Yuko wapi rais Kikwete? Wako wapi viongozi wa nchi?

1800

JF-Expert Member
Dec 27, 2010
2,215
603
Wadau naamini wote tunayajua mambo ya mauji ra raia wasio na hatia yanavyoendelea kiholela huku kukiwa hakuna nia ya dhati toka kwa viongozi wetu kuanzia wa serikali mpaka jeshi la polisi,bad enough kwa kua hao viongozi wanaouliwa sio ndugu zao,wanazidi kututia uchungu kwa kwa kutuona Watanzania ni mahayawani wa kutupwa kwa kuja na majibu ya kejeli na propaganda nyepesi juu ya mauaji yanayoendelezwa.

Kauli kama za Chagongja,Tendwa,Nape Nnauye na jana Wassira kupitia Tbc,ni kauli za dharau kwa Watanzania kwa vile wanatuchukulia ni mahayawani tusiokua na tafakari hata kidogo kwa mambo yaliyo na majibu ya wazi kama matukio hayo ya mauaji yanayoendelea!nimeangalia video ya tukio la vurugu za Iringa,video ambayo nina amini serikali na jeshi la polisi wasingependa ionekane kwa Watanzania kutokana na udhalimu waliofanya na uongo wa kitoto wanaojaribu kutupa Watanzania,katika video hiyo labda mwanadamu aliye na upeo wa level ya kuku ndie atakaekubaliana na matamko ya kipropaganda mfu yanayotolewa na viongozi wetu kama Wassira na Tendwa!!

Najiuliza kitu kimoja rais wetu Kikwete mbona yuko kimya hajatoa kauli hata moja kama vile mauaji haya ni halali kabisa!ni wazi kipindi cha mwalimu Nyerere mtu kama kamanda Kamuhanda na askari wote waliohusika na tukio lile kwa kua wameonekana wazi sasa hivi wangekua ndani ya mikono ya sheria!serikali yetu imeshndwa kutumia rasilimali zetu kuendeleza viwanda,kuendeleza elimu afya hata kulinda raia wenu mpaka mnabariki mauaji kwa sababu na propaganda zisizo na kichwa wala miguu.

Wakumbuke Mwi Nyerere alijenga viwanda,aliboresha elimu kwa kilimo tu,hakugusa madini wala kulangua ardhi kwa wageni,wao wanagawana madini,wanagawa ardhi kwa kisingizio cha uwekezaji kumbe ni uchukuaji,wameua viwanda,wanadidimiza elimu kiasi cha wasiojua kusoma na kuandika imeongezeka (wanatengeza taifa la wajinga) bado hawaridhiki na sasa wameamua kuua raia wake bila hatia!ila wakumbuke kua bila kuchukua taadhari ukweli ni kua mwisho wa yote uko mlangoni,dalili za raia kuto ogopa wala kuheshimu vyombo vya dola hasa polisi,maandamano ya juzi ya waislamu yenye sauti kali mpaka waziri kusalimu amri,ni wazi sasa Watanzania hawako tayari kuendelea kunyanyaswa na wanajua haki zao zinakandamizwa na wachache!viongozi amkeni sasa kabla ya kuchelewa
 
Jamaa hafai kwa nafasi aliyonayo.Yeye cha muhimu kwake ni kujijengea jina katika mataifa ya nje.Sijui anaota kuja kufukuzia ukatibu mkuu wa umoja wa mataifa?

Tuna hasara kama taifa.
 
Jamaa hafai kwa nafasi aliyonayo.Yeye cha muhimu kwake ni kujijengea jina katika mataifa ya nje.Sijui anaota kuja kufukuzia ukatibu mkuu wa umoja wa mataifa?

Tuna hasara kama taifa.

Mkuu kwa kweli inatia shaka, hasira na huzuni pia! yeye kama kiongozi mkuu wa taifa ilipaswa kua mkali waziri wa wizara husika na IGP pia, naamini nao wangekua wakali na kuwachukulia sheria wote wanaofanya uovu huo! Sasa yeye hasipokua mkali anategemea nani atamuogopa?

