchi yetu na nyimbo tuliimba
-Wakati ule wanafunzi kwenda kufanya kazi za mwalimu nyumbani kwake ilikuwa ni heshima kubwa, sasa hivi ni kesi
-Mashairi ya "Karudi baba mmoja" na "Sizitaki mbichi hizi" yalikuwa kichwani kwa kila mwanafunzi
-Jioni zilikuwa ni nyakati za kupiga hadithi na vitendawili au michezo ya kujificha. Siku hizi ni kuangalia TV
Nitaendelea......
 
siku za sikukuu kulikuwa na tamaduni za kupeana chakula hasa pilau, kama mimi ni mkristo na ni krismass lazima pilau ipikwe na niwagawie jirani zangu hasa ambao sio wakristo, na wao vileviile ikifika sikukuu yao wanafanya hivyo hivyo....
 
Zaman wale wa born town kucheki movie Avaron,Empress,New Chox au Drive Inn,wale wapenzi wa movie za kihindi Cameo ndio ilikuwa mpango mzima,kabla ya movie mangoma ya wanyamwezi yalikuwa yanapolomoshwa,wanyamwez kama wakina Billy Ocean,Cool n the Gang wengineo ndio ilikuwa stata kabla ya movie kuanza,da!miaka ile ilikuwa bomba kuwai kutokea katika maisha yangu na nina uhakika kwa wale vijana wa 90s na waliopitia viwanja vile,watakuwa wanamiss kipndi kile,da!kwa bahati mbaya vyote vimekufa.
 
-matibabu ilikuwa bure. Hospitali za binafsi hazikuwepo labda za misheni.
-ukivaa chupi ilikuwa ni dili kubwa!
-hakukuwa na skini taiti
-viatu ilikuwa tunanunua bora
-nyumba 10 alikuwa anaheshimika kama hakimu. Ukigombana na mkeo anakwenda kushitaki na kulala kwa mjumbe
-ukimwi ulikuwa hakuna zaidi ya kisonono na kaswende
-wasichana wa kazi walikuwa bwerere siku hizi ni shida!
-hakukuwa na magril kwenye milango na madirisha
-nyerere alikuwa kama mungu
-kawawa alikuwa alionekana kama kichekesho kwa stori za "kawawa funika kikombe"
-tulifanywe tuamini kuwa kambona ni adui wa nchi yetu na nyimbo tuliimba
-wakati ule wanafunzi kwenda kufanya kazi za mwalimu nyumbani kwake ilikuwa ni heshima kubwa, sasa hivi ni kesi
-mashairi ya "karudi baba mmoja" na "sizitaki mbichi hizi" yalikuwa kichwani kwa kila mwanafunzi
-jioni zilikuwa ni nyakati za kupiga hadithi na vitendawili au michezo ya kujificha. Siku hizi ni kuangalia tv
nitaendelea......
karudi baba mmoja toka safari ya mbali
kavimba yote mapaja na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja ili kumtaka hali
wakata na kauli iwafae maishani
.....................................................
Roho naona yashindwa kifo kibenikabili
.........................................................
Kama mataka mali mtayapata shambani
 
-Zamani ilikuwa mwanafunzi/mtoto ukifanya kosa unaadhibiwa na mtu mzima yeyote na kokote

-ukimwona mwalimu mbali na mzigo unamkimbilia na kumpokea

-hujajaladia daftari ni kosa kubwa...
 
karudi baba mmoja toka safari ya mbali
kavimba yote mapaja na kutetemeka mwili
watoto wake wakaja ili kumtaka hali
wakata na kauli iwafae maishani
.....................................................
Roho naona yashindwa kifo kibenikabili
.........................................................
Kama mataka mali mtayapata shambani

Hahaha...
 
Back
Top Bottom