Yote tisa, kumi CCM wametuweza kweli kweli

MMGL0846.jpg


Chakula kwa Fikra Zako: CCM wamefanikiwa jambo moja ambalo sikulidhania linaweza kufanikiwa miezi michache tu nyuma; wamewachagulia wapinzani mgombea wao wa Urais, timu yake na mashabiki wake na kulazimisha upinzani (hasa CHADEMA) kubadilisha wagombea wake na kuwapokea kwa furaha waliotolewa kama zawadi na CCM kwao.

Kama kweli - alivyodai Lissu - kuwa CHADEMA walishampitisha Dr. Slaa kuwa mgombea wao wa Urais kwenye kikao cha Kamati Kuu basi kumuondoa yeye (aliyekuwa anahofiwa sana na CCM labda kuliko mtu mwingine yeyote miaka hii mitano) ni mkakati ambao umefanikiwa kupitiliza. Leo wana CDM (sijui kama ni wengi au la) wamejipanga kushangilia mapinduzi ya kimkakati waliyofanyiwa na CCM wakiamini kuwa wamepewa zawadi.

Leo mtu aliyekijenga chama na kupigwa pamoja nao anaonekana hana mpango ati ni kikwazo cha "mabadiliko" wakati mtu ambaye hajawahi kuwa na rekodi ya mabadiliko au hata kuutetea upinzani anahusishwa na mabadiliko! Jeraha hili la upinzani haliwezi kuponeshwa na wale wale waliosibabishwa; tuliambiwa "akili ndogo zisitawale akili kubwa"... sasa siyo tu akili ndogo zinatawala akili kubwa; akili kubwa zenyewe hazijijui kuwa ziliwahi hata kuwa akili kubwa!

Vyovyote vile itakavyokuwa CCM itaendelea kutawala ama kupitia Magufuli au kupitia Lowassa. Hili wapo ambao hawataki kuamini ndilo limetokea huku wenyewe wakiamini kuwa wanapigania "mabadiliko". Kuigeuza upande mmoja wa shilingi ukasema "umebadilisha" ni kweli; lakini hujabadilisha shilingi!

Hapa CCM wametutia kidole...




Cha macho!.. hata hatuoni tena.


MMM

Upo Tanzania? Issue siyo Lowasa Vs Magfuli au Ukawa Vs CCM. Issue ni Change Vs CCM and my best choice is Change. Period.
 
Dr Slaa alikuwa mgombea 'kiraka' alipokosekana Sitta walimweka yeye, angekosekana Lowasa au Sumaye wangemweka yeye. Hilo Dr Slaa analijua manaake hakuna nchi yeyote duniani 'Padre' wa katoliki amekuwa Rais. Mwanakijiji muulize Dr Slaa akiwa masomoni Vatican alikuwa ni katibu wa ccm tawi la vatican nini ilikuwa role yake? kuna uhusiano gani kati ya CCM na vatican? MM ishi katika uhalisia tatizo sio Lowasa mulika torch vizuri kama wewe siyo lofa utaliona!
 
Kama nakumbuka vizuri, mwaka 2005 Mzee Mwanakijiji ulimuunga mkono Kikwete na nakumbuka uliwahi kusema mara kadhaa kule bcstimes.com kwamba wewe ni CCM.

Sasa mimi nauliza: je, wewe bado ni mwanachama wa CCM/ wewe bado ni CCM?

Kama wewe si mwanachama wa CCM/ wewe si CCM, ni lini uliacha kuwa mCCM?

Manake saa ingine huwa nadhani kwamba huenda upinzani wa Tanzania umejaa mamluki wa CCM ili kuudhofisha tu.


Makubwa haya!
Nyani Ngabu vipi tena hizi ngumu za Usoni muda huu kweli na utu uzima huu Mzee wa Watu ataamka kweli?.
Kumbe mamluki wa mabadiliko wako kila kona.Dah! ni heri Wapumbafu na malofa waliokuwa Jangwani wakaendelea na safari yao ya Matumaini bila Kamanda anayesomeka.
 
Last edited by a moderator:
Pole sana km unadhani lowasa anatumika na ccm, kwa taarifa yako lowasa kuhama ccm kamaanisha!!

Pili km unafikir ccm wanatumia lowasa, jiulize hizi rough za nn? Hii nguvu kubwa inayotumika kumzuia, jiulize ni nn?
 
Vyovyote vile itakavyokuwa CCM itaendelea kutawala ama kupitia Magufuli au kupitia Lowassa. Hili wapo ambao hawataki kuamini ndilo limetokea huku wenyewe wakiamini kuwa wanapigania "mabadiliko". Kuigeuza upande mmoja wa shilingi ukasema "umebadilisha" ni kweli; lakini hujabadilisha shilingi!

Hapa CCM wametutia kidole...




Cha macho!.. hata hatuoni tena.


MMM

Kumbe sijakusoma vizuri. Kuchukua like- Lowassa Moyoni akiwa CCM lakini kwa nje yuko na jezi ya CDM kwa mwamvuli wa CDM hukua aimba Peoples Poweeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeer! Kwa 90% tayari hatua moja ya mabadiliko lazima tukubaliane na hili na kama hili hulioni kweli kazi ya mabadiliko hata umlete Masiha itakuwa ngumu.


Vyombo vingi vya habari viliita umati huo “Mafuriko”
 
CDM imeuza tunu zake kwa u-Raisi, kama vile Esau alivyouza haki ya uzaliwa wa kwanza kwa chakula. Wasipoupata, Mbowe na wote waliojiingiza kumleta Lowassa wawe voted out of the office.
 
Kama ilikuwa sio ya kuchambua wagombea kwanini aanze kueleza maswala Ya Jangwani kuhusu Babu seya,mashekhe mara kusomba watu kwenye mikutano wakati kwa mujibu wa maelezo yake alisema alishajitoa zamani kabla hata kampeni hazijaanza,je hayo nayo ni miongoni ya mambo yaliyomfanya ajitoe kwenye siasa..jaman tukubali tu kuwa Dr.Slaa alitakiwa atueleze kuhus wagombea wengine.

Alikuwa akimwelezea mhamiaji haramu wa CHADEMA na sera mpya mpya alizokuja nazo kuona kama kuna lolote aliloongeza
 
Pole sana km unadhani lowasa anatumika na ccm, kwa taarifa yako lowasa kuhama ccm kamaanisha!!

Pili km unafikir ccm wanatumia lowasa, jiulize hizi rough za nn? Hii nguvu kubwa inayotumika kumzuia, jiulize ni nn?
Of course kamaanisha ili aupate uraisi. Unafikiri nini kingine kimemhamisha?
 
Kama nakumbuka vizuri, mwaka 2005 Mzee Mwanakijiji ulimuunga mkono Kikwete na nakumbuka uliwahi kusema mara kadhaa kule bcstimes.com kwamba wewe ni CCM.

Sasa mimi nauliza: je, wewe bado ni mwanachama wa CCM/ wewe bado ni CCM?

Kama wewe si mwanachama wa CCM/ wewe si CCM, ni lini uliacha kuwa mCCM?

Manake saa ingine huwa nadhani kwamba huenda upinzani wa Tanzania umejaa mamluki wa CCM ili kuudhofisha tu.[/QUOTE]


Ulikua hujui hilo

Kinachotokea sasahivi wale mamluki hawawezi tena kubaki alipo EL ....Coz anawajua vizur
 
Sitegemei leo nimuone Mzee Mwanakijiji akimkubali Lowassa hata kama atakuwa huku Ukawa, ninacho kiona ni kitu kama chuki binafsi na kinyongo kisicho kwisha, anakumbuka ilikuwa ni miaka miwili baada ya Lowassa kujiuzulu hukusiana na Richmond na hakuwahi kuongea kwa kipidi chote hicho, Kuna siku moja Lowassa akahojiwa na Tido Muhando kipindi hicho akiwa Tbc, Mzee Mwanakijii kwa kufuraha na bashasha isiyojificha alikuwa wa kwanza kumpigia simu Mwakyembe kufanya nae mahojiano akimwelezea kijinsi Lowassa alivyokuwa akiongelea juu ya mwenendo wa lilesaka la Richmond, wakati huo Mwakyembe hakuwa na taarifa ya mahojiano yale aliyekuwa wa kwanza kumwambia ni huyu huyu mzee....

Nisimalize uhondo pitie hii video halafu mniambie inahashiria nini??

Mara nyingine najiuliza inakuwaje kuhojiwa ahojiwe Lowassa majibu ya maswali ya kwenye yale mahojiano aulizwe Mwakyembe badala ya Lowassa mwenyewe?? Mwanakijiji alikusudia nini hapa?





Hii hapa mahojiano kati ya Tido na Lowassa

Salary Slip chukua haya maelezo yangu unganisha na mada yako tafadhali..


Asante kwa taarifa, nilikuwa sijui
Ngoja nafuatilie
 
Last edited by a moderator:
MMGL0846.jpg


Chakula kwa Fikra Zako: CCM wamefanikiwa jambo moja ambalo sikulidhania linaweza kufanikiwa miezi michache tu nyuma; wamewachagulia wapinzani mgombea wao wa Urais, timu yake na mashabiki wake na kulazimisha upinzani (hasa CHADEMA) kubadilisha wagombea wake na kuwapokea kwa furaha waliotolewa kama zawadi na CCM kwao.

Kama kweli - alivyodai Lissu - kuwa CHADEMA walishampitisha Dr. Slaa kuwa mgombea wao wa Urais kwenye kikao cha Kamati Kuu basi kumuondoa yeye (aliyekuwa anahofiwa sana na CCM labda kuliko mtu mwingine yeyote miaka hii mitano) ni mkakati ambao umefanikiwa kupitiliza. Leo wana CDM (sijui kama ni wengi au la) wamejipanga kushangilia mapinduzi ya kimkakati waliyofanyiwa na CCM wakiamini kuwa wamepewa zawadi.

Leo mtu aliyekijenga chama na kupigwa pamoja nao anaonekana hana mpango ati ni kikwazo cha "mabadiliko" wakati mtu ambaye hajawahi kuwa na rekodi ya mabadiliko au hata kuutetea upinzani anahusishwa na mabadiliko! Jeraha hili la upinzani haliwezi kuponeshwa na wale wale waliosibabishwa; tuliambiwa "akili ndogo zisitawale akili kubwa"... sasa siyo tu akili ndogo zinatawala akili kubwa; akili kubwa zenyewe hazijijui kuwa ziliwahi hata kuwa akili kubwa!

Vyovyote vile itakavyokuwa CCM itaendelea kutawala ama kupitia Magufuli au kupitia Lowassa. Hili wapo ambao hawataki kuamini ndilo limetokea huku wenyewe wakiamini kuwa wanapigania "mabadiliko". Kuigeuza upande mmoja wa shilingi ukasema "umebadilisha" ni kweli; lakini hujabadilisha shilingi!

Hapa CCM wametutia kidole...




Cha macho!.. hata hatuoni tena.


MMM

Along th eway, CDM ilikusanya kila aina ya majuha ili mradi kuonesha kuwa wanapendwa na wanachama wengi. bahati mbaya hii kusanya kusanya, imewapa nguvu hawa akili ndogo na ndio wamekuwa wapayukaji wakuu na wenye kusikilizwa zaidi na mwenyekiti, ambaye ndio mshika rimoti ya kila kitu CHADEMA.


Kinachoendelea sasa ni majonzi, CCM hakuna walilofanya kuzidi ubwege wa CDM kukubali kuamuliwa na watu wasioweza hata kufanya constructive analysis ya sentensi zaidi ya 3.

akipewa hoja defense mechanism yake ya kwanza ni kuhamaki, ya pili ni kutukana. SMH
 
Nimeshaanza kuiona mijadala itakayokuwepo hapa baada ya uchaguzi, matokeo kutangazwa, na Rais kuapishwa,

Niombe tu watu tuweke akiba ya maneno, hasa washabiki wa chadema (sio wanachama,
Chadema imeharibiwa na washabiki na sio wanachama, watu ambao hauwezi kujua kama kesho watakuwepo, pale inapotokea mchezo kuokwenda kama walivyotegemea washabiki. Mtaji pekee utakaobaki, ni wanachama, ambao kwa wakati huu chadema imeamua kuwanyamazisha na kutotaka kuwasikiliza kwa namna yoyote, yoyote anayetoa maoni ambayo yapo against wao, regadless ni kweli anaonekana msaliti.

As for me, I'm loading for November, after election......
 
Back
Top Bottom