Yuko wapi Fred Mpendazoe?

Wadau hebu naomba kujulishwa wapi alipo Fred Mpendazoe je bado ni mwanachama wa Chadema?

ukipata jibu na mimi nauliza wako wapi wakina Juliana Shonza, Mtela Mwampamba, Dkt. Walid Kabour, Tambwe Hiza, Habib Mchange, Thomas Ngawaiya n.k
 
Fred Mpendazoe yupo SNV kama senior Advisor -WASH na anachapa kazi. Ni mwanachama hai wa Chadema. Kwa tetesi nilizo nazo atagombea nafasi ya makamu mwenyekiti kwenye uchaguzi wa ndani mwaka 2014.
 
ukipata jibu na mimi nauliza wako wapi wakina Juliana Shonza, Mtela Mwampamba, Dkt. Walid Kabour, Tambwe Hiza, Habib Mchange, Thomas Ngawaiya n.k

Mkuu umenikumbusha hawa bendera fuata upepo, nilishawasahau
 
Jamaa yupo na mkataba na kampuni moja ya wazungu na ktk mkataba wake ilikuwa ni kuepuka siasa public kipindi cha mkataba. Sasa sijui anafanya nini kukiimarisha chama?
 
Sasa aongee nini yeye sio kiongozi CDM kaajiriwa huo muda wa kupiga blah blah blah atautoa wapi?Huwezi tumikia mabwana 2 ajira na siasa.Labda Nape anaweza..............
 
Mpaka sasa Mpendazoe anapiga kampeni za chinichini Jimbo la Kishapu kupitia cdm. 2015 ame target kugombea tena jimbo la Kishapu kupitia cdm.
 
Yupo kaajiriwa na shirika la kimataifa la SNV.

Jana niliuliza mpendazoe bado ni mwanachama Wa chadema? nikashangaa ile post Leo siioni kuna mtu mwingine ameleta hii sio mbaya kama yupo SNV bado chadema? Mana kwenye mikutano ya kuimarisha chama sijawahi kumsikia au ndo wale wale mamluki??? Kazi maalum?????
 

mkuu una roho ngumu sana , ID yako imenisononesha sana ! Huyo jamaa ALICHOTUFANYIA MAN U SIWEZI KUSAHAU .
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…