Yuko wapi Nsa Kaisi ?

Yuko wapi Nsa Kaisi ?

by that time akiwa Kagera nafikiri ilikuwa ni 1983's, inaonekana unamjua sana huyu mheshimiwa; mimi nilikua mdogo sana lkn nimekua napata taarifa zake, watu wa namna hii ndiyo wanafaa kuongoza hii nchi bwana.
Wahujumu uchumi Mkoa wa Kagera miaka hiyo hawatamsahau! Alikuwa mmoja wa washauri mahiri wa uchumi wa rais wa awamu ya tatu!
 
Kwa ufahamu wangu nsa kaisi alikuwa daktari wa wakina mama na watoto muhimbili,. Lakini kwa sasa ni mstaafu,. Sjui atakuwa wapi dsm au kwao mbeya

Hapana sio huyu Daktari na Profesa wa magonjwa ya akina mama bali anayezungumziwa ni mwanasiasa ambaye alikuwa mkuu wa mkoa wa Kagera kwenye miaka ya 80 na baadae akawa mkuu wa mkoa wa Mtwara. Kuna wakati aliingia Bungeni Karimjee Hall akiwa amevaa suluali ya jeans ikabidi Ndugu Spika amtoe nje. Ninavyofahamu huyu Nsa Kaisi yupo hapa nchini na anaendelea vizuri na maisha
 
Ni kweli huyu bwana ni jembe, akiwa mkuu wa mkoa wa mara kuna wakati alikuwa anatembelea ofisi mbali mbali za umma kujionea ubabaishaji unaofanyika na anaondoka bila hata watendaji hao kufahamu kuwa mgeni wao alikuwa ni nani (kinyadhifa) na hivyo kujikuta watendaji hao wakiitwa ofisini kwake na kuambiwa mapungufu yao kazini.
 
Nakumbuka tetesi hii kutoka kwa Dereva wake wakati akiwa Kagera: Kuna mama mmoja alichukua maziwa lita 5 eti anaenda kumpelekea nyumbani kwake, akamkuta anapiga deki, basi akaambiwa asubiri kidogo. Baada ya kumaliza Kaisi akatoka na Mugs mbili, akamwambia yule mama lazima wayanywe wao wawili mpaka yaishe kwani yeye anakaa peke yake na yule mama anajua hilo (Nasikia alikuwa Secretary wake). Basi zoezi likaanza Mama wa watu akajikuta anakunywa maziwa vikombe kibao bila kutaraijia na yaliyobaki yule mama aliambiwa aondoke nayo.

Kwa kweli alikuwa anaepuka vishawishi vya Rushwa za aina zote.
Duh! Ee bwana ee! Hahahahaaaa! Huyo ndo Nsa Nkaisi! Kwa kweli hawa ndiyo wachache Mwalimu alifauru kuwapandikiza fikra za kizalendo (patriotism) katika itikadi ya Ujamaa na kipaumbele kwao ilikuwa ni kulitumikia taifa and no nonsense! Walikuwa hawahongeki bana.
 
Namkumbuka lilikuwa bonge la jembe enzi za mwalinu. Alipokuwa mkuu wa mkoa Kagera nakumbuka hakuwa na mke wala hausugeli kwake. Tabia yake hiyo hiyo, ukimsapraizi kwake utakuta anapiga deki (akiwa mkuu wa mkoa) na akikuheshimu sana asikutoe benzi atakutole kiti chini ya mti whoever you are na ataendelea kudeki. Patakapokauka ndo atakukaribisha ndani. Nkais bwana!

Hahaaaaaaa, umenikumbusha mbali sana mkuu. Nikupe basi, mkuu wa wilaya mtwara na RPC enzi hizo walimtembelea wikiendi wakamkuta anafanya usafi akawakaribisha vizuri na akawaambia tusaidiane basi kupiga deki ili tuendelee vizuri na mazungumzo yetu.