Si kila mtu atakua anafanya madudu kwa kuamini kua mkuu hana muda wa kufuatilia mambo haya! Nakumbuka kipindi cha uongozi wa Mwl Nyerere, kuna vifo vilitokea kizembe na waziri wa mambo ya ndani kipindi hiko Alhaj Ally H Mwinyi alilazimika kujiuzuru bila kushinikizwa na hii yote ilitokana na uadilifu wa kiuongozi na ufuatwaji wa sheria chini ya Mwl Nyerere, lakini awamu hii kila waziri akifanya madudu tena ya wazi yeye ndie anakua mkali kwa wananchi na kejeli za dharau kama vile sijiuzuru,mtapata wapi waziri kama mimi!what a ****??!

Naamini Mh K.i.k.w.e.t.e angekua mkali kwa mawaziri na watendaji wake tusingeyashuhudia haya yanayolipelekea taifa letu kwenye giza la chuki, uhasama na wananchi kuanza kutolieshimu wala kuogopa jeshi la polisi na serikali
 
Mheshimwa wetu mtukufu Edward Lowassa alishasema kua hii nchi haina uongozi, kila mtu anajifanyia anachotaka...boy was he soo right...Hii nchi ina Rais on paper kwamba kikatiba rais tunae lakini kiuongozi hatuna na hii nchi imeshamshinda...he knows that..the people surrounding him know that and wananchi know that as well..hapa tunasogeza siku tuu tuna count down to 2015
 
Jamaa hafai kwa nafasi aliyonayo.Yeye cha muhimu kwake ni kujijengea jina katika mataifa ya nje.Sijui anaota kuja kufukuzia ukatibu mkuu wa umoja wa mataifa?

Tuna hasara kama taifa.

Inamaana hao umoja wa mataifa watakuwa wajinga kama waTz kwa kuongozwa na mtu asiyejua matatizo yao?
 
Mheshimwa wetu mtukufu Edward Lowassa alishasema kua hii nchi haina uongozi, kila mtu anajifanyia anachotaka...boy was he soo right...Hii nchi ina Rais on paper kwamba kikatiba rais tunae lakini kiuongozi hatuna na hii nchi imeshamshinda...he knows that..the people surrounding him know that and wananchi know that as well..hapa tunasogeza siku tuu tuna count down to 2015

Mkuu fanya kuediti na uondoe neno mtukufu wetu maana kama ni utukufu ni kwako na si wengine kama fisadi huko kwenu ndo mnaowatusa ishia kujisemea wewe na siyo wengine
 
Inamaana hao umoja wa mataifa watakuwa wajinga kama waTz kwa kuongozwa na mtu asiyejua matatizo yao?

Umoja wa mataifa ni mbali sana huko,hapa hapa Africa mashariki tu sidhani kama kuna nchi itakayohitaji hata ushauri tu wa mkuu huyu mara atakapotoka kuna madarak
 
Mkuu kwa kweli inatia shaka,hasira na huzuni pia!yeye kama kiongozi mkuu wa taifa ilipaswa kua mkali waziri wa wizara husika na igp pia,naamini nao wangekua wakali na kuwachukulia sheria wote wanaofanya uovu huo!sasa yeye hasipokua mkali anategemea nani atamuogopa?si kila mtu atakua anafanya madudu kwa kuamini kua mkuu hana muda wa kufuatilia mambo haya!nakumbuka kipindi cha uongozi wa Mwl Nyerere,kuna vifo vilitokea kizembe na waziri wa mambo ya ndani kipindi hiko Alhaj Ally H Mwinyi alilazimika kujiuzuru bila kushinikizwa na hii yote ilitokana na uadilifu wa kiuongozi na ufuatwaji wa sheria chini ya Mwl Nyerere,lakini awamu hii kila waziri akifanya madudu tena ya wazi yeye ndie anakua mkali kwa wananchi na kejeli za dharau kama vile sijiuzuru,mtapata wapi waziri kama mimi!what a ****??!naamini Mh K.i.k.w.e.t.e angekua mkali kwa mawaziri na watendaji wake tusingeyashuhudia haya yanayolipelekea taifa letu kwenye giza la chuki,uhasama na wananchi kuanza kutolieshimu wala kuogopa jeshi la polisi na serikali

ukimya wake ni ishara kuwa naye ni mhusika, tunachomwomba Mungu ni kuwa alikabidhiwa nchi hii salama na haiache salama. ukimya juu una lake jambo.
 
