GE2025 Yericko Nyerere: Nitaisuka upya Kigamboni, Barabara za Lami na kufuta Tozo za Daraja na Vivuko

GE2025 Yericko Nyerere: Nitaisuka upya Kigamboni, Barabara za Lami na kufuta Tozo za Daraja na Vivuko

Matukio, Taarifa, Habari na Mijadala ya Wananchi WAKATI wa Mchakato wa Uchaguzi Mkuu 2025

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,499
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ameahidi kuibadilisha Kigamboni kwa kuhakikisha barabara zote kuu zinawekwa lami.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni, Yericko amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshindwa kukamilisha mradi wa barabara ya kilomita 60 kutoka Feli hadi Buyuni, licha ya kuanza tangu mwaka 2008, ambapo kila mwaka wamekuwa wakijenga kilomita moja pekee.

Ameongeza kuwa CCM imekuwa ikiwaletea wananchi kanga na vitenge badala ya kutekeleza miradi ya maendeleo, hali aliyoitaja kuwa ni hatari kwa mustakabali wa wananchi wa Kigamboni.

Kuhusu Tozo za daraja na vivuko amedai ni haramu na wizi ambao wanafanya CCM na Serikali yake

 
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ameahidi kuibadilisha Kigamboni kwa kuhakikisha barabara zote kuu zinawekwa lami.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni, Yericko amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshindwa kukamilisha mradi wa barabara ya kilomita 60 kutoka Feli hadi Buyuni, licha ya kuanza tangu mwaka 2008, ambapo kila mwaka wamekuwa wakijenga kilomita moja pekee.

Ameongeza kuwa CCM imekuwa ikiwaletea wananchi kanga na vitenge badala ya kutekeleza miradi ya maendeleo, hali aliyoitaja kuwa ni hatari kwa mustakabali wa wananchi wa Kigamboni.

Kuhusu Tozo za daraja na vivuko amedai ni haramu na wizi ambao wanafanya CCM na Serikali yake

Huyu anachekesha sana yaani sana 😃😃😃😃😃
 
hilo pekee linaonyesha hajui hata kazi ya ubunge ni ipi ingawaje anataka kuwa mmoja wao, sasa hayo yote atayafanya yeye kama nani huko serikalini? sana sana mbunge anachoweza kufanya ni kusema bungeni kwamba jimboni kwake hakuna barabara lkn hilo kila mbunge wa tanzagiza anaweza kulisema na anayeamua wapi br ijengwe ni serikali tu na siyo mbunge ...
 
Haka kajamaa hakana jipya ..kanaropoka tu kama kamevimbiwa
 
Hapo kwenye tozo kufuta unacheza na ajira za watu apo sizani km utatoboa
 
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Kigamboni kupitia Chama cha Ukombozi wa Umma (CHAUMMA), Yericko Nyerere ameahidi kuibadilisha Kigamboni kwa kuhakikisha barabara zote kuu zinawekwa lami.

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni, Yericko amesema Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimeshindwa kukamilisha mradi wa barabara ya kilomita 60 kutoka Feli hadi Buyuni, licha ya kuanza tangu mwaka 2008, ambapo kila mwaka wamekuwa wakijenga kilomita moja pekee.

Ameongeza kuwa CCM imekuwa ikiwaletea wananchi kanga na vitenge badala ya kutekeleza miradi ya maendeleo, hali aliyoitaja kuwa ni hatari kwa mustakabali wa wananchi wa Kigamboni.

Kuhusu Tozo za daraja na vivuko amedai ni haramu na wizi ambao wanafanya CCM na Serikali yake

Lile daraja lilijengwa kwa baadhi ya fedha za mifuko ya Bima ya Taifa. Wakifuta tozo hii mifuko itarudishaje fedha zao na kupata faida.
 
Back
Top Bottom