Ila pia nasikia alihasiwa kwa manufaa ya taifa hivyo inawezekana kweli hana mtoto
 
Ni kweli huyu bwana ni jembe, akiwa mkuu wa mkoa wa mara kuna wakati alikuwa anatembelea ofisi mbali mbali za umma kujionea ubabaishaji unaofanyika na anaondoka bila hata watendaji hao kufahamu kuwa mgeni wao alikuwa ni nani (kinyadhifa) na hivyo kujikuta watendaji hao wakiitwa ofisini kwake na kuambiwa mapungufu yao kazini.

100% right. Tulikuwa tunamuita mzee wa vipensi hususan akiwa katika shughuli za mtaani usiku wa manane. Aliwahi kupambana na majambazi peke yake usiku wa maneno eneo lilokuwa linaaminika eneo sugu mkoa fulani.
 
by that time akiwa Kagera nafikiri ilikuwa ni 1983's, inaonekana unamjua sana huyu mheshimiwa; mimi nilikua mdogo sana lkn nimekua napata taarifa zake, watu wa namna hii ndiyo wanafaa kuongoza hii nchi bwana.
Nakubaliana na wewe hapo pa bluu. Tatizo ndo hivyo tena wakisha-park wanaanza kulipia gharama ya sadaka waliyolitolea taifa and nobody cares enough for them! Pity for our national heroes.
 
Ni kweli huyu bwana ni jembe, akiwa mkuu wa mkoa wa mara kuna wakati alikuwa anatembelea ofisi mbali mbali za umma kujionea ubabaishaji unaofanyika na anaondoka bila hata watendaji hao kufahamu kuwa mgeni wao alikuwa ni nani (kinyadhifa) na hivyo kujikuta watendaji hao wakiitwa ofisini kwake na kuambiwa mapungufu yao kazini.

Yap huyo kanali wa jeshi alikuwa anapenda kuvaa pensi na kofia la "kandabongoman"
Alikuwa anaweza kutoka musoma na kuibuka wilayani bila taarifa na kuingia ofisi yeyote ya serikali kukagua namna huduma zinavyotolewa. Sasa akishamaliza mizunguko yake ndipo anawaita ofisini kwake wale wote aliopita ofisini kwao bila kujua na akakuta huduma zao zinalegalega.
Jamaa alikuwa anaogopwa ile mbaya na watumishi wa umma, hasa wazembe.
 
Kanali mstaafu anaishi Oysterbay si mbali sana na Karibu Hotel. Mara kdhaa anaonekana asubuhi akiwa katika joging. Hajaacha kuvaa pensi na raba! Huyu jamaa ni kifaa sijapata kuona. Wakati fulani Lowassa akiwa waziri, alizuru Mtwara wakati huo Kaisi akiwa RC. Chakula kiliandaliwa, lowassa na wageni wengine waliketi kula., Yeye akatoka akaenda zake kukaa chini ya mti akiwa hana habari na mtu hadi walipomnaliza kula. Huwezi kujua anakula muda gani au analala muda gani! Ana tabia zote za kikomando!!
 
nasikia aliumia vita ya kagera hadi jogoo amenuna! yuko kama dk kamuzu wamuyaya!
 
siyo kweli jamaa hana tamaa hiyo.

Tamaa? Nani kasema kwamba ana tamaa? Nilichosema ni kwamba huenda ni businessman.
Search for Acacia Co. Ltd. formed by 5 friends? I believe he was one of the directors?
Mkuu vipi ni ndugu yetu nini?
 
Kumbe nchi hii ina viongozi wa kukumbukwa!
 
Kuna dereva wake akiwa RC Mtwara alinunua mchele akiwa Mbeya alete Mtwara kwa family!Kaisi alivyoona kile kiroba wakiwa njiani kuja Dar akamwambia weka gari pembeni akakishusha kiroba barabarani!akamwambia marufuku kubeba mzigo bila ruhusa yangu na akamlipa hela yake wakakiacha kiroba.

Anaweza kusafiri na dereva from Mtwara to Dodoma hamna story zaidi ya salamu mpaka wanafika
 
Kama ni Kaisi wa Kyela nasikia kajilimbikizia sana mashamba na viwanja kule, pia ni mbabe sana kwa taharifa za juu juu..hayo ya uzalendo ndo kwanza nayasikia hapa! Tetesi za kutokuwa na mtoto hata mmoja nazo zipo!!
 
Back
Top Bottom