Sjui ni mimi peke yangu ninayepata shida na aina ya michango ya hawa watoto wa marehemu Mzee Kawawa. Wanaongea vitu vya hovyo sana. Week iliyopita kama mtu-Vita Kawawa alikuwa anasema hakuna shida na deni letu na kuna wakati akalinganisha na level ya madeni ya Marekani na Japan! Leo hii dada mtu anasema kitendo cha Tanzania kualikwa kwenye G8 ni heshma kubwa!
Ukiangalia nchi zinazounda G8 zote zina maslahi Tanzania. Kilichofanyika pale ni uchief-Mangungo na hawa watoto wangejishughulisha kusoma wangejua sio jambo la heshma kama ambavyo wanadai. Nchi kama Brazil, India, South Africa na China etc zimeunda umoja wao- BRICKS, wanaona kabisa G8 sio mahali pao. Kusema tushangilie kuitwa G8 ni sawa na kusema mama ntilie afurahie kuitwa kwenye kikao cha Bakheresa na Mengi! Ni dhahiri huyu mama ntilie atajikita zaidi kuomba na lazima a-trade off something. Sisi tume-trade off nini hawa big boys?