Yuwapi David Kafulila wa Adani?

Small letter

JF-Expert Member
Joined
Jun 7, 2024
Posts
306
Reaction score
188
Hii si kawaida yake mtendaji mkuu huyu wa PPP kuwa kimya hasa pale anapoona umma wa Watanzania unahitaji majibu juu ya hoja yoyote ya PPP.

Kwa historia yake Kafulila ni kijana anayechukia sana rushwa na Ufisadi tangu utoto wake naamini hili kila Mtanzania atakubaliana nami.

Lakini tangu billionaire la Kihindi likutwe na hatia ya kutoa rushwa ili kupambania tenda huko Marekani jamaa huyu amekuwa kimya sana, kulikoni?

Mtakumbuka Billionaire hili la Kihindi tayari lilishaonesha nia ya kuwekeza zaidi nchi Tanzania hasa kwenye Umeme wa jua pamoja na kujenga msongo wa umeme.

Wenzetu Kenya tayari wamemfurusha Bwana Adani Gautam,

"Sisi Tanzania tuko Upande gani?"

Kafulila usijifiche njoo utuambie Adani bado anazo sifa za kuendelea kuwekeza Tanzania?

Je, kwenye hii vita ya Adani na Marekani na Tanzania tumo au au laa.

Kafulila njoo utuambie usikwepe.

Pia soma: David Kafulila atolea ufafanuzi wa Adani kuwekeza katika Miundombinu ya Umeme kwa Ubia
 
Sasa Mnataka ufafanuzi gani wabongo?
Mambo ya Adani na Marekani yanawahusu?
Halafu Adani kwani keshapewa huo mradi?
Adani sifa anayopoteza ni Uaminifu kwenye kupata kazi ila sio kwenye kufanya kazi.
Sioni tatizo la huyu muhindi
 
Huyu nyani mkongwe hasikii wala haoni analamba asali!
 
Sasa Mnataka ufafanuzi gani wabongo?
Mambo ya Adani na Marekani yanawahusu?
Halafu Adani kwani keshapewa huo mradi?
Adani sifa anayopoteza ni Uaminifu kwenye kupata kazi ila sio kwenye kufanya kazi.
Sioni tatizo la huyu muhindi
Wewe ni mtu wa ajabu sana .mla rushwa ana credibility gani na kama wewe uliwaaminisha wananchi huyo mtu ni safi je anayemtetea huyo mhindi ana sifa hata ya kuwa kiongozi?na wewe unajuaje kama hajapewa mkataba wakati Tanzania mkataba ni siri?
 
Wewe ni mtu wa ajabu sana .mla rushwa ana credibility gani na kama wewe uliwaaminisha wananchi huyo mtu ni safi je anayemtetea huyo mhindi ana sifa hata ya kuwa kiongozi?na wewe unajuaje kama hajapewa mkataba wakati Tanzania mkataba ni siri?
Kilicho Siri ni content sio Mkataba wenyewe
 

Kafulila hana la kujibu maana aliingia mazima sasa kajificha hasemi chochote kama anaendelea na Adan au hapana.
 
Bilashaka yoyote,
Muungwana yupo na anaendelea na majukumu yake mazito na muhimu kwa Taifa, kama kawaida ofisini kwake..

Infact,
visionary leaders, wenye IQ kubwa, huwa hawakurupukagi kama manyumbu kwenye masuala muhimu ya kitaifa.

Wanafuatilia kwa karibu Ukweli wa mambo, wanafanya uchambuzi na tathmini ya kina, na ndipo sasa wanakuja na alternative plans mbadala ikiwa wamejiridhisha, mapungufu au dosari za walionyesha nia ya uwekezaji katika eneo Fulani.

So,
ustahimilivu na subra ni jambo la maana sana kwenye mambo haya muhimu kwa mustakabali na maslahi mapana ya waTanzania wote πŸ’

πŸ’
 
Sawa Mzee ila hata tweet tu hakuna
 
Mambo ya 2mbili hayo,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…