Amechanganyikiwa:A S-confused1:
Anaogopa nguvu ya umma:behindsofa:
 
Mtukufu ni Mungu peke yake, hakuna mwanadamu yeyote aliye na utukufu na aezaye kutukuka..soma Isaya 48: 7-8
 
Unayemwita mtukufu ni kwako wewe mwenyewe. usisemee watu wengine inawezekana unakula mafao haramu ya Richmwend na Dowananasi.
 
Hakuna haki wala haki haitatendeka iwapo wafuatao hawatajiuzulu au kuchomolewa na Kikwete kupisha uchunguzi:1. Waziri Nchimbi;2. Mkuu wa mkoa wa IRINGA; 3. RPC;4. Mkuu wa wilaya;5. OCD; na 6. mkuu wa upelezi mkoa (RCO), 7. Chagonja.
 
Leo naitangaza CCM kama janga la kitaifa linalohitaji kushughulikiwa na wananchi wote wenye mapenzi na hamu ya maendeleo. Ubaya wa CCM unaonekana vizuri kama mtu atatoka nje ya nchi hii. CCM imeshindwa kuunda serikali inayoshindwa kusema:
1. Acha rushwa, rudisha mali uliyoiba
2. Usijenge hapo
3. Usifanyie biashara hapo
4. Usifanye biashara hiyo hapo
5. Lipa kodi hata kama unauza sindano ya kuweka vishikizo kwenye shati
6. Kata miti hiyo wape vijana VETA wachonge madawati watoto wote wasikae chini
7. Sambaza maji ya mto huu na ule watu wote wapate maji
9. Chimba visima hapo na bwawa pale wananchi na mifugo yao wanywe maji
10. Jenga masoko kila kata watu wauze mazao na mifugo yao kirahisi
12. Vijana acheni kuhamia mijini kama hamna kazi za uhakika
13. Nununua boti na meli zile wakopeshe wavuvi wavue kisasa serikali ipate kodi yake
14. Wilaya hii limeni zao hili kisasa na wilaya ile limeni lile na nyie huko fugieni mifugo yenu huko huko
15. Bomoa jengo hili na lile hayakujengwa sehemu yake na hayana viwango
16. Asilimia 3 katika mikataba ya madini haitoshi kama ni hivyo yaacheni madini yetu mpaka itakapotangazwa tena

Msururu wa mambo ambayo serikali ya CCM inahitaji kutamka tu na kusimamia ili vilete tija kubwa kwa wananchi na taifa bila kuhitaji nguvu nyingi ama fedha za kigeni ni mengi. Kwanini CCM isitangaze kung'atuka kama alivyofanya muasisi wake alipotangaza kung'atuka wakati wananchi walivyokuwa wanafua nguo zao kwa mapapai mabichi? Hivi kweli viongozi wa CCM hawaoni aibu wanapotembelea miji ya nchi nyingine na kukuta mambo yanakwenda barabara? CCM sasa mtaji wao ni propaganda, wizi wa kura, nguvu za dola na rushwa, iko tayari kuona damu inamwagika ikilinda Tanzania isiangukie chama kinyinge, CCM itatutumbukiza katika janga baya sana kuonekana Afrika muda si mrefu kama itaendelea na spirit hii. Maana haitaweza kutunyamazisha wananchi wote mara moja kila mara, iko siku idadi ya watakaochoshwa na maisha haya itaongezeka, mungu si athumani yawezatokea mfadhili huko nje akakisikia kilio cha wanakandamizwa na CCM miaka nenda rudi, hapo ndipo janga kamili litakapotokea. Hebu ona Dar es Salaam iko kama gulio, kila mtaa umejaa nyanya, mitumba, chips, grocery. Mvua ikinyesha kidogo ndo usiseme, elimu duni, hospitali wagonjwa wako chini ya sakafu, nk. kwanini lakini CCM inahisi lazima ibaki madarakani?
 
