Ngoja tu niandike labda utapata chochote kipya.
Kwanza JCB ni moja ya ma-MC toka kundi la Hip Hop linaitwa WATENGWA, Maskani yao ni Kijenge Juu Arusha... Watengwa ya kina JCB, CHINDO MAN, CHABA, YUZZO, DONNIE, D-WIDA n.k ni kundi bora la Hip Hop kwangu Mimi, kwann...
1.Aina ya Muziki wanaofanya ktk Hip Hop unakubalika 95% (Ni ile Underground/Hardcore)
2.Kila Msanii ndani ya kundi Anastaili tofauti kuanzia Uandishi, Mitambao (Flow), na Midundo (Beats)
3.Kila Msanii kwenye kundi ana uwezo wa kusimama kama yeye na akatoboa mbele ya hadhira/mashabiki.
4.Muda.. Kundi hili lipo pa1 kwa muda mrefu sana, na wala hakuna vurumai wala chokochoko kama makundi mengine
5.Kundi Ambalo limeweza kuipeleka RAP ya kiswahili mbele, hasa nchini Ufaransa.
Tuje Kwa JCB... HAHAHAHAH, Mtengwa huyu anafahamika kwa jina la JACOB MAKALLA, nnyumbani kabisa ni Kijenge ya Juu nyuma ya Metropoo.
JCB ni brother flani kwenye hii gemu, ameanzia mbali sana... Toka enzi za Hardcore Unit akiwa pa1 na Spac Dawg na Lord Eyez.. (KAMA UMESIKILIZA ARUSHA CYPHER... Kuna sehemu JCB anachana hivi... SIONGELEI 96, AU 95 NAONGELEA 94.. Miaka ya 94 Jacob alikua ashaanza hizi harakati)
Kimuziki hapa Bongo huwezi taja Ma-MC 10 kisha usilitaje jina la JCB, (Kuwa makini, sizungumzii Marapa kama Harmorapa, au wana hip hop mguu nje mguu ndani kama ney wa mitego, madee, n.k)... Huyu Jacob ni MC, anatembea na misingi ya Hip Hop Kichwani.
Uandishi... Uandishi wa JCB ni wakipekee sanaaaaa, hafanani na wala hafananishwi.. Ukiangalia vzr uandishi wa JCB ni ule wa moja kwa moja Ila kwa kutumia Lugha ya Mtaani sana, JCB anaweza andika mstari ambao uko nusu na ili ueleweke ni lazima pia usubiri ukomo wa msitari wa pili (kina kinachofuata)
2.Mitambao... Nianze kwa kukuuliza swali, umewahi kumsikiliza JCB... je, Flow yake inafanana na nani hapa Bongo... HAKUNA, ila kwa mbele... Kwa mbali sana tena sana JCB anafanana na B.I.G NOTORIOUS.. Mimi napenda sana kusikiliza ngoma zake kwasababu ya ile Flow yake.
3.Ujumbe wa nyimbo... JCB sio MC wa siasa (Political Mc/Rapper) kama R.O.M.A au Kala Jeremiah, JCB sio rapper/Mc wa mapenzi kama Godzilla, Pia JCB sio Rapper/MC asiye na kitu kikuu cha kukiongelea/kudeliver kwa watu kwa manufaa ya jamii kama Dogo Janja, Ney, Madee, Weusi, n.k... JCB Anaandika kuhusu Maisha Ya mtaani... Ambako ndio chimbuko la Hip Hop,,, hebu soma mistari kadhaa ya JCB hapa chini toka ktk ngoma mbalimbali.
"Kitaa tunaishi na nyangumi, so dagaa inabidi niishi kihuni/Mara huyo ughaibuni/minya mpaka December/nilipopata dili haramu kwa mpemba.."
"Usipoangalia utaendelea kununua ma-jeans na kuyavaa coco beach/wakati wenzio tunawaza Paris"
Kesho nikiweza nitakuwekea mistari ambayo itakubadilisha kwa sehemu kubwa.
JCB ameshstoa Album Kali sana, ukiwa unasikiliza kama ni MTU wa hip hop huwezi kupeleka nyimbo mbele, zaidi ya kurudisha nyuma.. Fikiria Umetoka kusikiliza "SHIKILIA" au "Nimefurahishwa" au "Nakalla" au "KIJITI".
Tafuta ngoma hizo hapo Juu..
b5-click