Yu wapi Bi Naila Jidawi...?

Yu wapi Bi Naila Jidawi...?

alipata kuwa mbunge cuf na baadaye kuwa mgombea mwenza wa nccr mageuzi 2005 chiniya dk.mvungi lakini kwa muda mrefu hatujapata kumsikia tena,, kwa yeyeotemwenye habari yake atujuze,,,,,
 
Bibi Naila Majid Jidawi
1.Alikuwa mbunge kwa tiketi ya CUF mwaka 1995, akafukuzwa kwenye chama na kuwa mbunge wa makakama mpaka 2000,
2. Alihamia NCCR na kuwa mgombea mwenza wa urais pamoja na marehemu Dr. Mvungi 2000
3. Hotel yake aidha iliunguzwa au iliungua wakati huo
Kwa sasa inasemekana anaishi na mme mwingine inchi moja wapo ya kiarabu hana mpango wa siasa pia wanafanya kazi sambamba na Rahima Quaros (malkia wa nyuki).
 
Wakuu wa JF,

Naulizia tu kwa kujikumbusha historia ya siasa ya Zanzibar kidogo. Yu wapi Bi Naila Jidawi ? Bi mkubwa mwenye makeke sana katika harakati za chama cha CUF kule visiwani Zanzibar

Naomba tu kuweka kumbukumbu sawa kwa kusema mie nlianza kumfahamu huyu Bi mkubwa miaka ya 1994 nlipokuwa Mgambo Jkt kwa kupitia luninga ya TV ZANZINAR yaani TVZ channel kule Mgambo tulifunga antena ndefu sanaa

Sasa huyo Bi mkubwa Naila Jidawi kipindi kile ndio ugomvi wake na Maalim Seif uko juu sanaa , Nnachokumbuka ni kuwa Maalim Seif hakuthamini hata kidogo mchango wa Bi mkubwa huuyoo ambae alitoa nyumba yake kuifanya ofisi na mwisho wa siku Maalim Seif akamfukuza kwenye chama....

Wadau wenye kumbukumbu zaidi, hebu fungukeni zaidi....

Huyu Bi mkubwa ndio anafaa kuwa Rais wa kike ajaye kwa Zanzibar na huku bara tukiwa na Makinda yetu....

Shata apu!
 
Bi Naila yupo Unguja anafanya biashara zake na kusupport akina mama wajasiriamali. Ana Hotel maeneo ya Bwenjuu kwa wale wanaoifahamu Unguja.
Bwenjuu! Inaitwa jina lipi mh.? Ni Paje au Bwenjuu?
 
Tatizo la Slaa anahisi kwamba kuna sehemu fulani ya maisha yake aliikosea, sasa kama vile anataka kucatch up. Katika kufanya hivyo ndio anajikuta wakati mwingi anafanya uhuni usioendana na umri wake. Age mates wake kina Kingunge na malecela sasa hivi wameshastaafu...
Hivi kutofautiana itikadi yaweza kuwa chanzo cha kukosa nidhamu kiasi hiki? Unatumika/kujipendekeza vibaya sana mkubwa wangu. Hata mimi ni CCM tena nyadhifa kibao UVCCM, siwezi kuwa na tabia mbovu kama yako kwani naongozwa na kanuni halisi za chama na mwasisi mareh. Nyerere na mafundisho ya dini yangu. Mwana CDM mwenye hekima hawezi kusimama na kumkashfu mzee Makamba au Kigunge. Tabia mnazoiga toka kwa kina Lissu,Lema,Mwingulu na Nkamia zitawapeleka kubaya sana. Muda mwingine yapaswa UJITAMBUE.
 
Kuna mwanasiasa mwingine Wa Znz aliwahi kutekwa alikua muwakilishi Wa jimbo la Mkunazini Kupitia Cuf anaitwa Msabaha!
Huyu nae sijui yuko wapi?

Huyu mama Jidawi atakua kabanwa na majukumu ya familia na aliamua kuachana na Siasa!
 
Anamiliki RGB oil..na visima vya mafuta Oman..alizaa na JK in late 1980's mapacha wawili wakiume..chezea malkia wa "gon'gole" wewe

Mh! Ama hakika Uzi unavyobadilishwa mpaka raha, toka Kwa mama Jidawi mpaka Malkia wa Nyuki kuzaa na JK!!! Ama hakika hii ndo JF HGT.
 
mkuu mbona mada haijataja dr Slaa? inazungumzia Zanzibar na Jidawi sasa hayo ya Slaa umeyatoa wapi. Chadema wanawatesa sana nyie ndugu,mtakufa na presha kwasababu ya Chadema wakati wenyewe wanakula bata.