Leo naitangaza CCM kama janga la kitaifa linalohitaji kushughulikiwa na wananchi wote wenye mapenzi na hamu ya maendeleo. Ubaya wa CCM unaonekana vizuri kama mtu atatoka nje ya nchi hii. CCM imeshindwa kuunda serikali inayoshindwa kusema:
1. Acha rushwa, rudisha mali uliyoiba
2. Usijenge hapo
3. Usifanyie biashara hapo
4. Usifanye biashara hiyo hapo
5. Lipa kodi hata kama unauza sindano ya kuweka vishikizo kwenye shati
6. Kata miti hiyo wape vijana VETA wachonge madawati watoto wote wasikae chini
7. Sambaza maji ya mto huu na ule watu wote wapate maji
9. Chimba visima hapo na bwawa pale wananchi na mifugo yao wanywe maji
10. Jenga masoko kila kata watu wauze mazao na mifugo yao kirahisi
12. Vijana acheni kuhamia mijini kama hamna kazi za uhakika
13. Nununua boti na meli zile wakopeshe wavuvi wavue kisasa serikali ipate kodi yake
14. Wilaya hii limeni zao hili kisasa na wilaya ile limeni lile na nyie huko fugieni mifugo yenu huko huko
15. Bomoa jengo hili na lile hayakujengwa sehemu yake na hayana viwango
16. Asilimia 3 katika mikataba ya madini haitoshi kama ni hivyo yaacheni madini yetu mpaka itakapotangazwa tena

Msururu wa mambo ambayo serikali ya CCM inahitaji kutamka tu na kusimamia ili vilete tija kubwa kwa wananchi na taifa bila kuhitaji nguvu nyingi ama fedha za kigeni ni mengi. Kwanini CCM isitangaze kung'atuka kama alivyofanya muasisi wake alipotangaza kung'atuka wakati wananchi walivyokuwa wanafua nguo zao kwa mapapai mabichi? Hivi kweli viongozi wa CCM hawaoni aibu wanapotembelea miji ya nchi nyingine na kukuta mambo yanakwenda barabara? CCM sasa mtaji wao ni propaganda, wizi wa kura, nguvu za dola na rushwa, iko tayari kuona damu inamwagika ikilinda Tanzania isiangukie chama kinyinge, CCM itatutumbukiza katika janga baya sana kuonekana Afrika muda si mrefu kama itaendelea na spirit hii. Maana haitaweza kutunyamazisha wananchi wote mara moja kila mara, iko siku idadi ya watakaochoshwa na maisha haya itaongezeka, mungu si athumani yawezatokea mfadhili huko nje akakisikia kilio cha wanakandamizwa na CCM miaka nenda rudi, hapo ndipo janga kamili litakapotokea. Hebu ona Dar es Salaam iko kama gulio, kila mtaa umejaa nyanya, mitumba, chips, grocery. Mvua ikinyesha kidogo ndo usiseme, elimu duni, hospitali wagonjwa wako chini ya sakafu, nk. kwanini lakini CCM inahisi lazima ibaki madarakani?

Mkuu umezidi kuipaisha CCM , kama hizo ndo zitakuwa sera za Magwanda.
 
wadau naamini wote tunayajua mambo ya mauji ra raia wasio na hatia yanavyoendelea kiholela huku kukiwa hakuna nia ya dhati toka kwa viongozi wetu kuanzia wa serikali mpaka jeshi la polisi,bad enough kwa kua hao viongozi wanaouliwa sio ndugu zao,wanazidi kututia uchungu kwa kwa kutuona watanzania ni mahayawani wa kutupwa kwa kuja na majibu ya kejeli na propaganda nyepesi juu ya mauaji yanayoendelezwa....
Tanzania hatuna rais wa nchi,hatuna viongozi wa nchi tunaviongozi wa ccm.ambapo wanachojali ni kulinda masilahi yao na familia zao. MUNGU IBARIKI TANZANIA.
 
ukimya wake ni ishara kuwa naye ni mhusika, tunachomwomba Mungu ni kuwa alikabidhiwa nchi hii salama na haiache salama. ukimya juu una lake jambo.

Mfano mdogo tu wa uongozi bora - kama Mhe Kikwete angekalipia kwa dhati mauaji ya Morogoro sidhani kama kuna kichaa ye yote kama huyu Kamuhanda angethubutu kufanya mauaji mengine Iringa baada ya wiki mbili.

Na sidhani kama kuna mediocres wake kama akina Nchimbi, Nape, Wassira, na Tendwa wangepata uthubutu wa kufanyia unyama huu kejeli kama hizo wanazotoa!!!

Binadamu anauwawa kama kuku (hata kuku huwa anawekewa staha ya dua) lijitu linajiita mkuu wa nchi linakaa kimya kana kwamba hiyo habari haimhusu.

Kweli ni kiwete wa akili!!!!!
 
Back
Top Bottom