Zogoo da khama
JF-Expert Member
- May 20, 2013
- 638
- 607
Habari
Kuna hii tabia ya wapangaji kutojishughilisha/ kutoshiriki shughuli za kijamii katika maeneo waliopanga shida nini?
Mtu anapanga lakini hashiriki iwe msiba, harusi, kutengeneza barabara, kuchimba mtaro wa maji anasema hayamuhusu anayehusika ni mwenye nyumba hii iko sawa kweli?
Haya mtaani jamaa kafiwa na mzazi wake maiti ipo mwananyamala hospitali nyumba yote ni wapangaji tupo pia kila mtu na zake, majirani wanapita kafunga turubai ni yeye na nduguze toka jpili leo ndio wanazika, wamepita juu kwa juu toka mwananyamala hadi makaburini, jibu analo, huko FC dada kafiwa na mtoto kapakia maiti kwenye daladala wakagoma, pesa ya kukodi usafiri hana wala jeneza, mtaani wamemsusa kwavile hashirikiani nao, inabidi wana FC waitane kwenda kumfariji na kuona jinsi ya kuzika.
Tunajenga kizazi cha aina gani? Ukiwa mpangaji ndio huruhusiwi kuchangamana na jamii inayokuzunguka kweli, yakikufika utafanyaje?
Kuna hii tabia ya wapangaji kutojishughilisha/ kutoshiriki shughuli za kijamii katika maeneo waliopanga shida nini?
Mtu anapanga lakini hashiriki iwe msiba, harusi, kutengeneza barabara, kuchimba mtaro wa maji anasema hayamuhusu anayehusika ni mwenye nyumba hii iko sawa kweli?
Haya mtaani jamaa kafiwa na mzazi wake maiti ipo mwananyamala hospitali nyumba yote ni wapangaji tupo pia kila mtu na zake, majirani wanapita kafunga turubai ni yeye na nduguze toka jpili leo ndio wanazika, wamepita juu kwa juu toka mwananyamala hadi makaburini, jibu analo, huko FC dada kafiwa na mtoto kapakia maiti kwenye daladala wakagoma, pesa ya kukodi usafiri hana wala jeneza, mtaani wamemsusa kwavile hashirikiani nao, inabidi wana FC waitane kwenda kumfariji na kuona jinsi ya kuzika.
Tunajenga kizazi cha aina gani? Ukiwa mpangaji ndio huruhusiwi kuchangamana na jamii inayokuzunguka kweli, yakikufika utafanyaje?