Kwani umeambiwa mada imewekewa mpaka wa Jidawi tu?
 
Afadhali Nimeianza siku yangu na kicheko......eti "Hizi siasa za vyama vya magumshi ni TOO RISKY, ndio maana Dr. Slaa kasema ahakikishiwe fungu lake in advance". Wamuulize Mrema (Lyatonga)alivyopigika kwa kuingia kichwa kichwa NCCR- Mageuzi.

kimsingi hata wakimzitto kabwe dr. slaa wataendelea kumlipa kama mbunge wa bunge la dodoma ndiyo mkataba wake cdm ili kugombea urais wa tz sasa zitto naona alichelewa kuingia mkataba wa namna hiyo
 
Na mume wake alikuwa m1 wa makomandoo hodari wa JWTZ wa zama zao amabao walipigana vita mbali mbali ikiwemo ya RENAMO na FRELIMO mozambique!
 
The fixer

Duh umewahi kuishi Mgambo JKT,aysee umenikumbusha hiyo sehemu.Nimeishi kwa muda mrefu sana Mlimani.
Kwabojo,Kwa msanga,Gendagenda.Wachaa kabisa Tz ni kubwa jamani..!
 
Bi Naila Jidawi pia alikuwa ni Mwanasheria by profession. Alikuwa mwanasiasa kwa mapenzi yake. Alikuwa mpigania haki na mwanaharakati makini. Alikuwa Mwanamke jasiri.

Bi Naila Jidawi vilevile alikuwa ni mke wa aliyekuwa Komando maarufu wa JWTZ, ambaye jina lake lilipata kutamba sana miaka ya 1970's - 80's kutoka Zanzibar Colonel Mahfudh ambaye baadae alikwenda kuishi uhamishoni nchini Msumbiji mara baada ya kumalizika vita ya Kagera.

Bi Naila Jidawi na wenzie kadhaa walifukuzwa kwenye chama cha CUF baada ya kuhitilafiana na Katibu Mkuu wao Maalim Seif Sharif Hamadi. Na baada ya juhudi za kurejea ndani ya CUF kupitia njia za ki diplomasia na hata zile za kisheria (court of law) kushindikana alijiunga na CCM.

Bi Naila Jidawi bado yupo Zanzibar lakini naona ameamua kuwa 'dormant politician'. Sidhani kama ana hamu tena na siasa🙂
 
Bwenjuu! Inaitwa jina lipi mh.? Ni Paje au Bwenjuu?

Mkuu Ng'wanapagi..Ni Bwejuu siyo Bwenjuu..Ni sehemu mbili tofauti..

Paje unapovuka kituo kidogo cha polisi unaenda barabara ya Kulia na Bwejuu ni Kushoto kama unaelekea Michamvi..
 
Last edited by a moderator:
mkuu mbona mada haijataja dr Slaa? inazungumzia Zanzibar na Jidawi sasa hayo ya Slaa umeyatoa wapi. Chadema wanawatesa sana nyie ndugu,mtakufa na presha kwasababu ya Chadema wakati wenyewe wanakula bata.

Wasipomtaja wanakosa posho ya siku hiyo. Ndio maana kila siku wanazusha kila aina ya uzushi kuwapaka matope sana sana Dr Slaa, Mh Mbowe, Mh Lema, Mh Lissu na Mh Mnyika. Akilini mwao sijui wanaamini uzushi ukirudiwarudiwa unageuka ukweli???!!!
 
Wasipomtaja wanakosa posho ya siku hiyo. Ndio maana kila siku wanazusha kila aina ya uzushi kuwapaka matope sana sana Dr Slaa, Mh Mbowe, Mh Lema, Mh Lissu na Mh Mnyika. Akilini mwao sijui wanaamini uzushi ukirudiwarudiwa unageuka ukweli???!!!

Mkuu kitu cha uongo kikirudiwarudiwa sn Jamii hufikia hatua wanakiamini!! Kwahiyo Mkuu hiyo propaganda ya uongo Mkuu inafanya sn kazi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom