Herbalist Dr MziziMkavu
JF-Expert Member
- Feb 3, 2009
- 42,319
- 33,125
Kampuni la simu za viganjani la Zain inaipiga vita Kampuni ya Simu Tanzania (TTCL) katika mpango wake wa kupanua huduma za simu za mkononi. Tayari makao makuu ya Zain imeiandikia barua Serikali ya Bongo ikiitaka iachane na mipango ya kuisaidia mijihela TTCL ili kuboresha huduma zake, ikiwamo hiyo ya simu za mkononi. heheeee fitnaaaa
TTCL ni kampuni inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania ambayo imeingia ubia na kundi la kampuni za Zain ambapo Serikali inamiliki asilimia 65 wakati Zain ambayo awali ilikuwa Celtel inamiliki asilimia 35.
Kwenye barua hiyo , ilielezwa kuwa Zain hawafurahishwi na hatua ya TTCL ya kuwa na huduma ya simu za mkononi na inatamka wazi kuwa haiungi mkono upanuzi wa simu za mkononi za TTCL kutokana na mgongano wa maslahi uliopo kutokana na Zain kufanya biashara kama hiyo.
Ilifafanua kuwa nia hiyo ya Serikali inaifanya Zain ikose namna nyingine ya kuachana na kujihusisha na TTCL hasa kwenye mpango wa kupanua huduma za simu za mkononi za TTCL. Kwa barua hiyo ya Zain ni wazi kuwa wabia hao hawataki TTCL iendeshe biashara ya simu za mkononi; badala yake wanataka iendelee na biashara ya simu za mezani.
Katibu Mkuu Hazina, Ramadhan Kijjah, alikiri kupokea barua ya Zain ikiitaka Serikali ijiondoe katika kuiunga mkono TTCL ili ijitanue kwenye mtandao wa simu za mkononi.
Ni kweli hiyo barua nimeipata, lakini ninachoweza kukwambia ni kwamba sisi wizara hatuwezi kuchukua uamuzi wa kujiondoa hadi tutakapopata ushauri wa kitaalamu kutoka Wizara ya Miundombinu, alisema Kijjah.
Aliongeza kuwa wizara ya Miundombinu ndiyo yenye jukumu la kusimamia mambo ya kiufundi ya kampuni ya simu wakati Wizara ya Fedha ilishughulika na mambo ya fedha. Alipoulizwa sababu ya Zain kupinga Serikali kuiunga mkono TTCL huku wote wakiwa na hisa, Katibu Mkuu huyo alijibu: Hayo masuala yatajibiwa vizuri pale tutakapopata ushauri wa wenzetu wa Miundombinu.
TTCL ni kampuni inayomilikiwa na Serikali ya Tanzania ambayo imeingia ubia na kundi la kampuni za Zain ambapo Serikali inamiliki asilimia 65 wakati Zain ambayo awali ilikuwa Celtel inamiliki asilimia 35.
Kwenye barua hiyo , ilielezwa kuwa Zain hawafurahishwi na hatua ya TTCL ya kuwa na huduma ya simu za mkononi na inatamka wazi kuwa haiungi mkono upanuzi wa simu za mkononi za TTCL kutokana na mgongano wa maslahi uliopo kutokana na Zain kufanya biashara kama hiyo.
Ilifafanua kuwa nia hiyo ya Serikali inaifanya Zain ikose namna nyingine ya kuachana na kujihusisha na TTCL hasa kwenye mpango wa kupanua huduma za simu za mkononi za TTCL. Kwa barua hiyo ya Zain ni wazi kuwa wabia hao hawataki TTCL iendeshe biashara ya simu za mkononi; badala yake wanataka iendelee na biashara ya simu za mezani.
Katibu Mkuu Hazina, Ramadhan Kijjah, alikiri kupokea barua ya Zain ikiitaka Serikali ijiondoe katika kuiunga mkono TTCL ili ijitanue kwenye mtandao wa simu za mkononi.
Ni kweli hiyo barua nimeipata, lakini ninachoweza kukwambia ni kwamba sisi wizara hatuwezi kuchukua uamuzi wa kujiondoa hadi tutakapopata ushauri wa kitaalamu kutoka Wizara ya Miundombinu, alisema Kijjah.
Aliongeza kuwa wizara ya Miundombinu ndiyo yenye jukumu la kusimamia mambo ya kiufundi ya kampuni ya simu wakati Wizara ya Fedha ilishughulika na mambo ya fedha. Alipoulizwa sababu ya Zain kupinga Serikali kuiunga mkono TTCL huku wote wakiwa na hisa, Katibu Mkuu huyo alijibu: Hayo masuala yatajibiwa vizuri pale tutakapopata ushauri wa wenzetu wa Miundombinu.