Yuko wapi Emmanuel Nchimbi?


Kwanza kwa wanaomfahamu Nchimbi siyo mtu anayeweza kuitwa mwanasiasa Nguli. Nchimbi alibebwa na mambo machache

1. Family background- anatokea kwenye familia iliyokuwa na uongozi wa kisiasa
2. Students politics za Mzumbe zilimwigiza UVCCM
3. Wakati anaingia UVCCM hapakuwepo strong character hivyo ikawa rahisi kupenya
ILa, Nchimbi siyo strong politician is very average character kwenye mambo mengi.
Kuhusu kutoteuliwa katika teuzi za Magufuli zinazoendelea, jibu ni jepesi sana- Emanuel Nchimbi ndiye aliyeitisha kikao na waandishi wa habari na kueleza kwamba Chama hakifuata utaratibu katika kukata jina la Lowasa
 
Chukua hatua
 

Nchimbi na Sofia hawakua wanafiki maana waliweka wazi msimamo wao, maana hawezi kufanya hivo. Na wala hawakua na kosa Lolote maana kile kilikua kipindi cha uchaguzi na kuwa na makundi haikua tatizo
 
Nadhani kuna watu hawajui maana ya unafiki. Unafiki ni mtu kufanya vitu kwa siri. Lakini Nchimbi hakuwa mnafiki alisimamia anachokiamini.
Kweli ndiyo maana hawezi kufanya kazi na Magufuli, mpaka leo yeye bado anasimamia imani yake kwamba Lowassa ndiye rais aliyepaswa kuwa madarakani na siyo JPM.
 
Hivi yupo wapi dkt Slaa maana aliipigania sana Chadrma
 
Dr Nchimbi hakuwa mnafiki,ipo siku chama chake kitamtendea haki,kama walivyomkumbuka Philipo Malmo makamu mwenyekiti wa CCM bara
 
Muulize Lowassa!
 
Umemaliza kila kitu mkuu, Mungu akubariki.
 
Hivi yupo wapi dkt Slaa maana aliipigania sana Chadrma
Jaribu kuficha ujinga wako, kila anefuatilia siasa anajua alipo Dr. slaa kwa kuwa anapost mambo kutoka huko alipo na aliaga anaenda kupumzika, sio lazima uingize chadema hata kwenye swala lisilo husu chadema, wote tunajua Nchimba kapotea kimya kimya ndio maana anauliziwa hapa, kama unataka kujua zaidi kuhusu slaa anzisha mada yako acha kudandia dandia mwisho utaaibika.
 
Dr Nchimbi hakuwa mnafiki,ipo siku chama chake kitamtendea haki,kama walivyomkumbuka Philipo Malmo makamu mwenyekiti wa CCM bara
Philipo Malmo amekuwa makamu wa chairman tangu lini au mimi ndo niko nje ya habari mkuu
 
Mtoa post angependa kuona swali lake likijibiwa na yeye akalizika na majibu lakin kinachoendelea!!!!
 
Anaweza kuwa katibu mkuu wa ccm na hiyo itawaduwaza wengi, siasa ni mahesabu siyo sanaa Magu atathibitisha hilo.
 

Kwa hali hii huyu mtu lazma ataishi kama shetani ndani ya miaka kumi,
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…