UMUGHAKA
JF-Expert Member
- Sep 1, 2021
- 2,157
- 10,718
Nsikuchoshe na Usinchoshe, tusichoshane!
Ni kama vile Young Africans ni fupa la Sangara ambalo limenasa kwenye kolomeo la zee lenye husda liitwalo "TFF".
Kibaya zaidi fupa hilo limekwama na halimezeki wala halitoleki iwe kwa winchi ama kamba za chuma! Fupa hilo la Sangara linaendelea kuwaumiza viongozi wa TFF na hawana cha kufanya zaidi ya kuendelea kugugumia maumivu!
Miaka 2 ya Ubingwa wa Yanga viongozi wenye chuki na husda ya waziwazi kwa Yanga tumeshuhudia wakifanya fitina za kila namna ili Yanga aside Bingwa lakini imeshindikana.
1. Miaka 2 mfululizo wamekuwa wakimpangia Yanga ratiba ambayo si rafiki, mechi za mwisho za Yanga kwa misimu 2 mfululizo amekuwa akimalizia kule mkoani Mbeya, hii si bahati mbaya, tunajua ni uhuni na fitina ili kuihujumu Yanga lakini bahati Nzuri Yanga amekuwa akichukua Ubingwa Mapema na akifika huko ni kukalimilisha ratiba tu!
2. Mwaka huu wakaona waanzishe mfumo wa timu 4 zitakazocheza kwenye ngao ya Hisani (Ngao ya Jamii) ili kipenzi Chao Madunduka aweze kubebwa awezavyo achukue ngao hiyo, huu mfumo ni mfumo wa kihuni kwasababu ngao ya Hisani huwa inachezwa mechi moja tu!
Lengo lao lilifanikiwa kwasababu kila mmoja ni shahidi ile fainali namna refa alivyoamua waziwazi kumbeba Dunduka.
3. Haikuishia hapo, mwaka huu wameamua kabisa Yanga acheze mechi ngumu mfululizo ili adondoshe point kusudi kipenzi chao Dunduka aweze kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi nyingi.
Azam vs Yanga
Yanga vs Singida
Simba vs Yanga
Walijua kabisa hapo Yanga hachomoki na ndipo mahali ambapo Dunduka angemzidi Yanga Pointi, lakini hadi sasa hawaamini wanachokiona!
Baada ya Dunduka kukandwa ki kwelikweli wakaamua mechi ya Dunduka na Azam waisogeze mbele hadi Januari bila sababu ya Msingi ili kumbeba Dunduka.
Labda tu niaambie TFF ya Kwamba mtaionea Yanga kwenye mambo mengine lakini kwenye uwanja atawaahibisha tu, dadeeeeeeki!
The Greatest Umughaka A.K.A "River Mbaji".
Ni kama vile Young Africans ni fupa la Sangara ambalo limenasa kwenye kolomeo la zee lenye husda liitwalo "TFF".
Kibaya zaidi fupa hilo limekwama na halimezeki wala halitoleki iwe kwa winchi ama kamba za chuma! Fupa hilo la Sangara linaendelea kuwaumiza viongozi wa TFF na hawana cha kufanya zaidi ya kuendelea kugugumia maumivu!
Miaka 2 ya Ubingwa wa Yanga viongozi wenye chuki na husda ya waziwazi kwa Yanga tumeshuhudia wakifanya fitina za kila namna ili Yanga aside Bingwa lakini imeshindikana.
1. Miaka 2 mfululizo wamekuwa wakimpangia Yanga ratiba ambayo si rafiki, mechi za mwisho za Yanga kwa misimu 2 mfululizo amekuwa akimalizia kule mkoani Mbeya, hii si bahati mbaya, tunajua ni uhuni na fitina ili kuihujumu Yanga lakini bahati Nzuri Yanga amekuwa akichukua Ubingwa Mapema na akifika huko ni kukalimilisha ratiba tu!
2. Mwaka huu wakaona waanzishe mfumo wa timu 4 zitakazocheza kwenye ngao ya Hisani (Ngao ya Jamii) ili kipenzi Chao Madunduka aweze kubebwa awezavyo achukue ngao hiyo, huu mfumo ni mfumo wa kihuni kwasababu ngao ya Hisani huwa inachezwa mechi moja tu!
Lengo lao lilifanikiwa kwasababu kila mmoja ni shahidi ile fainali namna refa alivyoamua waziwazi kumbeba Dunduka.
3. Haikuishia hapo, mwaka huu wameamua kabisa Yanga acheze mechi ngumu mfululizo ili adondoshe point kusudi kipenzi chao Dunduka aweze kuongoza ligi kwa tofauti ya pointi nyingi.
Azam vs Yanga
Yanga vs Singida
Simba vs Yanga
Walijua kabisa hapo Yanga hachomoki na ndipo mahali ambapo Dunduka angemzidi Yanga Pointi, lakini hadi sasa hawaamini wanachokiona!
Baada ya Dunduka kukandwa ki kwelikweli wakaamua mechi ya Dunduka na Azam waisogeze mbele hadi Januari bila sababu ya Msingi ili kumbeba Dunduka.
Labda tu niaambie TFF ya Kwamba mtaionea Yanga kwenye mambo mengine lakini kwenye uwanja atawaahibisha tu, dadeeeeeeki!
The Greatest Umughaka A.K.A "River Mbaji".